< 1 Ukorintiyawa 9 >

1 Na meng in shutu ba? Na Meng gono katawari ba? Na Meng wa yene Yisa Cikilari bite ba? Na anug hère katuwa nacara nighere nan nya Ncikilari ba?
Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana?
2 Andi na Meng gono kadurari kiti namon ba, ai kiti mine ndi, bara anughere ba dursu annit meng gono kadura, nan nya Ncikilari.
Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni mhuri wa utume wangu katika Bwana.
3 Ulelere ukesu kiti nale nge na udi dumu zuni.
Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu.
4 Na arike nwanya tileoti sono ba?
Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5 Na wanya yira awani ba anan nyinnu Kutellẹ nafo kagisin nanan kadura, nin nuwana nan nya Ncikilari ame Bitrus.
Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini, kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana na Kefa?
6 Sa Barnabas nin mi arikere ba su katuwa casa?
Au ni mimi na Barnaba tu inatubidi kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?
7 Ghari di katuwa nafo kusoja, ame leo nin litime? Ghari ba bilisu imon nan nya a wanya aleo ba? Sa Ghari basu libiya ninab sa uwuru asonu madare?
Ni askari yupi aendaye vitani kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye shamba la mizabibu na asile matunda yake? Ni nani achungaye kundi na asipate maziwa yake.
8 Ndi belle ule imone bara likara nnit usurne? Na uduka bellin nano ba?
Je, nasema mambo haya katika mtazamo wa kibinadamu tu? Je, sheria haisemi vivyo hivyo?
9 Nafo na udi ninyerte nduka Musa, “Yenje uwa tursu fina unu kubi na adi katuwa kunen nileo.” Kidege innari cas Kutellẹ min nania?
Kwa maana imeandikwa katika Sheria ya Mose: “Usimfunge maksai kinywa apurapo nafaka.” Je, Mungu hapa anahusika na ngʼombe?
10 Na ame din nliru kitene bite ba? Iwa nyertin bara arikere, bara ulle na adi nikawa na asu nin ti kibinai, unan su kinorso na asu nin ti kibinai nworu aba se kubi ngirbe.
Je, Mungu hasemi haya hasa kwa ajili yetu? Hakika yameandikwa kwa ajili yetu, kwa sababu mtu anapolima na mpuraji akapura nafaka, wote wanapaswa kufanya hivyo wakiwa na tumaini la kushiriki mavuno.
11 Asa ti bilisa imon Ruhu nanya mine, uba yitu gbardang kagha arike nwase imon lisosin nye kiti mine?
Je, ikiwa sisi tulipanda mbegu ya kiroho miongoni mwenu, itakuwa ni jambo kubwa iwapo tutavuna vitu vya mwili kutoka kwenu?
12 Andi amon di pirizu imon na idi imine kiti mine, na arike dumun nile na ikatin ba? Na nanere ba, na tina se ileli imone ba. Tima teru ayi bara ti wa wantin uliru nlai Kristi.
Kama wengine wana haki ya kupata msaada kutoka kwenu, isingepasa tuwe na haki hiyo hata zaidi? Lakini sisi hatukutumia haki hii. Kinyume chake, tunavumilia kila kitu ili tusije tukazuia Injili ya Kristo.
13 Na anug yiru ba nworu allenge na idin su katuwa kutyin nlira iba se imonli mine kutyin nlire? Inung alle na idi katuwa kitene nbadagi, adi nli imonli me kikene bagade?
Je, hamjui kwamba, watu wafanyao kazi hekaluni hupata chakula chao kutoka hekaluni, nao wale wahudumiao madhabahuni hushiriki kile kitolewacho madhabahuni?
14 Nanere, Kutellẹ wa ni uduka aworo ulle na adin bellu nlai, iba se imonli me kiti nbellu nliru nlai.
Vivyo hivyo, Bwana ameamuru kwamba wale wanaohubiri Injili wapate riziki yao kutokana na Injili.
15 Vat nin nani, nan nsa se imomon nanya nile imone vatt ile imone bara inan su menku imomon ba, ukatin nku nin nworo anung yene ufo figiri nighe so uhem.
