< Lucas 23 >

1 Y se ardiñó sari ocola sueti, y lo lligueráron á Pilato.
Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
2 Y se chitáron á acusarle, penando: A ocona terelamos alachado pervirtiendo á amari sueti, y vedando platisarar jayere á Cæsar, y penando que ó sinela Christo Crallis.
Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
3 Y Pilato le puchabó, y penó: ¿Sinelas tucue o Crallis es Chuti? Y ó le rudeló penando: Tucue lo penelas.
Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
4 Penó Pilato á os Manclayes es Erajais, y á la sueti: Chichi, sos sinela choro alachelo andré ocona manu.
Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
5 Tami junos insistian, penando: Terela alborotado a sueti sat la beda, sos chibela por sari la Judéa, comenzando desde o chim de Galiléa, disde acoi.
Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
6 Pilato, sos juneló penar Galiléa, puchabó si sinaba de Galiléa.
Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
7 Y pur chaneló, que sinaba e jurisdicion de Herodes, lo bichabó á Herodes: sos al chiros socababa tambien andré Jerusalém.
Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
8 Y Herodes pur dicó á Jesus, se alendó baribu. Presas de baribu chiros le terelaba camelado dicar, presas habia junelado penar de ó barias buchias, y fronsaperaba dicarle querelar alguno zibo.
Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
9 Le quereló pues baribustrias preguntas: Tami ó le rudelaba chichi.
Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
10 Y sinaban os Manclayes es erajais, y os Libanes acusandole silamente.
Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 Y Herodes sat desqueres jundunáres ó despreció: y caquerandole le quereló chitar yeque conel parno, y aver begai o limbidió á Pilato.
Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
12 Y ocola chibes se quereláron monres Herodes y Pilato; presas palal sinaban daschmanuces entre sí.
Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
13 Pilato pues araqueró á os Manclayes es erajais, y á os Barandéres, y á la sueti.
Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
14 Y les penó: Terelais lanelado á mangue ocona manu, sasta pervertidor e sueti; y diquelad que puchabándole menda anglal de sangue, na alaché andré ocona manu yeque de ocolas buchias chorias de que o acusais.
akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
15 Ni Herodes Crallis: presas sangue bichabé á ó, y he acoi que se ha probisarado chichi, sos merezca meripen.
Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
16 Y andiar le despandaré despues de terelar curado.
Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
17 Y debisaraba despandarles yeque estardo andré o chibes e fiesta.
Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
18 Y sari a sueti diñó goles catanés, penando: Querelad merar a ocona, y despandanos á Barrabás.
Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
19 Ocona habia sinado bucharado andré l’estaripel por yeque sedicion ardiñada andré o foros, y por yeque mordipen.
(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
20 Y Pilato les chamulió de nuevo, camelando despandar á Jesus.
Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
21 Tami junos limbidiaban á diñar goles, penando: A la trijul con ó, A la trijul con ó.
Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
22 Y ó a trincha begai les penó: ¿Pues qué choro ha querdi ocona? Menda na alachelo andré ó necautia causa de meripen: le curelaré pues y le despandaré.
Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
23 Tami junos insistian mangando á goles bares, que sinase trijulado, y ardiñaban butér sus goles.
Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
24 Y Pilato penchabó, que se querelara ma junos mangaban.
Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
25 Y les despandó á ó sos por sedicion, y mordipen habia sinado bucharado andré l’estaripel, al sos habian mangado: y entregisaró á Jesus á las bastes de junos.
Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
26 Y pur lo lligueráron, ustiláron yeque manu de Cyrene, sos se hetó Simón, sos abillaba de yeque cosque: y le carguisaráron la trijul, somia que la lliguerase palal de Jesus.
Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
27 Y le plastañaban yeque plastañi bari de sueti, y de cadchias, sos le plañian y orobaban.
Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
28 Tami Jesus? límbidiandose hacia siras, les penó: Dugidas de Jerusalém, na orobeis opré mangue; antes orobad opré jirias matejas, ta opré jires chaborés.
Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
29 Presas abillarán chibeses andré que penarán: Majaradas as estériles, y as porias, sos na concibiéron, y as chuchai sos na diñáron de mamisarar.
Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
30 Entonces se chibarán á penar á as playas: Perad opré amangue: y á os bures: Ucharadnos.
Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
31 Presas si andré carschta bardry querelan ocono, ¿andré a seca, que se querelará?
Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
32 Y lligueraban tambien sat ó dui averes, sos sinaban chores, somia mulabarlos.
Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
33 Y pur bigoreáron á o stano, sos se heta de la Calavéra, le trijuláron oté; y os dui randés, yeque á la bastari, y aver á la can.
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
34 Tami Jesus penaba: Dada, ojabesalos: presas na chanelan, ma querelan. Y dividiendo desqueres talalorés, bucháron sustirias.
Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
35 Y a sueti sinaba dicando, y os Manclayes catanamente sat junos o denostabelaban, y penaban: A averes chibó lacho, listrabese á sí matejo, si ocona sinela o Christo, o camelado de Debél.
Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
36 Le caqueraban tambien os jundunares, chalando sunparal á ó, y chitandole anglal vinagre.
Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
37 Y penando: Si tucue sinelas o Crallis es Chuti, listrabelate á tun matejo.
na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 Y sinaba opré ó yeque titulo libanado andré letras Griegas, Latinas y Ybuchias: Ocona sinela o Crallis es Chuti.
Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
39 Y yeque de ocolas randes, sos sinaban luanados, o injuriaba, penando: Si tucue sinelas o Christo, listrabela á tun matejo, y á amangue.
Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
40 Tami o aver rudelando, le chingaró, penando: Ni aun tucue canguelas á Debél, sinando andré a mateja corypény?
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
41 Aromali amangue urgiyamos por amaro grecos, presas ustilamos ma merecen amarias obras: tami ocona chichi choro ha querdi.
Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
42 Y penába á Jesus: Erañó, enjallate de mangue pur abillares á tun chim.
Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
43 Y Jesus le penó; Aromali te penelo, que achibes sinarás con-a-mangue andré o Paraiso.
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44 Y sinaba ya casi a ocana zobia, y sari a chiquen se ucharó de tinieblas disde a ocana nubia.
Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
45 Y se chitó oruné o Cam: y o velo e cangri se asparabó pré medio.
kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
46 Y Jesus diñando yeque gole baro, penó: Dada: andré tirias bastes encomiendo minrio ylo: y penando ocono, espiró.
Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
47 Y pur dicó o Centurion ma habia anacado, diñó chimusolano á Debél, penando: Aromali, ocona manu sinaba lacho.
Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
48 Y sari a sueti sos sunparal sinaba, pur dicaba ma anacaba, se limbidiaba curandose andré os chepés.
Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
49 Y sares os pincherados de Jesus, y as cadchias sos le habian plastañado de Galiléa, sinaban dicando oconas buchias de dur.
Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
50 Y he acoi yeque gacho araquerado Joseph, sos sinaba Barander, gacho lachó ta justo:
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
51 Sos na habia consentido andré o consejo, ni andré os hechos de junos, de Arimathéa, foros e Judéa, sos ujaraba o chim de Debél.
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
52 Ocona bigoreó á Pilato, y le mangó o trupos de Jesus.
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 Y habiendole nicabado, lo involvisaró andré yeque sabana parni, y lo childó andré yeque sepulchro querdi andré un bur, anduque cayque disde entonces habia sinado childado.
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
54 Y sinaba o chibes de Parasceve, y sunparal sinaba a Canché.
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
55 Y abillando tambien as cadchias sos habian plastañado á Jesus desde Galiléa, dicáron o sepulchro, y a beda en que sinaba childado desquero trupos.
Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
56 Y limbidiandose, quináron bus ta unguentes; y reposáron a Canché sasta mandisarela a Eschastra.
Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

< Lucas 23 >