< Ulusetulilo 17 >

1 Jumo ughwa vanyamola lekela lubale alyale ni fitasa fiila lekela lubale akisa na pikum'bula, “Isa, nikukusona uluhighilo lwa mbwafu u m'baha juno ikukala mumalenga minga,
Mmoja wa malaika saba aliyekuwa na vitasa saba alikuja na kuniambia, “Njoo, nitakuonesha hukumu ya kahaba mkuu akaaye juu ya maji mengi,
2 juno ava tua va iisi vavombile naghwoope isa vuvwafu na muluhuje lwa muvuvwafu vwa mweene vano vikukala mu iisi vaghalile.”
ambaye wafalme wa nchi wamefanya mambo ya uzinzi naye na juu ya mvinyo wa uzinzi wake wakaao duniani wameleweshwa.”
3 Umunyamola akanoola mu mepo mpaaka kulukuve, nilya m'bwene u mwana mama ikalile pakyanya pa ng'anu indangali juno amemile amatavua agha nyamaligho. Ing'anu jilyale na maatu lekela lubale namapembe kijigho.
Malaika akanichukua katika Roho mpaka nyikani, na nilimwona mwanamke amekaa juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya matukano. Mnyama alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
4 Umwana mama alyafwasivue amenda gha sambalau ni ndangali apambilue ni sahabu amavue gha lutogo, ni lulu. Alyakolelile muluvoko lwa mweene ulwa sahabukino kimemile ifiinu fino fikalasia nhu vunyali vwa vuvwafu vwa mweene.
Mwanamke alivikwa nguo ya zambarau na nyekundu na amepambwa kwa dhahabu, mawe ya thamani, na lulu. Alikuwa ameshikilia mkononi mwake kikombe cha dhahabu kilichojaa vitu vya machukizo ya uchafu wa uasherati wake.
5 Pavweni vwa mwene lilembilue ilitavua lya vusyefu: “BABELI UM'BAHa, GHWE NG'INA GHWA VAMALAYA NI FINU FINO FIKARASI MU IISI.”
Juu ya paji la uso wake limeandikwa jina la siri: “BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA YA VITU VYA MACHUKIZO YA NCHI.”
6 Nikalula kuuti umwanamama uju akaghalile idanda ja vitiki ni danda javano valyafwile vwimila u Yesu. Unsiki ghuno nilyam'bwene, nikadeghile kyongo.
Nikaona ya kuwa mwanamke huyo alikuwa amelewa kwa damu ya waumini na damu ya waliokufa kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona, nilikuwa na mshangao mkuu.
7 Looli umunyamola akam'bula, “Kiki ghudegha? Nikukwolelela uvu mama kye kiinu kiki nu ng'aanu ikuntokla (ing'aanu ijio jinyamaatu lekela lubale namapembe ghala kijigho).
Lakini malaika akaniambia, “Kwa nini unashangaa? Nitakueleza maana ya mwanamke na mnyama amchukuaye (mnyama huyo mwenye vichwa saba na zile pembe kumi).
8 Ing'anu jino ukajivwene pwejikale, nakwejili kange lino, looli jiling'anisie kuhuma mu lina linlo lisila vusililo. Kange jighendelelaghe kuvomba uvunangi. Kuvala vano vikukala mu iisi, vala vano amatavua gha vanave naghalembilue mukitabu ikya vwuumi kuhuma livikua ulwalo lwa iisi - vilidegha pano vikujivona ing'anu jino pwiili, kuuti na pe jiili lino, looli alipipi pikwisa. (Abyssos g12)
Mnyama uliyemwona alikuwepo, hayupo tena sasa, lakini yuko tayari kupanda kutoka katika shimo lisilo na mwisho. Kisha ataendelea na uharibifu. Wale wakaao juu ya nchi, wale ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu - watashangaa wamwonapo mnyama aliyekuwepo, kwamba hayupo sasa, lakini yupo karibu kuja. (Abyssos g12)
9 Ing'emelo iiji vwimila vwa haala sino sivungike. Amaatu lekela lubale ni fidunda lekela lubale pano umwana mama alikalile lakyanya pa fyeene.
Wito huu ni kwa ajili ya akili zilizo na hekima. Vichwa saba ni milima saba ambapo mwanamke alikaa juu yake.
10 Joope kange ve vaatua lekela lubale. Ava tua vahano vaghwile, jumo kwale, jumo akyale na isile; unsiki ghuno ikwisa, ikukala unsiki n'debe.
Nayo pia ni wafalme saba. Wafalme watano wameanguka, mmoja yupo, na mwingine hajaja bado; wakati atakapokuja, atakaa kwa muda mfupi tu.
11 Ing'anu jino kwejilyale, looli lino napwiili, kange ghwe ntua ghwa lekela kwooni, looli ghwe jumo na vutua lekela lubale, kange iluta kuvunangi.
Mnyama aliyekuwepo, lakini sasa hayupo, yeye pia ni mfalme wa nane; lakini ni mmoja wa wale wafalme saba, na anaenda kwenye uharibifu.
12 Amapembe ghala kijigho ghano akaghavweene ve vatua kijigho vano navupiile uvutua, looli vikwupila uvutavulilua hwene vatua ku kivalilo kimo palikimo ni ng'anu.
Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao hawajapokea ufalme, lakini watapokea mamlaka kama wafalme kwa saa moja pamoja na mnyama.
13 Ava vali nu n'kolo ghumo pevikupela ingufu sa vanave nuvutavulilua vwa ng'aanu jiila.
Hawa wana shauri moja, na watampa nguvu zao na mamlaka yule mnyama.
14 Vilua ililugu avene nu mwana ng'olo. Looli umwanang'olo ikuvalefia ulwakuva Mutwa ghwa vatua Ntua ghwa vatua - mwamwene tukemelilue, tusalulivue, vapesie.”
Watafanya vita baina yao na Mwana kondoo. Lakini Mwana kondoo atawashinda kwa sababu ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme - na katika yeye tuliitwa, tulichaguliwa, waaminifu.”
15 Umunyamola akam'bula, “Amalenga ghala ghano akaghavwene, pala pano akikalileumalaya jula ve vaanhu, fupugha, fisina ni njovele.
Malaika akaniambia, “Yale maji uliyoyaona, hapo alipoketi yule kahaba ni watu, makutano, mataifa na lugha.
16 Amapembe ghala kijigho ghano aka ghavwene - ni ng'aanu jila vikusulagha u malaya juula. Voope vikum'bikagha mwene kange vufula, vilisagha um'biili ghwa mwene, pe vinyanyilila nu mwooto.
Zile pembe kumi ulizoziona - hizo na yule mnyama watamchukia yule kahaba. Nao watamfanya kuwa mpweke na uchi, watamla mwili wake, na watauteketeza kwa moto.
17 Ulwakuva u Nguluve avikile mu mojo gha vanave kum'pinda uluhuvilo lwa mwene ku lwiting'ano ulwakujipela ing'ano ingufu sivanave pikun'ema m'paka amasio gha Nguluve ghiiliva ghikwilana.
Maana Mungu ameweka mioyoni mwao kubeba kusudi lake kwa makubaliano ya kumpa mnyama nguvu zao kumtawala mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia.
18 Umwanamama jula juno alyam'bwene lye likaja lila ilivaha lino litemile uvutua vwa iisi.”
Yule mwanamke uliyemwona ni mji ule mkubwa utawalao juu ya wafalme wa nchi.”

< Ulusetulilo 17 >