< Ufunuo 9 >

1 Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu. (Abyssos g12)
And the fyfte angell blewe and I sawe a stare fall from heven vnto the erth. And to him was geven the kaye of the bottomlesse pytt. (Abyssos g12)
2 Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu. (Abyssos g12)
And he opened the botomlesse pytt and there arose the smoke of a grett fornace. And the sunne and the ayer were darkned by the reason of the smoke of the pytt. (Abyssos g12)
3 Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
And there cam out of the smoke locustes vpo the erth: and vnto them was geve power as the scorpions of the erth have power.
4 Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
And it hurt ye grasse of the erth: nether eny grene thinge: nether eny tree: but only those me which have not ye seale in their forhedes
5 Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
and to the was comaunded yt they shulde not kyll the but yt they shulde be vexed v monethes and their payne was as the payne yt cometh of a scorpion whe he hath stoge a ma.
6 Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
And in those dayes shall men seke deeth and shall not fynde it and shall desyre to dye and deeth shall flye fro the.
7 Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
And the similitude of the locustes was lyke vnto horses prepared vnto battayll and on their heddes were as it were crownes lyke vnto golde: and their faces were as it had bene the faces of men.
8 Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
And they had heare as the heare of wemen. And their tethe were as the tethe of lyons.
9 Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
And they had habbergions as it were habbergions of yron. And the sounde of their wynges was as the sounde of charettes when many horsses runne to gedder to battayle.
10 Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
And they had tayles lyke vnto scorpions and there were stinges in their tayles. And their power was to hurt men v. monethes.
11 Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi. (Abyssos g12)
And they had a kynge over them which is the angell of the bottomlesse pytt whose name in the hebrew tonge is Abadon: but in the greke tonge Apollion. (Abyssos g12)
12 Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
One woo is past and beholde two wooes come after this.
13 Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
And the sixte. angell blewe and I herd a voyce from the iiii. corners of the golden aultre which is before god
14 Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!”
saying to the sixte angell which had the trompe: Loose the iiii. angelles which are bounde in the grett ryver Eufrates.
15 Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
And the iiii. angelles were loosed which wer prepared for an houre for a daye for a moneth and for a yeare for to slee the thyrde part of me.
16 Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
And the nombre of horsme of warre were twenty tymes xM. And I herde the nobre of them.
17 Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
And thus I sawe the horses in a vision and them yt sate on the havynge fyry habbergions of a Iacyncte coloure and brymstony and the heeddes of ye horses werre as the heeddes of lyons. And out of their mouthes went forth fyre and smoke and brymstone.
18 Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
And of these iii. was the thyrde parte of men kylled: that is to saye of fyre smoke and brymstone which proceded out of the mouthes of them:
19 maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
For their power was in their mouthes and in their tayles: for their tayles were lyke vnto serpetes and had heedes and with them they dyd hurt:
20 Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
And the remnaunt of the me which were not kylled by these plages repented not of the dedes of their hondes that they shulde not worshyppe devyls and ymages of golde and sylver and brasse and stone and of wood which nether can se nether heare nether goo.
21 Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.
Also they repented not of their murther and of their sorcery nether of their fornacion nether of their thefte.

< Ufunuo 9 >