< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
"Look, my eye has seen all this. My ear has heard and understood it.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
What you know, I know also. I am not inferior to you.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
"Surely I would speak to Shaddai. I desire to reason with God.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
But you are forgers of lies. You are all physicians of no value.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Oh that you would be completely silent. Then you would be wise.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Hear now my reasoning. Listen to the pleadings of my lips.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Will you speak unrighteously for God, and talk deceitfully for him?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Will you show partiality to him? Will you contend for God?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Is it good that he should search you out? Or as one deceives a man, will you deceive him?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
He will surely reprove you if you secretly show partiality.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Shall not his majesty make you afraid, And his dread fall on you?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Your memorable sayings are proverbs of ashes, Your defenses are defenses of clay.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
"Be silent, leave me alone, that I may speak. Let come on me what will.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Why should I take my flesh in my teeth, and put my life in my hand?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Look, he will kill me. I have no hope. Nevertheless, I will maintain my ways before him.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
This also shall be my salvation, that a godless man shall not come before him.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Hear diligently my speech. Let my declaration be in your ears.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
See now, I have set my cause in order. I know that I am righteous.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Who is he who will contend with me? For then would I hold my peace and give up the spirit.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
"Only do not do two things to me; then I will not hide myself from your face:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
withdraw your hand far from me; and do not let your terror make me afraid.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Then call, and I will answer; or let me speak, and you answer me.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
How many are my iniquities and sins? Make me know my disobedience and my sin.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Why hide you your face, and hold me for your enemy?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Will you harass a driven leaf? Will you pursue the dry stubble?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
For you write bitter things against me, and make me inherit the iniquities of my youth:
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
You also put my feet in the stocks, and mark all my paths. You set a bound to the soles of my feet,
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
though I am decaying like a rotten thing, like a garment that is moth-eaten.

< Ayubu 13 >