+ Matiyu 1 >

1 Inyerte tisa kuwunun Yisa Kristi, usaun in Dauda, usaun Ibrahim.
Yesu Kristo alikuwa mzawa wa Daudi, mzawa wa Abrahamu. Hii ndiyo orodha ya ukoo wake:
2 Ibrahim wadi uchifin Ishaku, a Ishaku uchifi Yakubu, a Yakubu uchifin Yahuda nin nuanamẹ.
Abrahamu alimzaa Isaka, Isaka alimzaa Yakobo, Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake,
3 uchifin Parez nin Zaraha unuzun kumantin Tamar, Parez uchifin Hasruna, Hasruna uchifin Arama.
Yuda alimzaa Faresi na Zera (mama yao alikuwa Tamari), Faresi alimzaa Hesroni, Hesroni alimzaa Rami,
4 Arama wa maru Aminadaba ku, Aminadaba mara Nahashuna ku, Nahashuna mara.
Rami alimzaa Aminadabu, Aminadabu alimzaa Nashoni, Nashoni alimzaa Salmoni,
5 Salmuna ku, Saalmuna mara Bu'az ku unuzu kumantin Rahab, Bu'az mara Ubida ku, unuzu kumantin Ruth, Ubida mara Jesẹ ku.
Salmoni alimzaa Boazi (mama yake Boazi alikuwa Rahabu). Boazi na Ruthi walikuwa wazazi wa Obedi, Obedi alimzaa Yese,
6 Jesẹ wadi uchif ngoh Dauda, Dauda mara Solomon ku, unuzun kitin wanin Uriya.
naye Yese alimzaa Mfalme Daudi. Daudi alimzaa Solomoni (mama yake Solomoni alikuwa mke wa Uria).
7 Solomon wadi uchifin Rehoboam, Rehoboam mara Abija ku, Abija mara Asa ku.
Solomoni alimzaa Rehoboamu, Rehoboamu alimzaa Abiya, Abiya alimzaa Asa,
8 Asa mara Jehoshapat, Jehoshapat mara Joram ku, Joram wa maru Uzaya ku.
Asa alimzaa Yehoshafati, Yehoshafati alimzaa Yoramu, Yoramu alimzaa Uzia,
9 Uzaya mara Jotham ku, Jotham wa di uchifin Ahaz, Ahaz mara Hizikiya ku.
Uzia alimzaa Yothamu, Yothamu alimzaa Ahazi, Ahazi alimzaa Hezekia,
10 Hizikiya mara Manasa ku, Manasa mara Amon ku, Amon mara Josaya ku.
Hezekia alimzaa Manase, Manase alimzaa Amoni, Amoni alimzaa Yosia,
11 Josaya mara Jikoniya ku nin nuanẹ kubin kifuzun nonon Israila udumun u Babila.
Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake. Huo ulikuwa wakati Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babuloni.
12 Kimalin kifuzu udu u Babilẹ, Jikoniya mara Shealtiel ku, Shealtiel mara Zarubabel ku.
Baada ya Wayahudi kupelekwa uhamishomi Babuloni: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli alimzaa Zerobabeli,
13 Zarubabel mara Abiud ku, Abiud mara ilayikum ku, Ilayakum mara Azor ku.
Zerobabeli alimzaa Abiudi, Abiudi alimzaa Eliakimu, Eliakimu alimzaa Azori,
14 Azor mara Zadok ku, Zadok wadi uchifin Achim, Achim wadi uchifin Eliud.
Azori alimzaa Zadoki, Zadoki alimzaa Akimu, Akimu alimzaa Eliudi,
15 Eliud wadi uchifin Ileza, Ileza mara Mattana ku, Mattana mara Yakub ku.
Eliudi alimzaa Eleazeri, Eleazeri alimzaa Mathani, Mathani alimzaa Yakobo,
16 Yakub mara Yusufu ku, ulessin Maremu ulenge na awa maru Yisa ku unuzu kitene, ulenge na idin yicighe Kristi.
Yakobo alimzaa Yosefu, aliyekuwa mume wake Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
17 Vat naji aji uyiru kitin Ibrahim udak kubin Dauda aji likure nin na nassari, uyiru kubin Dauda udu kubi ko na iwa yiru nani udu u Babila aji likure nin na nassari.
Basi, kulikuwa na vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi mpaka Wayahudi walipochukuliwa mateka Babuloni, na vizazi kumi na vinne tangu kuchukuliwa mateka mpaka wakati wa Kristo.
18 Kumanti Yisa Kristi wadi nafo nengenari. Unene Maremu wa yiinnin aba su ilugma nin Yusufu, a na isa su ilugma ba iseghe nin liburin in Fip Kutellẹ.
Basi, hivi ndivyo Yesu Kristo alivyozaliwa: Maria, mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla hawajakaa pamoja kama mume na mke, alionekana kuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
19 Ulesse Yusufu wadi unan fiu Kutellẹ, na awa di nin su a nighe ncin nan nya nanit ba. Bara nani awa di nin su asughe likire.
Yosefu, mumewe, kwa vile alikuwa mwadilifu, hakutaka kumwaibisha hadharani; hivyo alikusudia kumwacha kwa siri.
20 Na awa di kpilizu ni leli imone, unan kadura Kutellẹ da kitime nan nya namoro, aworo, YUsufu, uusaun Dauda, na uwa lanza fiu in woru uyiru Maremu ku a so uwanife ba, bara fisudu fo na fidi nanya liburi me unuzu kitin Ruhu ulauwari.
Alipokuwa bado anawaza jambo hilo, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akamwambia, “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, maana amekuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
21 Ama maru gono, uma yichu lisame Yisa, bara amma tuchu anit me nanya nalapi mine.”
Atajifungua mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu, kwa kuwa yeye atawaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”
22 Vat nilele wase bara inan kulo imon ile na Cikilari wa belli nnu nanan liru nin nu me, a woro.
Basi, haya yote yalitukia ili litimie lile neno Bwana alilosema kwa njia ya nabii:
23 “Yenen kubura ma ti liburi kumaru gono, ima yicu lisame immanuel, uninare Kutellẹ ligowe nan ghirik.”
“Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kiume, naye ataitwa Emanueli” (maana yake, “Mungu yu pamoja nasi”).
24 Yusufu fita nanyan moro me asu nafo na unan kaduran Cikilare na bellinghe, ayira Maremmu ku aso uwanime.
Hivyo, Yosefu alipoamka usingizini alifanya kama malaika huyo alivyomwambia, akamchukua mke wake nyumbani.
25 Nanya nani iwa so lisosin nless nin wanii, na izuro ba udu kubi kongo na awa maru. A na lisan gone Yisa.
Lakini hakumjua kamwe kimwili hata Maria alipojifungua mtoto wa kiume. Naye Yosefu akampa jina Yesu.

+ Matiyu 1 >