< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And as he behelde, he sawe the rich men, which cast their giftes into the treasurie.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he sawe also a certaine poore widowe which cast in thither two mites:
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he sayd, Of a trueth I say vnto you, that this poore widowe hath cast in more then they all.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For they all haue of their superfluitie cast into the offerings of God: but she of her penurie hath cast in all the liuing that she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Nowe as some spake of the Temple, how it was garnished with goodly stones, and with consecrate things, he sayd,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
Are these ye things that ye looke vpon? the dayes will come wherein a stone shall not be left vpon a stone, that shall not be throwen downe.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
Then they asked him, saying, Master, but when shall these things be? and what signe shall there be when these things shall come to passe?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he sayd, Take heede, that ye be not deceiued: for many will come in my Name, saying, I am Christ, and the time draweth neere: follow ye not them therefore.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when ye heare of warres and seditions, be not afraid: for these things must first come, but the ende foloweth not by and by.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then said hee vnto them, Nation shall rise against nation, and kingdome against kingdome,
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
And great earthquakes shall be in diuers places, and hunger, and pestilence, and fearefull things, and great signes shall there be from heauen.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these, they shall lay their hands on you, and persecute you, deliuering you vp to the assemblies, and into prisons, and bring you before Kings and rulers for my Names sake.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
And this shall turne to you, for a testimoniall.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Lay it vp therefore in your heartes, that ye cast not before hand, what ye shall answere.
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will giue you a mouth and wisdome, where against all your aduersaries shall not be able to speake, nor resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
Yea, ye shalbe betrayed also of your parents, and of your brethren, and kinsmen, and friendes, and some of you shall they put to death.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And ye shall bee hated of all men for my Names sake.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Yet there shall not one heare of your heads perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
By your patience possesse your soules.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
And when ye see Hierusalem besieged with souldiers, then vnderstand that the desolation thereof is neere.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let them which are in Iudea, flee to the mountaines: and let them which are in the middes thereof, depart out: and let not them that are in the countrey, enter therein.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For these be the dayes of vengeance, to fulfill all things that are written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But woe be to them that be with childe, and to them that giue sucke in those dayes: for there shalbe great distresse in this land, and wrath ouer this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they shall fall on the edge of the sword, and shalbe led captiue into all nations, and Hierusalem shalbe troden vnder foote of the Gentiles, vntill the time of the Gentiles be fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
Then there shalbe signes in the sunne, and in the moone, and in the starres, and vpon the earth trouble among the nations with perplexitie: the sea and the waters shall roare.
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
And mens hearts shall faile them for feare, and for looking after those thinges which shall come on the worlde: for the powers of heauen shall be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then shall they see the Sonne of man come in a cloude, with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And when these things beginne to come to passe, then looke vp, and lift vp your heades: for your redemption draweth neere.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he spake to them a parable, Behold, the figge tree, and all trees,
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
When they nowe shoote foorth, ye seeing them, knowe of your owne selues, that sommer is then neere.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So likewise yee, when yee see these thinges come to passe, knowe ye that the kingdome of God is neere.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Verely I say vnto you, This age shall not passe, till all these things be done:
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heauen and earth shall passe away, but my wordes shall not passe away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
Take heede to your selues, lest at any time your hearts be oppressed with surfeting and drunkennesse, and cares of this life, and least that day come on you at vnwares.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For as a snare shall it come on all them that dwell on the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Watche therefore, and pray continually, that ye may be counted worthy to escape all these thinges that shall come to passe, and that ye may stand before the Sonne of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Nowe in the day time hee taught in the Temple, and at night hee went out, and abode in the mount that is called the mount of Oliues.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people came in the morning to him, to heare him in the Temple.

< Luka 21 >