< Matiyu 2 >

1 kubẹ na iwa maru Yisa ku in Baitalami un Yahudiya nayiri tigoh in Hiridus, amon anitt anan yiru yenju niyini kusari kitene nin Urushalima da ida woro,
Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
2 Adin weri ulenge na ina marughe ugoh na Yahudawe? Tina yene fiyini mere kusari kitene unnare ti da tida zazinghe.”
wakauliza, “Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu.”
3 Na ugoh Hiridus in lanza nani, ayi me nin na nitin Urushalima fita vat.
Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
4 Hiridus pitirino a didya na Priest nin na nan ninyerte nanit vat kiti kirum, anin tirino nani, “Nweri ima Kristi ku?”
Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, “Kristo atazaliwa wapi?”
5 I woro ghe nenge, “In Baitalamin Yahudiya, bara imon ile na nyan lirun nuu Kutullẹ na nyertin nari ine,
Nao wakamjibu, “Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
6 'A fe, ubaitalami, in myin Yahudiya, na fere ubene nan nya na nan bun Yahudiya, nani nan nya fere unan tigo ba nuzukuulenge na ama su libya nanit nig Israila.'”
Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli.”
7 Hiridus tunna ayicila anan yiru vat likire a tirino nani in dert kubi kongo na fiyine na nuzu.
Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
8 A to nani udu ubaitalahmi, a woro, “Can idi piziru ubeleng gono seng. Asa i se ghe, dan ida belli, bara meng wang nan do in di zazinghe.”
Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, “Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu.”
9 Na i lanza ugowe ku, i kiffo libau i nya, fiyine na ini yene kusari kitene tunna ncin nbun mine fidi duru fiyisina kiti kirum dert kiti kanga na gọnọ diku.
Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
10 Na iyene fiyinie, isu ayi abo nin liburi libo kang.
Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
11 Itunna ipira nan nya kilare iyene gone nin nene Maryamue. Itumuno izazin ghe. Itunna i puzuno tika mine i nakpaghe imon ile na i ming mun, izinariya, lubban a kwul.
Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
12 Na ise uwannu nataf kiti Kutellẹ nan nya namorona iwa kpilin kitin Hiridus ba, ifita i yira nlong libau ugang ukpillu kipin mine.
Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
13 Na inung nna nya, Gono kadura Kutellẹ tun na a da kitin Yusufu nan nya namoro, a woroghe, “Fita uyiru gono, kinesse nin nene urum udu uMasar, udi so kikane se kubi kongo na mbellin fi uliru bara na Hiridus ma pizuru gone a molu kining.”
Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto.”
14 A tunna nin kitik ka ne afita a yauna ggono kinesse nin nene inya mun ucindu umasar.
Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
15 Awa di so kikane udi duru kubin nkul in Hiridus, ulire nan kulo na cikilare wa bellin kitin nnan liru nin nuu Kutellẹ, “Unuzun nan nyan Masar nna yicila usaun ning ku.”
Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: “Nilimwita Mwanangu kutoka Misri.”
16 Na Hiridus iyene anitt ayinjing ane nrusuzo ghe, ayi nana ghe kang, ato idi molusu nnono ni lirine vat na niwadi in Baitalahmi, udu ligan nminne vat, ucizunu na kus aba utolu kadas nalenge na idurun ba, nafo kubatino kube na awa lanza Ubeleng nan nyan tinu na nit ajinjin ghe.
Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
17 Ulirue u ni wa kulo vilengwe na iwa bellin kitin Irimiya unan liru nin nuuKutellẹ.
Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
18 “I wa lanza liwani nan nyan rama, kuculu nin tiyom a liburi lisirne, Rahilla di kuculu nnono me.”
“Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki.”
19 Na Hiridus nku gono kadura Kutellẹ da kitin Yusufu nan nya namoro in masar.
Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
20 “Aworo, Fita, yauna gono kinesse nin nene, udo nan nyan nmin Israila.”
akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.”
21 Yusufue fita, a yauna gone nin nene, ada nan nya nmin Israila.
Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
22 Na alanza Arkila usari di tigon yahudiya kudarun ncife, Hiridus, fiu kiffo ghe na ado ba, vat nin woru Kutellẹ nwununghe kutuf nan nya namoro, ana lassina udu nmin ngalili.
Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
23 Amini ana wa dak ada da so nkan kipin na idin yiccu kinin unazarati, inan kulo uliru na iwa bellin tinu na nan nliru nnu Kutellẹ ima yiccu ghe kunan Nazarat.
akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.”

< Matiyu 2 >