< 2 Ukorintiyawa 12 >

1 Dole in foo figir, bara nani na mma se imong ku b, bara nani unuzu ina tiubun namoro nin belu nanya unuzun Cikilari.
Yanipasa nijisifu, ingawa haifaidi kitu. Nitaenda kwenye maono na ufunuo kutoka kwa Bwana.
2 Inyiru unit nanya Kristi nanya na kus tkure min nanase na ana kata sa nanya kidawo sa indas kidaw, nan meng yiru ba Kutelle yiru iwa yanghe udu nanya kitime kin taat.
Namjua mtu mmoja katika Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alichukuliwa juu hadi mbingu ya tatu. Kama ni katika mwili au nje ya mwili, sijui, Mungu ajua.
3 Tutung inyiru umong unit sa naya kidawo sa indas kidawo, na meng yiru ba Kutelle yiru.
Nami najua ya kwamba mtu huyu, kwamba ni katika mwili au nje ya mwili mimi sijui, lakini Mungu ajua,
4 ulena iwa yonghe udu kitene ule na awa di nin imong ilau kang na umon wasa a benle ba.
alinyakuliwa hadi Paradiso. Huko alisikia mambo yasiyoelezeka, mambo ambayo binadamu hana ruhusa ya kuyasimulia.
5 Kitenen leli unitere men ma foo figiri. Bara na nma foo figiri nin litinin ba se dei bara lidarni ning.
Nitajisifu kwa ajili ya mtu kama huyo, lakini sitajisifu kuhusu mimi mwenyewe ila mimi nitajisifia udhaifu wangu.
6 Andi indinin su in foo figiri. nan ma suo ulalan ba, bara idin belu kidegenere. Bara nani ima cinu ufoo figiri nanumon ba kpilizinu litinighe gbardan, na nafo idin yenju sa idin lanzuyi ba.
Hata kama ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga, kwa maana nitakuwa nasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu yeyote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.
7 Sa bara na mgbardan inda ciu mbele. Baranani na mma fiwu aba da nin fiwu liti ba i wa tiyifimat kidowo, kadura nnuzu shidtan idak ida firume, bara nwa foo figiri kang.
Ili kunizuia nisijivune kwa sababu ya ufunuo huu mkuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mjumbe wa Shetani, ili anitese.
8 Njun tat ina foo acara nin kiti Kutelle akalai mung ile imone nanya nin
Kwa habari ya jambo hili nilimsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu.
9 Amini na beli “ubolu nin batin fi” Bara na likara din kue naanya lidarne” too mma kpinu ufoo figiri nanya nanya lidarni ning bara likaara Kristin soo kitene ning
Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uweza wangu hukamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
10 Bara nani ubatine bara Krist, nanya lidarni, nanya nitop nnya nniy, nanya tinana nayii, nanya nkunekun, bara nani vat kubi kone diri likar, asa nta agang.
Hii ndiyo sababu, kwa ajili ya Kristo, nafurahia udhaifu, katika kutukanwa, katika taabu, katika mateso na katika shida, kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo nina nguvu.
11 In nasoo ulalan! anunghere natiy, bara anunghere wa ruyi, bara na nwa di ko cun kadas nang nadidiya nansn kadura ba barana mmen imonghari ba
Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ilinipasa kusifiwa na ninyi, kwa sababu mimi si dhalili kuliko wale “mitume walio bora,” ingawa mimi si kitu.
12 Kidegen nalap nan kadura wadi kiti mine nin nayashau vat, alap nin nalajibi nin nitwa ni didiya.
Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani, ishara, miujiza na maajabu, yalifanywa miongoni mwenu kwa saburi nyingi.
13 Bara na anung wadi iyiziari sa uanpani nafo nzisin natii alauw, bara na uwa so minu kutura ba? shawang ninmile utanue!
Je, ninyi ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila tu kwamba mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili!
14 Yeneng! Mba dak minu tutung unta, na ima lawu minu kutura ba bara na idinin su ni mong mine ba anunghere ndi nin suw. Nanono ba cisu bara acife ba bara nani acifari ba cisu bara n nono.
Sasa niko tayari kuja kwenu kwa mara hii ya tatu, nami sitawalemea, kwa sababu sitahitaji chochote chenu, ila ninawahitaji ninyi, kwa kuwa hata hivyo watoto hawaweki akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi huweka akiba kwa ajili ya watoto wao.
15 Nna yitu nin nayi abo kang in wultun bara anunghe uwa biiu usumine kang, ita usu ninghe baata?
Hivyo nitafurahi kutumia kila kitu nilicho nacho kwa ajili yenu, hata mwili wangu pia. Hata ingawa inaonekana ninavyozidi kuwapenda, ndivyo upendo wenu kwangu unavyopungua.
16 Bara na udi nani, nanan ti minu kutura nati ba. Bara na meng di jinjin, mere na fo minu nin kinu.
Iwe iwavyo, kwa vyovyote vile mimi sikuwalemea. Lakini kwa mimi kuwa mwerevu naliwapata.
17 In wa di kitene mine na uwa tuu umong udak kiti mine.
Je, nilijipatia faida kwa kumtumia mtu yeyote niliyemtuma kwenu?
18 Iwa ti Titus ku adak kiti mine inin tuu kani gwane ninghe, Titus se wa di kitene mine? Na tiwa cinu libau lirumme baa? Na tiwa cinuu nin niti nirume ba?
Nilimshawishi Tito aje kwenu, nami nilimtuma pamoja na ndugu yetu. Je, Tito aliwatumia ninyi ili kujipatia faida? Je, hatuenendi kwa roho moja, na hatuchukui hatua zile zile?
19 Idin cisu kokube tidin sesu atibite kiti mine? Nbun Kutelle tidin nin Kristi mbelu vat nimon bara uke minere.
Je, mmekuwa mkifikiri kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu? Sisi tumekuwa tukinena mbele za Mungu kama wale walio katika Kristo. Na chochote tufanyacho, ndugu wapendwa, ni kwa ajili ya kuwatia nguvu.
20 Idin cun fiu nwa dak nan mase minu nafo na idinin suwe, Na anung wang masai nafo na idinin suwe ba, au ti wase mayardang inshina nayi usu liti kubellum, ufoo figiri nin salin caunu.
Kwa kuwa nina hofu ya kwamba nitakapokuja naweza kuwakuta nisivyotaka, nanyi mkanikuta msivyotaka. Nina hofu kwamba panaweza kuwa na ugomvi, wivu, ghadhabu, fitina, masingizio, masengenyo, majivuno na machafuko.
21 Indin lanzu fiu nwa kpilin, Kutelle nighe uruu nighe kiti mine, mma nin gilu bara mgbardan mine naina malu ti kulapi nin burnu na inin na pizeru usunu nsalin lau nin nuzu nin na wani a hem nin su nimong nyi na iwadi isuzu ba.
Nina hofu kwamba nitakapokuja tena kwenu, Mungu wangu atanidhili mbele yenu, nami nitasikitishwa na wengi waliotenda dhambi mbeleni, na wala hawajatubu kwa uchafu wao, uasherati, na ufisadi walioushiriki.

< 2 Ukorintiyawa 12 >