< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
Élihu reprit la parole, et dit:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
Vous, sages, écoutez mes discours; et vous, savants, prêtez-moi l'oreille.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
Car l'oreille juge des discours, comme le palais goûte ce qu'on doit manger.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Choisissons ensemble ce qui est juste; voyons, entre nous, ce qui est bon.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Job a dit: “Je suis juste, mais Dieu met mon droit de côté;
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
En dépit de mon droit, je suis un menteur; ma plaie est douloureuse, sans que j'aie péché. “
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
Y a-t-il un homme tel que Job, qui boit le blasphème comme l'eau,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
Qui marche dans la compagnie des ouvriers d'iniquité, et qui va avec les hommes pervers?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
Car il a dit: L'homme ne gagne rien à se plaire avec Dieu.
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
C'est pourquoi, vous qui avez de l'intelligence, écoutez-moi. Loin de Dieu la méchanceté! loin du Tout-Puissant l'injustice!
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
Il rend à l'homme selon ses œuvres, et il fait trouver à chacun selon sa conduite.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Certainement Dieu ne commet pas d'injustice, le Tout-Puissant ne fait pas fléchir le droit.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
Qui lui a commis le soin de la terre? Qui lui a confié l'univers?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
S'il ne pensait qu'à lui, s'il retirait à lui son esprit et son souffle,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
Toute chair expirerait à la fois, et l'homme retournerait dans la poussière.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Si donc tu as de l'intelligence, écoute cela; prête l'oreille au son de mes paroles.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Eh quoi! celui qui haïrait la justice, régnerait-il? Et condamnerais-tu celui qui est souverainement juste?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
Lui qui dit aux rois “Scélérat! “et “Méchant! “aux princes;
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
Qui n'a point égard à la personne des grands, qui ne connaît pas le riche plus que le pauvre, car ils sont tous l'ouvrage de ses mains?
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
En un moment ils mourront; au milieu de la nuit, un peuple est ébranlé et passe; le potentat puissant est emporté, et non par une main d'homme.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
Car les yeux de Dieu sont sur les voies de l'homme, et il regarde tous ses pas.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
Il n'y a ni ténèbres ni ombre de la mort, où se puissent cacher les ouvriers d'iniquité.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
Il ne regarde pas à deux fois un homme, pour le faire aller en jugement avec lui.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
Il brise les puissants, sans enquête, et il en établit d'autres à leur place,
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Parce qu'il connaît leurs œuvres; il les renverse de nuit, et ils sont brisés.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Il les flagelle comme des impies, à la vue de tout le monde,
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Parce qu'ils se sont détournés de lui, et n'ont pas du tout pris garde à ses voies.
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
Ils ont fait monter jusqu'à lui le cri du pauvre, et il a entendu la clameur des affligés.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
S'il donne le repos, qui est-ce qui le condamnera? S'il cache sa face, qui le regardera? soit qu'il s'agisse d'un peuple ou d'un particulier,
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
Pour que l'homme impie ne règne pas, pour qu'il ne soit pas en piège au peuple.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
Car a-t-il dit à Dieu: “J'ai souffert, je ne pécherai plus;
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
Ce que je ne vois pas, montre-le-moi; si j'ai fait le mal, je ne le ferai plus? “
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Est-ce donc d'après tes idées que le mal doit être puni? Car tu as montré du mécontentement. Ainsi, c'est à toi de décider, non à moi! Dis ce que tu sais.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Les hommes de sens me diront, ainsi que le sage qui m'aura écouté:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
“Job ne parle pas avec con-naissance, et ses paroles sont sans intelligence. “
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Ah! que Job soit éprouvé jusqu'à la fin, puisqu'il a répondu comme les méchants!
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
Car il ajoute à son péché une transgression nouvelle; il s'applaudit au milieu de nous; il parle de plus en plus contre Dieu.

< Ayubu 34 >