< San Mateo 24 >

1 YA si Jesus jumuyong gui templo ya mapos; manmato y disipuluña sija, para umafanue ni y mafatinas y templo.
Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
2 Si Jesus jaope sija, ilegña: Ti inlie todo estesija? Magajet jusangane jamyo, na ti umapolo güine un acho gui jilo otro acho, na ti umayulang.
Yesu akawaambia, “Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
3 Ya anae matatachong güe gui sabana Olibo, manmato guiya güiya y disipulo sija, ya ilegñija: Sangane jam ngaean ufanjuyong estesija na güinaja, yan jafa taemano na señat y finatomo, yan y jinecog y tiempo? (aiōn g165)
Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?” (aiōn g165)
4 Ya maninepe as Jesus, ilegña: Adaje ya chamiyo fanmadadague ni jaye.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5 Sa megae ufanmato pot y naanjo, ya ujaalog: Guajo si Cristo; ya megae ujadague.
Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
6 Ya infanmanjungog guera yan sinangan nu y guera; atan ya chamiyo ninafañachatsaga; sa nesesita na todo este ufanjuyong, lao trabia ti y jinecog.
Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7 Sa ufangajulo nasion contra nasion, yan raeno contra raeno; ya uguaja ñinalang yan linao gui lugat sija.
Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
8 Ya todo este sija na güinaja y tutujon y pininite.
Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9 Ayo nae infanmaentrega para infanmanapute, ya infanmapuno; ya infanmachatlie gui todo nasion pot y naanjo.
“Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
10 Ya megae innafanmatompo; ya ufanaentrega unos y otros, ya ufanachatlie unos y otros.
Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
11 Ya megae ti manmagajet na profeta ufangajulo, ya ujadague megae.
Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
12 Ya pot y janamegae y tinaelaye, y güinaeyan y megae janamanenggeng.
Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
13 Lao y sumungon asta y jinecog, este usatba.
Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.
14 Ya umapredica este y ebangelion y raeno gui todo y tano, para testimonio gui todo y nasion, ya ayo nae ufato y jinecog.
Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
15 Enaomina an inlie y chinatlie y inginon na yinilang, ni y jasangan si Daniel profeta ni tumotojgue gui santos na lugat; (y tumataetae güiya utungo).
“Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
16 Ayo nae y mangaegue guiya Judea, manmalago para y taquilo na jalomtano;
hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.
17 Ya y gaegue gui jilo atof, ti ufanunog ya ujachule jafa gui guimaña;
Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
18 Ya y gaegue gui fangualuan, ti ufanalo tate ya ujachule y magagoña.
Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
19 Lao ay ay para y manmapotgue, yan y mannanasuso, güije na jaane!
Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
20 Fanmanaetae, sa y jinanaonmiyo, munga gui tiempon manenggeng ni y sabado.
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
21 Sa ayo na tiempo uguaja dangculo na pininite, ya desde y tutujon y tano asta pago, taya nae guaja; ya taya mas na uguaja asta jinecog.
Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
22 Yaguin ayo na jaane sija ti manafangadada, ni un catne usiña ninalibre; lao pot y manmaayig, ayo sija na jaane umanafangadada.
Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23 Yaguin jaye na taotao umalog nu jago: Estagüe si Cristo, pat ayo; chamo jumojonggue.
“Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
24 Sa ufangajulo y ti manmagajet na Cristo yan ti manmagajet na profeta sija; ya ufanmamanue dangculo na señat sija, yan mannamanman, ya, yaguin siña, ujadagueja asta y manmaayig.
Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
25 Estagüe na jusangane jamyo antes.
Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.
26 Yaguin ilegñija nu jamyo: Estagüe na gaegue güi desierto, chamo jumajanao; pat, Estagüe, na gaegue gui sanjalom gui cuatto, chamo jumojonggue.
Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
27 Sa calang y lamlam ni y jumuyong gui sancatan, ya manina gui sanlichan, taegüijija locue y minamaela y Lajin taotao.
maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
28 Sa manoja nae mañaga y tataotao y matae, ayo locue nae ufandaña y aguila sija.
Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29 Ti apmam despues di y pininiten ayo sija na jaane, y atdao ujomjom, ya y pilan ti ufanina; ya y pution sija ufamodong guine y langet; ya y nina siñan y langet ufanmayengyong.
“Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
30 Ayo nae uanog señat y Lajin taotao gui langet; yan ayo nae ufanugung todo y tribu sija gui tano; ya ujalie y Lajin taotao na mamamaela gui jilo y mapagajes sija gui langet, yan y ninasiñaña yan y dangculon minalagña.
Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
31 Ya utago y angetña sija yan y dangculo na catin y trompeta ya ujanadaña y inayigñija guine y cuatro manglo, desde y un punta gui langet asta y otro.
Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
32 Tingo y acomparasion y trongcon igos. Yanguin y ramasña mañaña ya manjagon, intingo na jijot y fañomnagan.
“Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33 Taegüenaoja locue jamyo, yaguin inlie todo este sija na güinaja, intingoja na esta jijot gui petta sija.
Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
34 Magajet jusangane jamyo, na ti ufanmalofan este na generasion, asta qui todo este sija na güinaja manmacumple.
Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
35 Y langet yan y tano ufanmalofan; lao y sinanganjo sija ti ufanmalofan.
Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 Lao ayo na jaane yan ayo na ora, taya tumungo, ni y angjet sija gui langet ni y Lajiña, na y Tatajoja.
“Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
37 Lao calang y jaanin Noe, taegüijija locue y minamaela y Lajin taotao.
Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
38 Sa ayo na jaane sija y antes di y dilubio, estaba mañochocho yan manguiguimen, ya manasagua, yan manafanaasagua, asta ayo na jaane anae jumalom si Noe gui atca,
Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
39 Ya ti jatungo asta qui mato y dilubio, ya manchinile todos sija; taegüijija locue y minamaelan y Lajin taotao.
Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
40 Ya ayo na jaane uguaja dos gui fangualuan; y uno umacone, ya y otro umapolo:
Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
41 Dos palaoan manguguleg gui mitate; y uno umacone, y ya otro umapolo.
Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
42 Fanbela sa ti intingo jafa na jaane nae ufato y Señotmiyo.
Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
43 Tingo este na yaguin y gaeguima jatungo ngaean nae ufato y saque, ubelagüe, sa ti upolo na umayulangguan ni iyasija.
Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
44 Enao mina jamyo locue fanlisto, sa y Lajin taotao ufato güije na ora gui anae ti injajaso.
Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
45 Jaye y tifáfababa yan y malate na tentago, ni y señotña ninamagasgüe gui guimaña, para uninanae sija nañija gui tiempo?
Yesu akaendelea kusema, “Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
46 Dichoso ayo na tentago, yaguin mato y amuña ya sineda jafatitinas taegüije.
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47 Magajet jusangane jamyo, na uninamagasgüe todo gui iyoña.
Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48 Lao yaguin ayo y taelaye na tentago ilegña gui corasonña: Y amujo ufato atrasao;
Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
49 Ya sigue di janafanlamen y mangachongña, y chumochocho yan gumiguimen yan y manbeglacho:
kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50 Y señot ayo na tentago ufato güije na jaane gui anae ti jananangga yan y ora ni ti jatungo,
bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51 Ya uyenajo güe ni latigo yan ufinanue ni y patteña yan hipocrita sija ayo nae uguaja tumanges, yan chegcheg nifen.
Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.

< San Mateo 24 >