< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
[A Song of Ascents.] Jehovah, remember David and all his affliction,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
how he swore to Jehovah, and vowed to the Mighty One of Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
"Surely I will not come into the structure of my house, nor go up into my bed;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
I will not give sleep to my eyes, or slumber to my eyelids;
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
until I find out a place for Jehovah, a dwelling for the Mighty One of Jacob."
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Look, we heard of it in Ephrathah. We found it in the field of Jaar:
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
"We will go into his dwelling place. We will worship at his footstool.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Arise, Jehovah, to your resting place, you and the ark of your strength.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Let your priest be clothed with righteousness. Let your faithful ones shout for joy."
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For your servant David's sake, do not turn away the face of your anointed one.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Jehovah has sworn to David in truth. He will not turn from it: "I will set the fruit of your body on your throne.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
If your children will keep my covenant, my testimony that I will teach them, their children also will sit on your throne forevermore."
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For Jehovah has chosen Zion; he has desired it for his dwelling.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
"This is my resting place forever. Here I will live, for I have desired it.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
I will abundantly bless her provision. I will satisfy her poor with bread.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Her priests I will also clothe with salvation. Her faithful ones will shout aloud for joy.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
There I will make the horn of David to bud. I have ordained a lamp for my anointed.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
I will clothe his enemies with shame, but on himself, his crown will be resplendent."

< Zaburi 132 >