< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Après cela, Job ouvrit la bouche et maudit le jour de sa naissance.
2 Kisha akasema:
Et, prenant la parole, Job dit:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Périsse le jour où je suis né, et la nuit qui a dit: Un homme est conçu!
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Que ce jour soit ténèbres, que Dieu ne s'en enquière pas d'en haut, qu'aucune lumière ne brille sur lui!
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Que les ténèbres et l'ombre de la mort le reprennent, qu'une sombre nuée demeure sur lui, qu'une éclipse le remplisse d'horreur!
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Que l'obscurité s'empare de cette nuit, qu'elle ne se réjouisse pas au milieu des jours de l'année, qu'elle n'entre pas dans le compte des mois!
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Voici, que cette nuit soit stérile, et qu'aucun cri de joie n'y survienne!
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Qu'ils la maudissent ceux qui maudissent les jours, ceux qui sont habiles à faire lever Léviathan!
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Que les étoiles de son crépuscule soient obscurcies, qu'elle attende la lumière et qu'il n'y en ait point, et qu'elle ne voie pas les paupières de l'aurore!
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Parce qu'elle n'a pas fermé le sein qui me porta, et n'a point caché la douleur à mes yeux!
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Que ne suis-je mort dès le sein de ma mère? Au sortir de ses flancs, que n'ai-je expiré?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Pourquoi des genoux se sont-ils présentés à moi, et pourquoi des mamelles pour être sucées?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Car, maintenant, je serais couché et tranquille, je dormirais, je serais en repos,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
Avec les rois et les arbitres de la terre, qui se bâtissent des mausolées,
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
Avec les princes qui ont de l'or, qui remplissent d'argent leurs maisons.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Ou bien, comme l'avorton caché, je n'existerais pas; comme les petits enfants qui n'ont pas vu la lumière.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Là, les méchants ne tourmentent plus personne, et là se reposent les hommes fatigués;
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Avec eux, les captifs sont tranquilles: ils n'entendent plus la voix de l'exacteur.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Là, le petit et le grand sont ensemble, et l'esclave est délivré de son maître.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Pourquoi donne-t-on la lumière au malheureux, et la vie à ceux dont l'âme est pleine d'amertume?
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Qui attendent la mort, et elle ne vient point, qui la recherchent plus qu'un trésor,
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Qui seraient contents jusqu'à l'allégresse et ravis de joie, s'ils trouvaient le tombeau?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
A l'homme qui ne connaît pas sa voie et que Dieu cerne de tous côtés?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Car je soupire au lieu de manger, et mes cris se répandent comme l'eau.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Ce que je crains m'arrive, et ce que j'appréhende vient sur moi.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Je n'ai ni paix, ni tranquillité, ni repos! Le tourment est venu!

< Ayubu 3 >