< Ezra 1 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Yahwe akatimiza neno lake ambalo Yeremia alisema, na kuinua roho ya Koreshi. Sauti ya Koreshi ikasambaa na kusikika katika ufalme wake. Hiki ndicho kilichoandikwa na kusemwa:
Now in the first year of Cyrus, king of Persia, in order that the word of the Lord given by the mouth of Jeremiah might come true, the spirit of Cyrus, king of Persia, was moved by the Lord, so that he made a public statement through all his kingdom, and put it in writing, saying,
2 “Koreshi, mfalme wa Uajemi, anasema: Yahwe, Mungu wa mbinguni, amenipa mimi ufalme wote wa dunia, na ameniteua mimi kumjengea yeye nyumba katika Yerusalem ya Yuda.
These are the words of Cyrus, king of Persia: The Lord God of heaven has given me all the kingdoms of the earth; and he has made me responsible for building a house for him in Jerusalem, which is in Judah.
3 Yeyote katika watu wake (Mungu awe pamoja naye) anaweza kwenda Yerusalem na kujenga nyumba kwa ajili ya Yahwe, Mungu wa Israel, Mungu ambaye yuko Yerusalem.
Whoever there is among you of his people, may his God be with him, and let him go up to Jerusalem, which is in Judah, and take in hand the building of the house of the Lord, the God of Israel; he is the God who is in Jerusalem.
4 Watu wa kila sehemu katika ufalme waliosalia katika nchi na kuishi wanapaswa kuwapa wao fedha na dhahabu, mali na wanyama, pamoja na kutoa kwa hiari kwenye nyumba ya Mungu Yerusalem.”
And whoever there may be of the rest of Israel, living in any place, let the men of that place give him help with offerings of silver and gold and goods and beasts, in addition to the offering freely given for the house of God in Jerusalem.
5 Ndipo wakuu wa jamii ya Yuda na Benjamini, makuhani na walawi, na kila mmoja ambaye Roho wa Mungu alimwinua kuondoka na kujenga nyumba yake alisimama.
Then the heads of families of Judah and Benjamin, with the priests and the Levites, got ready, even all those whose spirits were moved by God to go up and take in hand the building of the Lord's house in Jerusalem.
6 Wale waliowazunguka karibu waliwasaidia kwa kuwapa fedha na vitu vya dhahabu, mali, wanyama, vitu vya thamani, na kutoa kwa hiari.
And all their neighbours gave them help with offerings of vessels of silver and gold and goods and beasts and things of great value, in addition to what was freely offered.
7 Mfalme Koreshi akarusu vitu ambavyo vilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, ambavyo Nebukadreza alitoa kutoka Yerusalem na kuviweka katika nyumba ya miungu yake.
And Cyrus the king got out the vessels of the house of the Lord which Nebuchadnezzar had taken from Jerusalem and put in the house of his gods;
8 Koreshi akavikabidhi kwenye mikono ya Mithredathi mtunza fedha, ambaye akavitoa na kuhesabu kwa Sheshbaza, kiongozi wa Yuda
Even these Cyrus made Mithredath, the keeper of his wealth, get out, and he gave them, after numbering them, to Sheshbazzar, the ruler of Judah.
9 Hii ilikuwa idadi yake: beseni thelathini za dhahabu, beseni elfu moja za fedha, beseni zingine ishirini na tisa,
And this is the number of them: there were thirty gold plates, a thousand silver plates, twenty-nine knives,
10 mabakuli thelathini ya dhahabu, mabakuli madogo ya fedha 410, na vitu elfu moja vya kuongezea.
Thirty gold basins, four hundred and ten silver basins, and a thousand other vessels.
11 Kulikuwa na vitu 5, 400 vya fedha na dhahabu. Sheshbaza akavileta vyote wakati wa uhamisho kutoka Babeli kwenda Yerusalem.
There were five thousand, four hundred gold and silver vessels. All these were taken back by Sheshbazzar, when those who had been taken prisoner went up from Babylon to Jerusalem.

< Ezra 1 >