< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Mon fils, ne mets point en oubli mon enseignement, et que ton cœur garde mes commandements.
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Car ils t'apporteront de longs jours, et des années de vie, et de prospérité.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Que la gratuité et la vérité ne t'abandonnent point: lie-les à ton cou, et écris-les sur la table de ton cœur;
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Et tu trouveras la grâce et le bon sens aux yeux de Dieu et des hommes.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Confie-toi de tout ton cœur en l'Eternel, et ne t'appuie point sur ta prudence.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
Considère-le en toutes tes voies, et il dirigera tes sentiers.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Ne sois point sage à tes yeux; crains l'Eternel, et détourne-toi du mal.
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
Ce sera une médecine à ton nombril, et une humectation à tes os.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Honore l'Eternel de ton bien, et des prémices de tout ton revenu.
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
Et tes greniers seront remplis d'abondance, et tes cuves rompront de moût.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
Mon fils, ne rebute point l'instruction de l'Eternel, et ne te fâche point de ce qu'il te reprend.
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Car l'Eternel reprend celui qu'il aime, même comme un père l'enfant auquel il prend plaisir.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Ô! que bienheureux est l'homme [qui] trouve la sagesse, et l'homme qui met en avant l'intelligence!
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
Car le trafic qu'on peut faire d'elle, est meilleur que le trafic de l'argent; et le revenu qu'on en peut avoir, est meilleur que le fin or.
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
Elle est plus précieuse que les perles, et toutes tes choses désirables ne la valent point.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Il y a de longs jours en sa main droite, des richesses et de la gloire en sa gauche.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Ses voies sont des voies agréables, et tous ses sentiers ne sont que prospérité.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
Elle est l'arbre de vie à ceux qui l'embrassent; et tous ceux qui la tiennent sont rendus bienheureux.
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
L'Eternel a fondé la terre par la sapience, et il a disposé les cieux par l'intelligence.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
Les abîmes se débordent par sa science, et les nuées distillent la rosée.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
Mon fils, qu'elles ne s'écartent point de devant tes yeux; garde la droite connaissance et la prudence.
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
Et elles seront la vie de ton âme, et l'ornement de ton cou.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Alors tu marcheras en assurance par ta voie, et ton pied ne bronchera point.
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
Si tu te couches, tu n'auras point de frayeur, et quand tu te seras couché ton sommeil sera doux.
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
Ne crains point la frayeur subite, ni la ruine des méchants, quand elle arrivera.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
Car l'Eternel sera ton espérance, et il gardera ton pied d'être pris.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
Ne retiens pas le bien de ceux à qui il appartient, encore qu'il fût en ta puissance de le faire.
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
Ne dis point à ton prochain: Va, et retourne, et je te le donnerai demain, quand tu l'as par-devers toi.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Ne machine point de mal contre ton prochain; vu qu'il habite en assurance avec toi.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
N'aie point de procès sans sujet avec aucun, à moins qu'il ne t'ait fait quelque tort.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Ne porte point d'envie à l'homme violent, et ne choisis aucune de ses voies.
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Car celui qui va de travers est en abomination à l'Eternel; mais son secret est avec ceux qui sont justes.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
La malédiction de l'Eternel est dans la maison du méchant; mais il bénit la demeure des justes.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Certes il se moque des moqueurs, mais il fait grâce aux débonnaires.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Les sages hériteront la gloire; mais l'ignominie élève les fous.

< Mithali 3 >