< Matendo 4 >

1 Petro na Yohane walipokuwa bado wanawahutubia watu, makuhani na mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na Masadukayo walifika.
While Peter and John were still speaking to the people, the chief priest, with the officer in charge at the Temple and the Sadducees, came up to them,
2 Walikasirika sana, maana hao mitume walikuwa wanawahubiria watu kwamba Yesu alifufuka, jambo ambalo linaonyesha wazi kwamba wafu watafufuka.
much annoyed because they were teaching the people, and because, through Jesus, they were preaching the resurrection from the dead.
3 Basi, waliwatia nguvuni na kwa kuwa usiku ulikuwa umekaribia, wakawaweka chini ya ulinzi mpaka kesho yake.
They arrested the apostles and, as it was already evening, had them placed in custody until the next day.
4 Lakini wengi kati ya wale waliosikia ujumbe wao waliamini, na idadi ya waumini ikawa imefika karibu elfu tano.
Many, however, of those who had heard the apostles’ message became believers in Christ, the number of the men alone amounting to about five thousand.
5 Kesho yake, viongozi wa Wayahudi, wazee na walimu wa Sheria, walikusanyika pamoja huko Yerusalemu.
The next day, a meeting of the leaders of the people, the elders, and the teachers of the Law was held in Jerusalem.
6 Walikutana pamoja na Anasi, Kayafa, Yohane, Aleksanda na wengine waliokuwa wa ukoo wa Kuhani Mkuu.
There were present Annas the high priest, Caiaphas, John, Alexander, and all who were of High-Priestly rank.
7 Waliwasimamisha mitume mbele yao, wakawauliza, “Ninyi mmefanya jambo hili kwa nguvu gani na kwa jina la nani?”
They had Peter and John brought before them, and questioned them. “By what power,” they asked, “Or in whose name have men like you done this thing?”
8 Hapo, Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akawaambia, “Viongozi na wazee wa watu!
Then, Peter, filled with the Holy Spirit, said, “Leaders of the people and elders,
9 Ikiwa mnatuuliza leo juu ya kile kitendo chema alichofanyiwa yule mtu aliyekuwa kiwete na jinsi alivyopata kuwa mzima,
since we are on our trial today for a kind act done to a helpless man, and are asked in what way the man here before you has been cured,
10 basi, ninyi na watu wote wa Israeli mnapaswa kujua kwamba mtu huyu anasimama mbele yenu leo, mzima kabisa, kwa nguvu ya jina lake Yesu wa Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, lakini Mungu akamfufua kutoka wafu.
let me tell you all and all the people of Israel, that it is by the name of Jesus Christ of Nazareth, whom you crucified and whom God raised from the dead – it is, I say, by his name that this man stands here before you lame no longer.
11 Huyu ndiye ambaye Maandiko Matakatifu yanasema: Jiwe mlilokataa ninyi waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
Jesus is ‘the stone which, scorned by you the builders, has yet become the corner stone.’
12 Wokovu haupatikani kwa mtu mwingine yeyote, kwa maana duniani pote, binadamu hawakupewa jina la mtu mwingine ambaye sisi tunaweza kuokolewa naye.”
And salvation is in him alone; for there is no other name in the whole world, given to people, to which we must look for our salvation.”
13 Hao wazee wa baraza, wakiwa wanajua kwamba Petro na Yohane walikuwa watu wasio na kisomo wala elimu yoyote, walishangaa juu ya jinsi walivyosema kwa uhodari. Wakatambua kwamba walikuwa wamejiunga na Yesu.
When the Council saw how boldly Peter and John spoke, and found that they were uneducated men of humble station, they were surprised, and realized that they had been companions of Jesus.
14 Lakini walipomwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuweza kusema kitu.
But, when they looked at the man who had been healed, standing there with them, they had nothing to say.
15 Hivyo, waliwaamuru watoke nje ya baraza, nao wakabaki ndani wakizungumza kwa faragha.
So they ordered them out of court, and then began consulting together.
16 Wakaulizana, “Tufanye nini na watu hawa? Kila mtu anayeishi Yerusalemu anajua kwamba mwujiza huu wa ajabu umefanyika, nasi hatuwezi kukana jambo hilo.
“What are we to do to these men?” they asked one another. “That a remarkable sign has been given through them is obvious to everyone living in Jerusalem, and we cannot deny it.
17 Lakini ili tupate kuzuia jambo hili lisienee zaidi kati ya watu, tuwaonye wasiongee na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
But, to prevent this thing from spreading further among the people, let us warn them not to speak in this name any more to anyone whatever.”
18 Kwa hiyo wakawaita tena ndani, wakawaonya wasiongee tena hadharani, wala kufundisha kwa jina la Yesu.
So they called the apostles in, and ordered them not to speak or teach in the name of Jesus.
19 Lakini Petro na Yohane wakawajibu, “Amueni ninyi wenyewe kama ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii yeye.
