< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
[A Song of Ascents.] Many times they have afflicted me from my youth up. Let Israel now say,
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
many times they have afflicted me from my youth up, yet they have not prevailed against me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The plowers plowed on my back. They made their furrows long.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
Jehovah is righteous. He has cut apart the cords of the wicked.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Let them be disappointed and turned backward, all those who hate Zion.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Let them be as the grass on the housetops, which withers before it grows up;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
with which the reaper doesn't fill his hand, nor he who binds sheaves, his bosom.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Neither do those who go by say, "The blessing of Jehovah be on you. We bless you in the name of Jehovah."

< Zaburi 129 >