< Yohana 1 >

1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
No princípio era o Verbo, e o Verbo estava com Deus, e o Verbo era Deus.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
Ele estava no princípio com Deus.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
Todas as coisas foram feitas por ele, e sem ele nada, do que foi feito, se fez.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
Nele estava a vida, e a vida era a luz dos homens;
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
E a luz resplandece nas trevas, e as trevas não a compreenderam.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
Houve um homem enviado de Deus, cujo nome era João.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
Este veio para testemunho, para que testificasse da luz; para que todos cressem por ele.
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
Não era ele a luz; mas para que testificasse da luz.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
Este era a luz verdadeira, que alumia a todo o homem que vem ao mundo.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
Estava no mundo, e o mundo foi feito por ele, e o mundo não o conheceu.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
Veio para o que era seu, e os seus não o receberam.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
Mas, a todos quantos o receberam, deu-lhes o poder de serem feitos filhos de Deus, a saber, aos que crêem no seu nome;
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
Os quais não nasceram do sangue, nem da vontade da carne, nem da vontade do varão, mas de Deus.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
E o Verbo se fez carne, e habitou entre nós, e vimos a sua glória, como a glória do unigênito do Pai, cheio de graça e de verdade.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
João testificou dele; e clamou, dizendo: Este era aquele de quem eu dizia: O que vem depois de mim é antes de mim, porque era primeiro do que eu.
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
E todos nós recebemos também da sua plenitude, e graça por graça.
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
Porque a lei foi dada por Moisés; a graça e a verdade vieram por Jesus Cristo.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
Deus nunca foi visto por alguém. O Filho unigênito, que está no seio do Pai, ele no-lo declarou.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
E este é o testemunho de João, quando os judeus mandaram de Jerusalém sacerdotes e levitas para que lhe perguntassem: Quem és tu
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
E confessou, e não negou; confessou: Eu não sou o Cristo.
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
E perguntaram-lhe: Pois que? És tu Elias? E disse: Não sou. És tu profeta? E respondeu: Não.
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
Disseram-lhe pois: Quem és? para que demos resposta àqueles que nos enviaram; que dizes de ti mesmo?
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
Disse: Eu sou a voz do que clama no deserto: endireitai o caminho do Senhor, como disse o profeta Isaias.
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
E os que tinham sido enviados eram dos fariseus;
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
E perguntaram-lhe, e disseram-lhe: Porque batizas pois, se tu não és o Cristo, nem Elias, nem o profeta?
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
João respondeu-lhes, dizendo: Eu batizo com água; mas no meio de vós está um a quem vós não conheceis.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
Este é aquele que vem após mim, que já foi antes de mim, do qual eu não sou digno de desatar a correia da alparca.
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
Estas coisas aconteceram em Bethania, da outra banda do Jordão, onde João estava batizando.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
No dia seguinte João viu a Jesus, que vinha para ele, e disse: Eis aqui o Cordeiro de Deus, que tira o pecado do mundo.
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
Este é aquele do qual eu disse: Após mim vem um varão que já foi antes de mim; porque já era primeiro do que eu.
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
E eu não o conhecia; mas, para que fosse manifestado a Israel, por isso vim eu batizando com água.
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
E João testificou, dizendo: Eu vi o espírito descer do céu como uma pomba, e repousar sobre ele.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
E eu não o conhecia, mas o que me mandou a batizar com água esse me disse: Sobre aquele que vires descer o espírito, e repousar sobre ele, esse é o que batiza com o Espírito Santo.
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
E eu vi, e tenho testificado que este é o Filho de Deus.
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
No dia seguinte João estava outra vez ali, e dois dos seus discípulos;
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
E, vendo por ali andar a Jesus, disse: Eis aqui o Cordeiro de Deus.
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
E os dois discípulos ouviram-no dizer isto, e seguiram a Jesus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
E Jesus, voltando-se e vendo que eles o seguiam, disse-lhes: Que buscais? E eles lhe disseram: rabi, (que, traduzido, quer dizer, Mestre) onde moras?
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
Ele lhes disse: Vinde, e vede. Foram, e viram onde morava, e ficaram com ele aquele dia: e era já quase a hora décima.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
Era André, irmão de Simão Pedro, um dos dois que ouviram aquilo de João, e o haviam seguido.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
Este achou primeiro a seu irmão Simão, e disse-lhe: Já achamos o Messias (que, traduzido, é o Christo).
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
E levou-o a Jesus. E, olhando Jesus para ele, disse: Tu és Simão, filho de Jonas; tu serás chamado Cephas (que quer dizer Pedro).
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
No dia seguinte quis Jesus ir à Galiléia, e achou a Felipe, e disse-lhe: Segue-me.
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
E Felipe era de Betsaida, cidade de André e de Pedro.
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Felipe achou Nathanael, e disse-lhe: Havemos achado aquele de quem Moisés escreveu na lei, e os profetas, a saber: Jesus de Nazareth, filho de José.
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
Disse-lhe Nathanael: Pode vir alguma coisa boa de Nazareth? Disse-lhe Felipe: Vem, e vê.
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
Jesus viu Nathanael vir ter com ele, e disse dele: Eis aqui um verdadeiro israelita, em quem não há dolo.
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
Disse-lhe Nathanael: de onde me conheces tu? Jesus respondeu, e disse-lhe: Antes que Felipe te chamasse, te vi eu, estando tu debaixo da figueira.
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanael respondeu, e disse-lhe: rabi, tu és o Filho de Deus, tu és o Rei de Israel.
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jesus respondeu, e disse-lhe: Porque te disse: Vi-te debaixo da figueira, crês? coisas maiores do que estas verás.
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
E disse-lhe: Na verdade, na verdade vos digo que daqui em diante vereis o céu aberto, e os anjos de Deus subirem e descerem sobre o Filho do homem.

< Yohana 1 >