< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
After this Job opened his mouth, and cursed his day.
2 Kisha akasema:
Job answered:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
"Let the day perish in which I was born, the night which said, 'A man is conceived.'
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Let that day be darkness. May God above not care about it, neither let the light shine on it.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Let darkness and the shadow of death claim it for their own. Let a cloud dwell on it. Let the blackness of the day terrify it.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
As for that night, let thick darkness seize on it. Let it not rejoice among the days of the year. Let it not come into the number of the months.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Look, let that night be barren. Let no joyful voice come in it.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Let them curse it who curse the day, who are ready to rouse up leviathan.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Let the stars of its twilight be dark. Let it look for light, but have none, neither let it see the eyelids of the morning,
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
because it did not shut up the doors of my mother's womb, nor did it hide trouble from my eyes.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
"Why did I not die from the womb? Why did I not give up the spirit when my mother bore me?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Why did the knees receive me? Or why the breast, that I should suck?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
For now should I have lain down and been quiet. I should have slept, then I would have been at rest,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
with kings and counselors of the earth, who built up waste places for themselves;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
or with princes who had gold, who filled their houses with silver:
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
or as a hidden untimely birth I had not been, as infants who never saw light.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
There the wicked cease from troubling. There the weary are at rest.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
There the prisoners are at ease together. They do not hear the voice of the taskmaster.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
The small and the great are there. The servant is free from his master.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
"Why is light given to him who is in misery, life to the bitter in soul,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Who long for death, but it doesn't come; and dig for it more than for hidden treasures,
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
who rejoice exceedingly, and are glad, when they can find the grave?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Why is light given to a man whose way is hid, whom God has hedged in?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
For my sighing comes before I eat. My groanings are poured out like water.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
For the thing which I fear comes on me, That which I am afraid of comes to me.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
I am not at ease, neither am I quiet, neither have I rest; but trouble comes."

< Ayubu 3 >