< Ufunuo 14 >

1 Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
And I loked and loo a lambe stode on the mount Syon and with him C. and xliiii. thousande havynge his fathers name written in their forhedes.
2 Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
And I herde a voyce from heven as the sounde of many waters and as the voyce of a gret thoundre And I herde the voyce of harpers harpynge with their harpes.
3 Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
And they songe as it were a newe songe before the seate and before the foure beestes and the elders and no man coulde learne that songe but the hondred and xliiii. M. which were redemed from the erth.
4 Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
These are they which were not defyled with wemen for they are virgyns. These folowe the lambe whither soever he goeth. These were redemed from men beynge the fyrste frutes vnto God and to the lambe
5 Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
and in their mouthes was foude no gyle. For they are with oute spott before the trone of god.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios g166)
And I sawe an angell flye in the myddes of heven havynge an everlastynge gospell to preache vnto them that sytt and dwell on the erth and to all nacions kinreddes and tonges and people (aiōnios g166)
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji.”
sayinge with a lowde voyce: Feare God and geve honour to him for the houre of his iudgement is come: and worshyppe him that made heven and erth and the see and fountaynes of water.
8 Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, “Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake—divai kali ya uzinzi wake!”
And there folowed another angell sayinge: Babilon is fallen is fallen that gret cite for she made all nacions drynke of the wyne of hyr fornicacion.
9 Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
And the thyrde angell folowed them sayinge with aloude voyce: Yf eny man worshippe the beest and his ymage and receave hie marke in his forhed or on his honde
10 yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
the same shall drynke of the wyne of the wrath of God which is powred in the cuppe of his wrath. And he shalbe punnysshed in fyre and brymstone before the holy Angels and before the lambe.
11 Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn g165)
And the smoke of their turment ascendeth vp evermore. And they have no rest daye ner nyght which worshippe ye beast and his ymage and whosoever receaveth the prynt of his name. (aiōn g165)
12 Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
Here is the pacience of saynctes. Heare are they that kepe the commaundmentes and the fayth of Iesu.
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana.” Naye Roho asema, “Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata.”
And I herde a voyce from heven sayinge vnto me: wryte. Blessed are the deed which here after dye in the lorde even soo sayth the sprete: that they maye rest fro their laboures but their workes shall folowe them.
14 Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
And I loked and beholde a whyte clowde and apon the clowde one syttynge lyke vnto the sonne of man havynge on his heed a golde crowne and in his honde a sharpe sykle.
15 Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, “Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva.”
And another angell came oute of the temple cryinge with a lowde voyce to him that sate on the clowde. Thruste in thy sycle and repe: for the tyme is come to repe for the corne of the erth is rype.
16 Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
And he that sate on the clowde thrust in his sykle on the erth and the erth was reped.
17 Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
And another angell came oute of the temple which is in heven havynge also a sharpe sycle.
18 Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, “Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!”
And another angell came oute from yt aultre which had power over fyre and cryed with a lowde crye to him that had the sharpe sykle and sayde: thrust in thy sharpe sykle and gaddre the clusters of the erth for her grapes are rype.
19 Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
And the angell thrust in his sykle on the erth and cut doune the grapes of the vyneyarde of the erth: and cast them into the gret wynefat of the wrath of god
20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.
and the wynefat was trodden with out the cite and bloud came oute of the fat eve vnto the hors brydles by the space of a thowsande and. vi. C. furlonges.

< Ufunuo 14 >