< Lucas 23 >

1 Y se ardiñó sari ocola sueti, y lo lligueráron á Pilato.
Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2 Y se chitáron á acusarle, penando: A ocona terelamos alachado pervirtiendo á amari sueti, y vedando platisarar jayere á Cæsar, y penando que ó sinela Christo Crallis.
Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
3 Y Pilato le puchabó, y penó: ¿Sinelas tucue o Crallis es Chuti? Y ó le rudeló penando: Tucue lo penelas.
Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
4 Penó Pilato á os Manclayes es Erajais, y á la sueti: Chichi, sos sinela choro alachelo andré ocona manu.
Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
5 Tami junos insistian, penando: Terela alborotado a sueti sat la beda, sos chibela por sari la Judéa, comenzando desde o chim de Galiléa, disde acoi.
Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
6 Pilato, sos juneló penar Galiléa, puchabó si sinaba de Galiléa.
Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
7 Y pur chaneló, que sinaba e jurisdicion de Herodes, lo bichabó á Herodes: sos al chiros socababa tambien andré Jerusalém.
Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8 Y Herodes pur dicó á Jesus, se alendó baribu. Presas de baribu chiros le terelaba camelado dicar, presas habia junelado penar de ó barias buchias, y fronsaperaba dicarle querelar alguno zibo.
Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9 Le quereló pues baribustrias preguntas: Tami ó le rudelaba chichi.
Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10 Y sinaban os Manclayes es erajais, y os Libanes acusandole silamente.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 Y Herodes sat desqueres jundunáres ó despreció: y caquerandole le quereló chitar yeque conel parno, y aver begai o limbidió á Pilato.
Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12 Y ocola chibes se quereláron monres Herodes y Pilato; presas palal sinaban daschmanuces entre sí.
Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13 Pilato pues araqueró á os Manclayes es erajais, y á os Barandéres, y á la sueti.
Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14 Y les penó: Terelais lanelado á mangue ocona manu, sasta pervertidor e sueti; y diquelad que puchabándole menda anglal de sangue, na alaché andré ocona manu yeque de ocolas buchias chorias de que o acusais.
akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15 Ni Herodes Crallis: presas sangue bichabé á ó, y he acoi que se ha probisarado chichi, sos merezca meripen.
Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16 Y andiar le despandaré despues de terelar curado.
Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
17 Y debisaraba despandarles yeque estardo andré o chibes e fiesta.
Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18 Y sari a sueti diñó goles catanés, penando: Querelad merar a ocona, y despandanos á Barrabás.
Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
19 Ocona habia sinado bucharado andré l’estaripel por yeque sedicion ardiñada andré o foros, y por yeque mordipen.
(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20 Y Pilato les chamulió de nuevo, camelando despandar á Jesus.
Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21 Tami junos limbidiaban á diñar goles, penando: A la trijul con ó, A la trijul con ó.
lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22 Y ó a trincha begai les penó: ¿Pues qué choro ha querdi ocona? Menda na alachelo andré ó necautia causa de meripen: le curelaré pues y le despandaré.
Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
23 Tami junos insistian mangando á goles bares, que sinase trijulado, y ardiñaban butér sus goles.
Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24 Y Pilato penchabó, que se querelara ma junos mangaban.
Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25 Y les despandó á ó sos por sedicion, y mordipen habia sinado bucharado andré l’estaripel, al sos habian mangado: y entregisaró á Jesus á las bastes de junos.
Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26 Y pur lo lligueráron, ustiláron yeque manu de Cyrene, sos se hetó Simón, sos abillaba de yeque cosque: y le carguisaráron la trijul, somia que la lliguerase palal de Jesus.
Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27 Y le plastañaban yeque plastañi bari de sueti, y de cadchias, sos le plañian y orobaban.
Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28 Tami Jesus? límbidiandose hacia siras, les penó: Dugidas de Jerusalém, na orobeis opré mangue; antes orobad opré jirias matejas, ta opré jires chaborés.
Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29 Presas abillarán chibeses andré que penarán: Majaradas as estériles, y as porias, sos na concibiéron, y as chuchai sos na diñáron de mamisarar.
Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30 Entonces se chibarán á penar á as playas: Perad opré amangue: y á os bures: Ucharadnos.
Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31 Presas si andré carschta bardry querelan ocono, ¿andré a seca, que se querelará?
Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
32 Y lligueraban tambien sat ó dui averes, sos sinaban chores, somia mulabarlos.
Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33 Y pur bigoreáron á o stano, sos se heta de la Calavéra, le trijuláron oté; y os dui randés, yeque á la bastari, y aver á la can.
Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34 Tami Jesus penaba: Dada, ojabesalos: presas na chanelan, ma querelan. Y dividiendo desqueres talalorés, bucháron sustirias.
Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35 Y a sueti sinaba dicando, y os Manclayes catanamente sat junos o denostabelaban, y penaban: A averes chibó lacho, listrabese á sí matejo, si ocona sinela o Christo, o camelado de Debél.
Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
36 Le caqueraban tambien os jundunares, chalando sunparal á ó, y chitandole anglal vinagre.
Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37 Y penando: Si tucue sinelas o Crallis es Chuti, listrabelate á tun matejo.
wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 Y sinaba opré ó yeque titulo libanado andré letras Griegas, Latinas y Ybuchias: Ocona sinela o Crallis es Chuti.
Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
39 Y yeque de ocolas randes, sos sinaban luanados, o injuriaba, penando: Si tucue sinelas o Christo, listrabela á tun matejo, y á amangue.
Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
40 Tami o aver rudelando, le chingaró, penando: Ni aun tucue canguelas á Debél, sinando andré a mateja corypény?
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41 Aromali amangue urgiyamos por amaro grecos, presas ustilamos ma merecen amarias obras: tami ocona chichi choro ha querdi.
Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42 Y penába á Jesus: Erañó, enjallate de mangue pur abillares á tun chim.
Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
43 Y Jesus le penó; Aromali te penelo, que achibes sinarás con-a-mangue andré o Paraiso.
Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
44 Y sinaba ya casi a ocana zobia, y sari a chiquen se ucharó de tinieblas disde a ocana nubia.
Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45 Y se chitó oruné o Cam: y o velo e cangri se asparabó pré medio.
na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46 Y Jesus diñando yeque gole baro, penó: Dada: andré tirias bastes encomiendo minrio ylo: y penando ocono, espiró.
Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47 Y pur dicó o Centurion ma habia anacado, diñó chimusolano á Debél, penando: Aromali, ocona manu sinaba lacho.
Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
48 Y sari a sueti sos sunparal sinaba, pur dicaba ma anacaba, se limbidiaba curandose andré os chepés.
Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49 Y sares os pincherados de Jesus, y as cadchias sos le habian plastañado de Galiléa, sinaban dicando oconas buchias de dur.
Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50 Y he acoi yeque gacho araquerado Joseph, sos sinaba Barander, gacho lachó ta justo:
Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51 Sos na habia consentido andré o consejo, ni andré os hechos de junos, de Arimathéa, foros e Judéa, sos ujaraba o chim de Debél.
Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52 Ocona bigoreó á Pilato, y le mangó o trupos de Jesus.
Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 Y habiendole nicabado, lo involvisaró andré yeque sabana parni, y lo childó andré yeque sepulchro querdi andré un bur, anduque cayque disde entonces habia sinado childado.
Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54 Y sinaba o chibes de Parasceve, y sunparal sinaba a Canché.
Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55 Y abillando tambien as cadchias sos habian plastañado á Jesus desde Galiléa, dicáron o sepulchro, y a beda en que sinaba childado desquero trupos.
Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56 Y limbidiandose, quináron bus ta unguentes; y reposáron a Canché sasta mandisarela a Eschastra.
Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.

< Lucas 23 >