< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
But Job answered and said,
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
To whom do you attach yourself, or whom are you going to assist? is it not he that [has] much strength, and [he] who has a strong arm?
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
To whom have you given counsel? is it not to him who has all wisdom? whom will you follow? is it not one who has the greatest power?
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
To whom have you uttered words? and whose breath is it that has come forth from you?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Shall giants be born from under the water and the inhabitants thereof?
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Hell is naked before him, and destruction has no covering. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
He stretches out the north wind upon nothing, and he upon nothing hangs the earth;
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
binding water in his clouds, and the cloud is not tore under it.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
He keeps back the face of his throne, stretching out his cloud upon it.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
He has encompassed the face of the water by an appointed ordinance, until the end of light and darkness.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
The pillars of heaven are prostrate and astonished at his rebuke.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
He has calmed the sea with [his] might, and by [his] wisdom the whale has been overthrown.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
And the barriers of heaven fear him, and by a command he has slain the apostate dragon.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Behold, these are parts of his way; and we will listen to him at the least intimation of his word: but the strength of his thunder who knows, when he shall employ [it]?

< Ayubu 26 >