< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Then Bildad the Shuhite answered,
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
"How long will you hunt for words? Consider, and afterwards we will speak.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Why are we counted as animals, which have become unclean in your sight?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
You who tear yourself in your anger, shall the earth be forsaken for you? Or shall the rock be removed out of its place?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
"Yes, the light of the wicked shall be put out, The spark of his fire shall not shine.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
The light shall be dark in his tent. His lamp above him shall be put out.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
The steps of his strength shall be shortened. His own counsel shall cast him down.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
For he is cast into a net by his own feet, and he wanders into its mesh.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
A snare will take him by the heel. A trap will catch him.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
A noose is hidden for him in the ground, a trap for him in the way.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Terrors shall make him afraid on every side, and shall chase him at his heels.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
His strength shall be famished. Calamity shall be ready at his side.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
The members of his body shall be devoured. The firstborn of death shall devour his members.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
He shall be rooted out of his tent where he trusts. He shall be brought to the king of terrors.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
There shall dwell in his tent that which is none of his. Sulfur shall be scattered on his habitation.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
His roots shall be dried up beneath. Above shall his branch be cut off.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
His memory shall perish from the earth. He shall have no name in the street.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
He shall be driven from light into darkness, and chased out of the world.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
He shall have neither son nor grandson among his people, nor any remaining where he sojourned.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Those who come after shall be astonished at his day, as those who went before were frightened.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Surely such are the dwellings of the unrighteous. This is the place of him who doesn't know God."

< Ayubu 18 >