< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Heureux l'homme qui ne marche pas selon le conseil des méchants, et qui ne se tient pas dans la voie des pécheurs, et qui ne s'assied pas au banc des moqueurs;
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
Mais qui prend son plaisir dans la loi de l'Éternel, et médite sa loi jour et nuit.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Il sera comme un arbre planté près des eaux courantes, qui rend son fruit dans sa saison et dont le feuillage ne se flétrit point; et dans tout ce qu'il fait, il réussira.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Il n'en sera pas ainsi des méchants; mais ils seront comme la paille que le vent chasse au loin.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
C'est pourquoi les méchants ne subsisteront pas dans le jugement, ni les pécheurs dans l'assemblée des justes.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
Car l'Éternel connaît la voie des justes, mais la voie des méchants périra.

< Zaburi 1 >