< Ayubu 24 >

1 “Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
But why have the seasons been hidden from the Lord,
2 Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
while the ungodly have passed over the bound, carrying off the flock with the shepherd?
3 Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
They have led away, the ass of the fatherless, and taken the widow's ox for a pledge.
4 Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
They have turned aside the weak from the right way: and the meek of the earth have hidden themselves together.
5 Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
And they have departed like asses in the field, having gone forth on my account according to their own order: his bread is sweet to [his] little ones.
6 Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
They have reaped a field that was not their own before the time: the poor have laboured in the vineyards of the ungodly without pay and without food.
7 Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
They have caused many naked to sleep without clothes, and they have taken away the covering of their body.
8 Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
They are wet with the drops of the mountains: they have embraced the rock, because they had no shelter.
9 Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
They have snatched the fatherless from the breast, and have afflicted the outcast.
10 Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
And they have wrongfully caused [others] to sleep without clothing, and taken away the morsel of the hungry.
11 Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
They have unrighteously laid wait in narrow places, and have not known the righteous way.
12 Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
Who have cast forth [the] poor from the city and their own houses, and the soul of the children has groaned aloud.
13 “Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
Why then has he not visited these? forasmuch as they were upon the earth, and took no notice, and they knew not the way of righteousness, neither have they walked in their [appointed] paths?
14 Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
But having known their works, he delivered them into darkness: and in the night one will be as a thief:
15 Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
and the eye of the adulterer has watched [for] the darkness, saying, Eye shall not perceive me, and he puts a covering on his face.
16 Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
In darkness he digs through houses: by day they conceal themselves securely: they know not the light.
17 Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
For the morning is to them all [as] the shadow of death, for [each] will be conscious of the terror of the shadow of death.
18 “Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
He is swift on the face of the water: let his portion be cursed on the earth; and let their plants be laid bare.
19 Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol h7585)
[Let them be] withered upon the earth; for they have plundered the sheaves of the fatherless. (Sheol h7585)
20 Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
Then is his sin brought to remembrance, and he vanishes like a vapour of dew: but let what he has done be recompensed to him, and let every unrighteous one be crushed like rotten wood.
21 Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
For he has not treated the barren woman well, and has had no pity on a feeble woman.
22 Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
And in wrath he has overthrown the helpless: therefore when he has arisen, [a man] will not feel secure of his own life.
23 Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
When he has fallen sick, let him not hope to recover: but let him perish by disease.
24 Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
For his exaltation has hurt many; but he has withered as mallows in the heat, or as an ear of corn falling off of itself from the stalk.
25 “Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”
But if not, who is he that says I speak falsely, and will make my words of no account?

< Ayubu 24 >