< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Blessed is the one who doesn't follow the advice of the wicked, or take the path of sinners, or join in with scoffers.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
But his delight is in the law of Jehovah, and on his law he meditates day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
He will be like a tree planted by the streams of water, that brings forth its fruit in its season, whose leaf also does not wither, and whatever he does shall prosper.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Not so with the wicked; instead, they are like the chaff which the wind drives away.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For Jehovah knows the way of the righteous, but the way of the wicked shall perish.

< Zaburi 1 >