< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Mais, maintenant, des hommes plus jeunes que moi se moquent de moi, des hommes dont je n'aurais pas daigné mettre les pères avec les chiens de mon troupeau.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Et qu'aurais-je pu faire de la force de leurs mains? En eux avait péri toute vigueur.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Exténués par la disette et la faim, ils broutent les lieux arides, depuis longtemps désolés et déserts.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Ils cueillent l'herbe sauvage près des buissons, et la racine des genêts est leur nourriture.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
On les chasse du milieu des hommes; on crie après eux comme après un larron;
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Ils habitent dans des torrents affreux, dans les trous de la terre, et parmi les rochers.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
On les entend braire dans les buissons, ils s'étendent pêle-mêle sous les chardons;
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Race impie, race sans nom, qui avait été chassée du pays!
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Et maintenant je suis le sujet de leurs chansons, et je fais la matière de leurs propos.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Ils m'ont en horreur, ils s'éloignent de moi; ils ne craignent pas de me cracher au visage.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Parce que Dieu a détendu la corde de mon arc et m'a humilié, ils ont secoué tout frein devant moi.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Cette engeance se lève à ma droite; ils poussent mes pieds; ils construisent contre moi des routes pour me nuire;
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Ils rompent mon chemin, ils aident à ma ruine, eux à qui personne ne porterait secours.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Ils arrivent comme par une large brèche, ils se précipitent au milieu du fracas.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Toutes les terreurs se tournent contre moi, elles poursuivent ma prospérité comme le vent, et mon bonheur a passé comme un nuage!
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
Et maintenant mon âme se fond en moi, les jours d'affliction m'ont atteint;
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
La nuit perce mes os et les détache, et ceux qui me rongent ne dorment pas.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Par la violence extrême de mon mal, mon vêtement se déforme; il me serre comme le col de ma tunique.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Dieu m'a jeté dans la boue, et je ressemble à la poussière et à la cendre.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Je crie vers toi, et tu ne me réponds pas; je me tiens debout devant toi, et tu me considères!
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Tu es devenu cruel pour moi; tu t'opposes à moi avec toute la force de ton bras.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Tu m'enlèves, tu me fais chevaucher sur le vent, et tu me fais fondre au bruit de la tempête.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Oui, je sais bien que tu m'amènes à la mort, et dans la demeure, rendez-vous de tous les vivants.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Seulement, n'étendrait-on pas la main au milieu de la ruine? Et, dans sa calamité, ne serait-il donc pas permis de pousser un cri?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Ne pleurais-je pas sur l'homme qui passait de mauvais jours? Mon âme n'était-elle pas affligée à cause du pauvre
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
J'ai attendu le bonheur, et le malheur est arrivé. J'espérais la lumière, et les ténèbres sont venues.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mes entrailles bouillonnent sans repos; les jours d'affliction m'ont assailli.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Je marche tout noirci, et non par le soleil. Je me lève dans l'assemblée, et je crie.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Je suis devenu le frère des chacals, et le compagnon des autruches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ma peau se noircit et tombe. Mes os sont brûlés par la fièvre.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Ma harpe s'est changée en deuil, et mon luth en voix de pleurs.

< Ayubu 30 >