< Yohana 3 >

1 Basi kulikuwa na Farisayo ambaye jina lake Nikodemo, mmoja wa wajumbe wa baraza la Wayahudi.
There was nowe a man of the Pharises, named Nicodemus, a ruler of the Iewes.
2 Mtu huyu alimwendea Bwana Yesu usiku na akamwambia, “Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu kutoka kwa Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kutenda ishara hizi zote Mungu asipokuwa pamoja naye.”
This man came to Iesus by night, and sayd vnto him, Rabbi, we knowe ye thou art a teacher come from God: for no man could do these miracles that thou doest, except God were with him.
3 Yesu akamjibu, “Amini, amini, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”
Iesus answered, and said vnto him, Verely, verely I say vnto thee, except a man be borne againe, he can not see the kingdome of God.
4 Nikodemo akasema,” Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, je anaweza?”
Nicodemus sayde vnto him, Howe can a man be borne which is olde? can he enter into his mothers wombe againe, and be borne?
5 Yesu akajibu, “Amini, amini mtu sipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
Iesus answered, Verely, verely I say vnto thee, except that a man be borne of water and of the Spirite, hee can not enter into the kingdome of God.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
That which is borne of the flesh, is flesh: and that that is borne of the Spirit, is spirit.
7 Usishangae kwa sababu nilikuwambia, 'ni lazima kuzaliwa mara ya pili.'
Marueile not that I said to thee, Yee must be borne againe.
8 Upepo huvuma popote upendapo na sauti yake mwaisikia, lakini hamjui utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo hali ya kila aliyezaliwa na roho.
The winde bloweth where it listeth, and thou hearest the sound thereof, but canst not tell whence it commeth, and whither it goeth: so is euery man that is borne of the Spirit.
9 Nikodemo akajibu, kwa kusema, “Mambo haya yawezekanaje?”
Nicodemus answered, and said vnto him, Howe can these things be?
10 Yesu akamjibu, “Wewe u mwalimu wa Israeli, hata hauyajui mambo haya?
Iesus answered, and saide vnto him, Art thou a teacher of Israel, and knowest not these things?
11 Amini, amini, nakuambia, kile tunachokifahamu twakishuhudia kwa kile tulichokiona. Lakini hampokei ushuhuda wetu.
Verely, verely I say vnto thee, wee speake that we know, and testifie that we haue seene: but yee receiue not our witnesse.
12 Kama nimewambia mambo ya hapa duniani na hamuamini, mtawezaje kuamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni?
If when I tel you earthly things, ye beleeue not, howe should yee beleeue, if I shall tel you of heauenly things?
13 Maana hakuna aliyepanda juu kutoka mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka, Mwana wa Adamu.
For no man ascendeth vp to heauen, but he that hath descended from heauen, that Sonne of man which is in heauen.
14 Kama vile Musa alivyomwinua nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu lazima ainuliwe,
And as Moses lift vp the serpent in the wildernesse, so must that Sonne of man be lift vp,
15 ili kwamba wote watakaomwamini wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
That whosoeuer beleeueth in him, shoulde not perish, but haue eternall life. (aiōnios g166)
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, kwamba akamtoa mwanae wa pekee, ili kwamba mtu yeyote amwaminiye asiangamie bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
For God so loued the worlde, that hee hath giuen his onely begotten Sonne, that whosoeuer beleeueth in him, should not perish, but haue euerlasting life. (aiōnios g166)
17 Kwa sababu Mungu hakumtuma mwanae duniani ili auhukumu ulimwengu, bali kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye.
For God sent not his Sonne into the world, that he should condemne the world, but that the world through him might be saued.
18 Amwaminiye Yeye hatahukumiwa. Yeye asiyemwamini tayari ameshahukumiwa kwa sababu hajaliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
Hee that beleeueth in him, is not condemned: but hee that beleeueth not, is condemned already, because he hath not beleeued in the Name of that onely begotten Sonne of God.
19 Hii ndiyo sababu ya hukumu, ya kwamba nuru imekuja ulimwenguni, lakini wanadamu wakapenda giza zaidi ya nuru kwa sababu matendo yao yalikuwa maovu.
And this is the condemnation, that that light came into the worlde, and men loued darknesse rather then that light, because their deedes were euill.
20 kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru wala haji nuruni ili matendo yake yasije yakawekwa wazi.
For euery man that euill doeth, hateth the light, neither commeth to light, least his deedes should be reprooued.
21 Lakini, yeye atendaye kweli huja kwenye nuru ili matendo yake yaonekane kwamba yametendwa kwa utiifu wa Mungu.
But he that doeth trueth, commeth to the light, that his deedes might bee made manifest, that they are wrought according to God.
22 Baada ya haya, Yesu pamoja na wanafunzi walienda katika nchi ya Yudea. Huko alitumia muda pamoja nao na alikuwa akibatiza.
After these things, came Iesus and his disciples into the lande of Iudea, and there taried with them, and baptized.
23 Sasa Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainea karibu na Salim maana kulikuwa na maji mengi pale. Watu walikuwa wakija kwake na kubatizwa,
And Iohn also baptized in Enon besides Salim, because there was much water there: and they came, and were baptized.
24 kwa kuwa Yohana alikuwa hajatupwa gerezani.
For Iohn was not yet cast into prison.
25 Kisha palitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi kuhusu sikukuuu za utakaso.
Then there arose a question betweene Iohns disciples and the Iewes, about purifying.
26 Wakaenda kwa Yohana wakamwambia, “Rabi, yeye uliyekuwa naye ng'ambo ya Mto Yorodani, yeye uliyeshuhudia habari zake, tazama, anabatiza na wote wanaenda wanamfuata.”
And they came vnto Iohn, and saide vnto him, Rabbi, he that was with thee beyond Iorden, to whom thou barest witnesse, behold, he baptizeth, and all men come to him.
27 Yohana akajibu mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa kama amepewa kutoka mbinguni.
Iohn answered, and saide, A man can receiue nothing, except it be giuen him from heauen.
28 Ninyi wenyewe mwashuhudia kuwa nalisema kuwa, 'mimi sio Kristo', badala yake nilisema, 'nimetumwa mbele yake.'
Yee your selues are my witnesses, that I sayde, I am not that Christ, but that I am sent before him.
29 Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika.
He that hath the bride, is the bridegrome: but the friend of the bridegrome which standeth and heareth him, reioyceth greatly, because of the bridegromes voyce. This my ioy therefore is fulfilled.
30 Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
He must increase, but I must decrease.
31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
Hee that is come from an hie, is aboue all: he that is of the earth, is of the earth, and speaketh of the earth: hee that is come from heauen, is aboue all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
And what hee hath seene and heard, that he testifieth: but no man receiueth his testimonie.
33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
He that hath receiued his testimonie, hath sealed that God is true.
34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
For hee whome God hath sent, speaketh the woordes of God: for God giueth him not the Spirit by measure.
35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.
The Father loueth the Sonne, and hath giuen all things into his hande.
36 Yeye amwaminiye Mwana anao uzima wa milele, lakini kwa yeye asiye mtii Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hushikamana juu yake. (aiōnios g166)
Hee that beleeueth in the Sonne, hath euerlasting life, and hee that obeyeth not the Sonne, shall not see life, but the wrath of God abideth on him. (aiōnios g166)

< Yohana 3 >