< Matendo 3 >

1 Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
One day, as Peter and John were going up into the Temple Courts for the three o’clock Prayers,
2 Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
a man, who had been lame from his birth, was being carried by. This man used to be set down every day at the gate of the Temple called ‘the Beautiful Gate,’ to beg of those who went in.
3 Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
Seeing Peter and John on the point of entering, he asked them to give him something.
4 Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
Peter fixed his eyes on him, and so did John, and then Peter said, “Look at us.”
5 Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
The man was all attention, expecting to get something from them;
6 Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
but Peter added, “I have no gold or silver, but I give you what I have. In the name of Jesus Christ of Nazareth, get up and walk.”
7 Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
Grasping the lame man by the right hand, Peter lifted him up. Instantly the man’s feet and ankles became strong,
8 Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
and, leaping up, he stood and began to walk about, and then went with them into the Temple Courts, walking, and leaping, and praising God.
9 Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
All the people saw him walking about and praising God;
10 Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
and, when they recognized him as the man who used to sit begging at the Beautiful Gate of the Temple, they were utterly astonished and amazed at what had happened to him.
11 Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
While the man still clung to Peter and John, the people all quickly gathered around them in the Colonnade named after Solomon, in the greatest astonishment.
12 Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
On seeing this, Peter said to the people, “People of Israel, why are you surprised at this? And why do you stare at us, as though we, by any power or piety of our own, had enabled this man to walk?
13 Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
The God of Abraham, Isaac, and Jacob, the God of our ancestors, has done honor to his servant Jesus – him whom you gave up and disowned before Pilate, when he had decided to set him free.
14 Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
You, I say, disowned the holy and righteous one, and asked for the release of a murderer!
15 Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
The guide to life you put to death! But God raised him from the dead – and of that we are ourselves witnesses.
16 Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
And it is by faith in the name of Jesus, that this man, whom you all see and know, has – by his name – been made strong. Yes, it is the faith inspired by Jesus that has made this complete cure of the man, before the eyes of you all.
17 “Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
And yet, my friends, I know that you acted as you did from ignorance, and your rulers also.
18 Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
But it was in this way that God fulfilled all that he had long ago foretold, as to the sufferings of his Christ, by the lips of all the prophets.
19 Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
Therefore, repent and turn so that your sins may be wiped away; so that happier times may come from the Lord himself,
20 Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
and so that he may send you, in Jesus, your long-appointed Christ.
21 Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
But heaven must be his home, until the days of the Universal Restoration, of which God has spoken by the lips of his holy prophets from the very first. (aiōn g165)
22 Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
Moses himself said – ‘The Lord your God will raise up from among yourselves a prophet, as he raised me. To him you will listen whenever he speaks to you.
23 Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
And it will be that should anyone among the people not listen to that prophet, he will be utterly destroyed.’
24 Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
Yes, and all the prophets from Samuel onwards, and all their successors who had a message to deliver, told of these days.
25 Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
You yourselves are the heirs of the prophets, and heirs, too, of the covenant which God made with your ancestors, when he said to Abraham – ‘In your descendants will all the nations of the earth be blessed.’
26 Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”
For you, first, God raised up his servant, and sent him to bless you, by turning each one of you from his wicked ways.”

< Matendo 3 >