< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Moreover Jehovah answered Job,
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
"Shall he who argues contend with Shaddai? He who argues with God, let him answer it."
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Then Job answered Jehovah,
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
"Look, I am of small account. What shall I answer you? I lay my hand on my mouth.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
I have spoken once, and I will not answer; Yes, twice, but I will proceed no further."
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Then Jehovah answered Job out of the whirlwind,
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
"Now brace yourself like a man. I will question you, and you will answer me.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Will you even annul my judgment? Will you condemn me, that you may be justified?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Or do you have an arm like God? Can you thunder with a voice like him?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
"Now deck yourself with excellency and dignity. Array yourself with honor and majesty.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Pour out the fury of your anger. Look at everyone who is proud, and bring him low.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Look at everyone who is proud, and humble him. Crush the wicked in their place.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Hide them in the dust together. Bind their faces in the hidden place.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Then I will also admit to you that your own right hand can save you.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
"Look now at the sauropod, which I made as well as you. He eats grass as an ox.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Look now, his strength is in his thighs. His force is in the muscles of his belly.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
He moves his tail like a cedar. The sinews of his thighs are knit together.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
His bones are like tubes of bronze. His limbs are like bars of iron.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
He is the chief of the ways of God. He who made him gives him his sword.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
Surely the mountains produce food for him, where all the animals of the field play.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
He lies under the lotus trees, in the covert of the reed, and the marsh.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
The lotuses cover him with their shade. The willows of the brook surround him.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Look, if a river overflows, he doesn't tremble. He is confident, though the Jordan swells even to his mouth.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Shall any take him when he is on the watch, or pierce through his nose with a snare?

< Ayubu 40 >