Lakini sijatumia hata mojawapo ya haki hizi. Nami siandiki haya nikitumaini kwamba mtanifanyia mambo hayo. Heri nife kuliko mtu yeyote kuninyima huku kujisifu kwangu.
16 Asa ndin bellu uliru nlai, na nile imon na iba fo figiri ba, bara ikifoi nsu nani, kash nin mi asa na nbelle uliru a nlai ba.
Lakini ninapohubiri Injili siwezi kujisifu maana ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipoihubiri Injili!
17 Bare nwa su illenge imone nani nin kibinai kirum, mba seru ulada andi na nin kibinai kirum ba ndu nin katuwa kanga na iwa nie.
Nikihubiri kwa hiari, ninayo thawabu. Lakini kama si kwa hiari, basi ninachofanya ni kutekeleza tu uwakili niliowekewa.
18 Iyaghari ulada nighe? nworu uwa bellu uliru nlai meng ba ni uliru nlai sa useru nimomon, nan baseru ile imon na nyene inaghari nanya nliru kulelle.
Basi je, thawabu yangu ni nini? Thawabu yangu ni hii: Ya kwamba katika kuhubiri Injili niitoe bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.
19 Bara nani meng shutu na cara na nit vat, nlawa kucin kiti nanit vat, bara nnan wunno annit vat.
Ingawa mimi ni huru, wala si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya kuwa mtumwa wa kila mtu, ili niweze kuwavuta wengi kadri iwezekanavyo.
20 Kiti na yahudawa so nafo kuyahudawa, bara nna wuno ayahudawa, kiti na ilenge na imin nduka, nso nafoo allenge na imin (vat nin nani, na meng min ushara ba) nnan wunun alle na imnin ushara.
Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi. Kwa watu wale walio chini ya sheria, nilikuwa kama aliye chini ya sheria (ingawa mimi siko chini ya sheria), ili niweze kuwapata wale walio chini ya sheria.
21 Kiti nale na isali nin nshara, meng wan so nafo unan nsalin nshara. (na Meng litinighe na nta unan nsalin nshara ba kiti Kutellẹ ndi nanya nduka Kristi) nnan wunno alle na isali nan nya nshara.
Kwa watu wasio na sheria nilikuwa kama asiye na sheria (ingawa siko huru mbali na sheria ya Mungu, bali niko chini ya sheria ya Kristo), ili niweze kuwapata wale wasio na sheria.
22 Kiti nan nsali likara, meng so unan sali likara anan sali likara nso imon vat kiti anit vat bara ko niyagh Meng tucu among.
Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niweze kuwapata walio dhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia yoyote niweze kuwaokoa baadhi yao.
23 Nchin su imon vat bbara ubellen nliru Kutellẹ, bara Meng ma nan se upiru nan nya imari me.
Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake.
24 Na anung yiru nwo nanyan cum vat anang cume din su ucume, ama waseme minere asa asere uduke? Bara nani sun ucum ilii uduke.
Je, hamjui kwamba katika mashindano ya mbio wote wanaoshindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu apewaye tuzo? Kwa hiyo kimbieni katika mashindano kwa jinsi ambavyo mtapata tuzo.
25 Unan katwa ncum din zulu kidowo me ayita nin minu nnu nanyan vat nzulu kidowo me. Inung dinsu iseru uduk ulenge na udin nanuzu, ama arik din cum tinan seru uduk un salin nanuzu.
Kila mmoja anayeshiriki katika mashindano hufanya mazoezi makali. Wao hufanya hivyo ili wapokee taji isiyodumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata taji idumuyo milele.
26 Bara nani, na meng din cum sa ukpiluzu ba a na ndas libau nfunu ba.
Kwa hiyo mimi sikimbii kama mtu akimbiaye bila lengo, sipigani kama mtu anayepiga hewa,
27 Ama meng kifu kidowo ning nning ta kinin kucin, bara kimalin wazi ninghe kiti namong, na meng wang iwa nazue mung ba.
la, bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha ili nikiisha kuwahubiria wengine, mimi nisiwe mtu wa kukataliwa.

< 1 Ukorintiyawa 9 >