< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
E, olhando ele, viu os ricos lançarem as suas ofertas na arca do tesouro;
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
E viu também uma pobre viúva lançar ali duas pequenas moedas;
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
E disse: Em verdade vos digo que lançou mais do que todos esta pobre viúva;
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
Porque todos aqueles deitaram para as ofertas de Deus, do que lhes sobeja; mas esta, da sua pobreza, deitou todo o sustento que tinha.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
E, dizendo alguns a respeito do templo, que estava ornado de formosas pedras e dádivas, disse:
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
Quanto a estas coisas que vêdes, dias virão em que se não deixará pedra sobre pedra, que não seja derribada.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
E perguntaram-lhe, dizendo: Mestre, quando serão pois estas coisas? E que sinal haverá quando estas coisas estiverem para acontecer?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
Disse então ele: vede não vos enganem, porque virão muitos em meu nome, dizendo: Eu sou o Cristo, e já o tempo está próximo; não vades portanto após eles.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
E, quando ouvirdes de guerras e sedições, não vos assusteis. Porque é necessário que estas coisas aconteçam primeiro, mas o fim não será logo.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Então lhes disse: levantar-se-a nação contra nação, e reino contra reino;
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
E haverá em vários lugares grandes terremotos, e fomes e pestilências; haverá também coisas espantosas, e grandes sinais do céu.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
Mas antes de todas estas coisas lançarão mão de vós, e vos perseguirão, entregando-vos às sinagogas e às prisões, e conduzindo-vos à presença de reis e presidentes, por amor do meu nome.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
E sobrevir-vos-a isto para testemunho.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Proponde pois em vossos corações não premeditar como haveis de responder,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
Porque eu vos darei boca e sabedoria a que não poderão contradizer nem resistir todos quantos se vos opuserem.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
E até pelos pais, e irmãos, e parentes, e amigos sereis entregues; e matarão alguns de vós.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
E por todos sereis aborrecidos por amor do meu nome.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Mas não perecerá nem um cabelo da vossa cabeça.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
Na vossa paciência possui as vossas almas.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
Porém, quando virdes Jerusalém cercada de exércitos, sabei então que já é chegada a sua assolação.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Então, os que estiverem na Judeia, fujam para os montes; e, os que estiverem no meio dela, saiam: e, os que nos campos, não entrem nela.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
Porque dias de vingança são estes, para que se cumpram todas as coisas que estão escritas.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Mas ai das grávidas, e das que criarem naqueles dias! porque haverá grande aperto na terra, e ira sobre este povo.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
E cairão ao fio da espada, e para todas as nações serão levados cativos; e Jerusalém será pisada pelos gentios, até que os tempos dos gentios se completem.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
E haverá sinais no sol, e na lua e nas estrelas; e na terra aperto das nações em perplexidade, pelo bramido do mar e das ondas;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Homens desmaiando de terror, na expectação das coisas que sobrevirão ao mundo. Porque as virtudes do céu serão abaladas.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
E então verão vir o Filho do homem numa nuvem, com poder e grande glória.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
Ora, quando estas coisas começarem a acontecer, olhai para cima, e levantai as vossas cabeças, porque a vossa redenção está próxima.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
E disse-lhes uma parábola: olhai para a figueira, e para todas as árvores;
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
Quando já tem brotado, vós sabeis por vós mesmos, vendo-as, que perto está já o verão.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
Assim também vós, quando virdes acontecer estas coisas, sabei que o reino de Deus está perto.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Em verdade vos digo que não passará esta geração até que tudo aconteça.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Passará o céu e a terra, mas as minhas palavras não hão de passar.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
E olhai por vós, não aconteça que os vossos corações se carreguem de glutonaria, embriaguez, e dos cuidados desta vida, e venha sobre vós de improviso aquele dia.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
Porque virá como um laço sobre todos os que habitam sobre a face de toda a terra.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Vigiai pois em todo o tempo, orando, para que sejais havidos por dignos de evitar todas estas coisas que hão de acontecer, e de estar em pé diante do Filho do homem.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
E de dia ensinava no templo, e à noite, saindo, ficava no monte chamado das Oliveiras.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
E todo o povo ia ter com ele ao templo, de manhã cedo, para o ouvir.

< Luka 21 >