< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Alors ces trois hommes-là cessèrent de répondre à Job, parce qu'il croyait être juste.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Et Élihu, fils de Barakéel, Buzite, de la famille de Ram, se mit dans une fort grande colère contre Job, parce qu'il se justifiait lui-même devant Dieu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Il se mit aussi en colère contre ses trois amis, parce qu'ils ne trouvaient rien à répondre, et que néanmoins ils avaient condamné Job.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Et Élihu avait attendu pour s'adresser à Job qu'ils eussent parlé, parce qu'ils étaient plus âgés que lui.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Élihu, voyant que ces trois hommes n'avaient plus aucune réponse à la bouche, se mit en colère.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Et Élihu, fils de Barakéel, Buzite, prit la parole, et dit: Je suis jeune et vous êtes des vieillards, aussi j'ai craint et je n'ai pas osé vous dire mon avis.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Je me disais: Les jours parleront, et le grand nombre des années fera connaître la sagesse.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Mais c'est l'esprit qui est dans les hommes, c'est le souffle du Tout-Puissant qui les rend intelligents.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Ce ne sont pas les aînés qui sont sages; ce ne sont pas les vieillards qui comprennent ce qui est juste.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
C'est pourquoi je dis: Écoute-moi; je dirai mon avis, moi aussi.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Voici, j'ai attendu vos discours, j'ai écouté vos raisonnements, jusqu'à ce que vous eussiez bien examiné les discours de Job.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Je vous ai suivis attentivement, et voici, pas un de vous n'a convaincu Job, pas un n'a répondu à ses paroles.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Ne dites pas: Nous avons trouvé la sagesse! Dieu seul le mettra en fuite, et non un homme.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Il n'a pas dirigé ses discours contre moi, et je ne lui répondrai pas à votre manière.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Ils sont consternés! Ils ne répondent plus! On leur a ôté l'usage de la parole!
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
J'ai attendu: puisqu'ils ne parlent plus, qu'ils se tiennent là sans répondre,
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Je répondrai, moi aussi, pour ma part; je dirai mon avis, moi aussi;
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Car je suis rempli de discours; l'esprit qui est en mon sein me presse.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Voici, mon sein est comme un vin sans issue, il va éclater comme des outres neuves.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Je parlerai donc et je me soulagerai, j'ouvrirai mes lèvres et je répondrai.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Qu'il ne m'arrive pas d'être partial, et de flatter qui que ce soit.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Car je ne sais pas flatter: mon créateur ne m'enlèverait-il pas bientôt!

< Ayubu 32 >