But Peter and John replied, “Whether it is right, in the sight of God, to listen to you rather than to him – judge for yourselves,
20 Kwa maana hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
for we cannot help speaking of what we have seen and heard.”
21 Basi, hao wazee wa Baraza wakawaonya kwa ukali zaidi, halafu wakawaacha huru. Hawakuweza kuwapa adhabu kwa sababu watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa sababu ya tukio hilo.
However, after further warnings, the Council set them at liberty, not seeing any safe way of punishing them, because of the people, for they were all praising God for what had occurred;
22 Huyo mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa miaka zaidi ya arobaini.
for the man who was the subject of this miraculous cure was more than forty years old.
23 Mara tu walipoachwa huru, Petro na Yohane walirudi kwa wenzao, wakawaeleza yale waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee.
After they had been set at liberty, the apostles went to their friends and told them what the chief priests and the elders had said to them.
24 Waliposikia habari hiyo waliungana pamoja katika kumwomba Mungu wakisema, “Bwana, wewe ni Muumba wa mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo!
All who heard their story, moved by a common impulse, raised their voices to God in prayer: “Sovereign Lord, it is you who has made the heavens, the earth, the sea, and everything that is in them,
25 Ndiwe uliyemfanya mtumishi wako, babu yetu Daudi, aseme kwa nguvu ya Roho Mtakatifu: Kwa nini mataifa yameghadhibika? Mbona watu wamefanya mipango ya bure?
and who, by the lips of our ancestor, your servant David, who spoke under the influence of the Holy Spirit, have said – ‘Why did the nations rage, and the peoples form vain designs?
26 Wafalme wa dunia walijiweka tayari, na watawala walikutana pamoja, ili kumwasi Bwana na Kristo wake.
The kings of the earth set their array, and its rulers gathered together, against the Lord and against his Christ.’
27 “Maana, kwa hakika, ndivyo Herode, Pontio Pilato, watu wa Israeli na watu wa mataifa walivyokutanika papa hapa mjini, kumpinga Yesu Mtumishi wako Mtakatifu ambaye umemtia mafuta.
There have indeed gathered together in this city against your holy servant Jesus, whom you has consecrated the Christ, not Herod and Pontius Pilate only, but the nations and the people of Israel besides –
28 Naam, walikutana ili wafanye yale ambayo ulikusudia na kupanga tangu mwanzo kwa uwezo wako na mapenzi yako.
yet only to do what you, by your power and of your own will, did long ago destine to be done.
29 Lakini sasa, ee Bwana, angalia vitisho vyao. Utuwezeshe sisi watumishi wako kuhubiri neno lako kwa uhodari.
Now, therefore, Lord, mark their threats, and enable your servants, with all fearlessness, to tell your message,
30 Nyosha mkono wako uponye watu. Fanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu Mtumishi wako Mtakatifu.”
while you stretch out your hand to heal, and cause signs and wonders to take place through the name of your holy servant Jesus.”
31 Walipomaliza kusali, pale mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, nao wote wakajazwa Roho Mtakatifu. Wote wakaanza kuhubiri neno la Mungu bila uoga.
When their prayer was ended, the place in which they were assembled was shaken; and they were all filled with the Holy Spirit, and began to tell God’s message fearlessly.
32 Jumuiya yote ya waumini ilikuwa moyo mmoja na roho moja. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na kitu chochote akakiweka kuwa mali yake binafsi, ila waligawana vyote walivyokuwa navyo.
The whole body of those who had become believers in Christ were of one heart and mind. Not one of them claimed any of his goods as his own, but everything was held for the common use.
33 Mitume walishuhudia kwa nguvu nyingi kufufuka kwa Bwana Yesu, naye Mungu akawapa baraka nyingi.
The apostles continued with great power to bear their testimony to the resurrection of the Lord Jesus, and God’s blessing rested on them all abundantly.
34 Hakuna mtu yeyote aliyetindikiwa kitu, maana waliokuwa na mashamba au nyumba walikuwa wanaviuza
Nor was there anyone in need among them, for all who were owners of land or houses sold them, and brought the proceeds of the sales
35 na kuwakabidhi mitume fedha hizo, zikagawiwa kila mmoja kadiri ya mahitaji yake.
and laid them at the apostles’ feet; and then everyone received a share in proportion to his wants.
36 Kulikuwa na Mlawi mmoja, mzaliwa wa Kupro, jina lake Yosefu, ambaye mitume walimwita jina Barnaba (maana yake, “Mtu mwenye kutia moyo”).
A Levite of Cyprian birth, named Joseph, (who had received from the apostles the additional name of ‘Barnabas’ – which means ‘The Consoler,’)
37 Yeye pia alikuwa na shamba lake, akaliuza; akazichukua zile fedha, akawakabidhi mitume.
Sold a farm that belonged to him, and brought the money and laid it at the apostles’ feet.

< Matendo 4 >