< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Alors l'Éternel répondit à Job du sein de la tempête, et dit:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Qui est celui-ci qui obscurcit mes plans par des discours sans science?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Ceins donc tes reins comme un vaillant homme, je t'interrogerai, et tu m'instruiras.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Où étais-tu quand je jetais les fondations de la terre? Dis-le, si tu as de l'intelligence.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Qui en a réglé les mesures, si tu le sais, ou qui a étendu le niveau sur elle?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Sur quoi en a-t-on fait plonger les bases, ou qui en a posé la pierre angulaire,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Quand les étoiles du matin poussaient ensemble des cris de joie, et les fils de Dieu, des acclamations?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Et qui renferma la mer dans des portes, quand elle sortit en s'élançant du sein de la terre;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
Quand je lui donnai la nuée pour vêtement, et l'obscurité pour langes;
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Quand j'établis ma loi sur elle, quand je lui mis des verrous et des portes,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Et que je lui dis: Tu viendras jusqu'ici, et tu n'iras pas plus loin; ici s'arrêtera l'orgueil de tes flots?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Depuis que tu es au monde, as-tu commandé au matin, as-tu marqué à l'aurore sa place,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
Pour qu'elle saisisse les extrémités de la terre, et que les méchants soient chassés?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
La terre change de forme comme l'argile sous le cachet, et toutes choses se lèvent comme pour la vêtir.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
La lumière des méchants leur est ôtée, et le bras des menaçants est rompu.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
As-tu pénétré jusqu'aux sources de la mer, et t'es-tu promené au fond de l'abîme?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort se sont-elles découvertes à toi? Et as-tu vu les portes de l'ombre de la mort?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
As-tu compris l'étendue de la terre? Si tu sais tout cela, dis-le!
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Où est le chemin du séjour de la lumière? Et les ténèbres, où est leur demeure?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Car tu peux les ramener à leur domaine, et tu connais les sentiers de leur maison!
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Tu le sais; car alors tu étais né, et le nombre de tes jours est grand!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
As-tu pénétré jusqu'aux trésors de neige? Et as-tu vu les trésors de grêle,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Que je réserve pour les temps de détresse, pour le jour de la bataille et du combat?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Par quels chemins se partage la lumière, et le vent d'orient se répand-il sur la terre?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Qui a donné à l'averse ses canaux, et sa voie à l'éclair des tonnerres,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
Pour faire pleuvoir sur une terre sans habitants, sur un désert sans hommes,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
Pour abreuver des lieux déserts et désolés, et faire germer et sortir l'herbe?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
La pluie a-t-elle un père? Ou, qui enfante les gouttes de rosée?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
De quel sein est sortie la glace? Et qui enfante le givre du ciel?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Les eaux se dissimulent, changées en pierre, et la surface de l'abîme se prend.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Peux-tu resserrer les liens des Pléiades, ou détacher les chaînes d'Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Fais-tu sortir en leur temps les signes du zodiaque? Et conduis-tu la grande Ourse avec ses petits?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Connais-tu les lois du ciel? Ou disposes-tu de son pouvoir sur la terre?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Élèves-tu ta voix vers la nuée, pour que des eaux abondantes te couvrent?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Envoies-tu les éclairs? Partent-ils, et te disent-ils: Nous voici?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Qui a mis la sagesse dans les nues, qui a donné au météore l'intelligence?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Qui compte les nuages avec sagesse, qui incline les outres des cieux,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
Quand la poussière se délaie et se met en fusion, et que les mottes s'agglomèrent?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Chasses-tu pour le lion sa proie, et assouvis-tu la faim des lionceaux,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
Quand ils se tapissent dans leurs repaires, quand ils sont aux aguets dans les fourrés?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Qui apprête la nourriture au corbeau, quand ses petits crient vers Dieu et volent çà et là, n'ayant rien à manger?

< Ayubu 38 >