< Yeremia 44 >

1 Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
La parole qui fut [adressée] à Jérémie touchant tous les Juifs qui demeuraient au pays d'Egypte, et qui habitaient à Migdol, à Taphnés, à Noph, et au pays de Patros, en disant:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
Ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: vous avez vu tout le mal que j'ai fait venir sur Jérusalem, et sur toutes les villes de Juda; et voici elles [sont] aujourd'hui un désert, et personne n'y demeure;
3 kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
A cause des maux qu'ils ont faits pour m'irriter, en allant faire des encensements pour servir d'autres dieux, lesquels ils n'ont point connus, ni eux, ni vous, ni vos pères.
4 Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
Et je vous ai envoyé tous mes serviteurs les Prophètes, me levant dès le matin, et les envoyant pour vous dire: ne commettez point maintenant cette chose abominable, laquelle je hais.
5 Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
Mais ils n'ont point écouté, et n'ont point incliné leur oreille pour se détourner de leur malice, afin de ne faire point d'encensements à d'autres dieux.
6 Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
C'est pourquoi ma fureur et ma colère s'est répandue sur eux et s'est allumée dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem, qui sont réduites en désert, [et] en désolation, comme [il paraît] aujourd'hui.
7 “Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
Maintenant donc, ainsi a dit l'Eternel, le Dieu des armées, le Dieu d'Israël: pourquoi faites-vous ce grand mal contre vous-mêmes, pour vous faire retrancher du milieu de Juda, hommes et femmes, petits enfants, et ceux qui tètent, afin qu'on ne vous laisse aucun de reste?
8 Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
En m'irritant par les œuvres de vos mains, en faisant des encensements à d'autres dieux dans le pays d'Egypte, auquel vous venez d'entrer pour y séjourner, afin que vous soyez retranchés, et que vous soyez en malédiction et en opprobre parmi toutes les nations de la terre?
9 Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
Avez-vous oublié les crimes de vos pères, et les crimes des Rois de Juda, et les crimes de leurs femmes, et vos propres crimes, et les crimes de vos femmes, qu'elles ont commis dans le pays de Juda, et dans les rues de Jérusalem?
10 Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
Jusques à ce jour ils n'ont point été affligés, ils n'ont point eu de crainte, et ils n'ont point marché en ma Loi, ni en mes ordonnances, que je vous ai proposées, et à vos pères aussi.
11 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: voici, je m'en vais tourner ma face contre vous pour vous nuire, et pour retrancher tout Juda.
12 Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
Et je prendrai le reste de ceux de Juda qui se sont préparés pour entrer au pays d'Egypte, et y séjourner, et ils seront tous consumés; ils tomberont dans le pays d'Egypte, ils seront consumés par l'épée, et par la famine, depuis le plus petit jusqu’au plus grand; ils mourront par l'épée, et par la famine; et ils seront en exécration, en étonnement, en malédiction, et en opprobre.
13 Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
Et je punirai ceux qui demeurent au pays d'Egypte, comme j'ai puni Jérusalem, par l'épée, par la famine, et par la mortalité.
14 Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
Et il n'y aura personne des restes de Juda d'entre ceux qui sont venus pour demeurer là, [c'est-à-dire], au pays d'Egypte, pour retourner au pays de Juda, auquel ils se promettent de retourner pour y demeurer, qui échappe, et qui y reste; car pas un ne retournera, sinon ceux qui se seront échappés [des autres].
15 Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
Mais tous ceux qui savaient que leurs femmes faisaient des encensements à d'autres dieux, et toutes les femmes qui étaient là en grande compagnie; et tout le peuple qui demeurait dans le pays d'Egypte, à Patros, répondirent à Jérémie, en disant:
16 “Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
Quant à la parole que tu nous as dite au Nom de l'Eternel, nous ne t'écouterons point;
17 Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
Mais nous ferons assurément tout ce qui est sorti de notre bouche en faisant des encensements à la Reine des cieux, et lui faisant des aspersions, comme nous et nos pères, nos Rois, et les principaux d'entre nous avons fait dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem, et nous avons eu alors abondamment de pain, nous avons été à notre aise, et nous n'avons point vu de mal.
18 Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
Mais depuis le temps que nous avons cessé de faire des encensements à la Reine des cieux, et de lui faire des aspersions, nous avons eu faute de tout, et nous avons été consumés par l'épée et par la famine.
19 Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
Quand nous faisions des encensements à la Reine des cieux, et quand nous lui faisions des aspersions, lui avons-nous offert à l'insu de nos maris des gâteaux sur lesquels elle était représentée, ou lui avons-nous répandu des aspersions?
20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
Alors Jérémie parla à tout le peuple, contre les hommes, et contre les femmes, et contre tout le peuple qui avait fait cette réponse, et leur dit:
21 “Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
L'Eternel ne s'est-il pas souvenu des encensements que vous avez faits dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem, vous et vos pères, vos Rois et les principaux d'entre vous, et le peuple du pays, et son cœur n'en a-t-il pas été touché?
22 Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
En sorte que l'Eternel ne l'a pu supporter davantage, à cause de la malice de vos actions, et à cause des abominations que vous avez commises; tellement que votre pays a été réduit en désert, et en étonnement, et en malédiction, sans que personne y habite, comme [il paraît] aujourd'hui.
23 Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
Parce donc que vous avez fait ces encensements, et que vous avez péché contre l'Eternel, et que vous n'avez point écouté la voix de l'Eternel, et n'avez point marché en sa Loi, ni en ses ordonnances, ni en ses témoignages, à cause de cela ce mal vous est arrivé, comme [il paraît] aujourd'hui.
24 Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
Puis Jérémie dit à tout le peuple, et à toutes les femmes: vous tous ceux de Juda, qui êtes au pays d'Egypte, écoutez la parole de l'Eternel.
25 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
Ainsi a parlé l'Eternel des armées le Dieu d'Israël, en disant: c'est vous, et vos femmes qui ont parlé par votre bouche touchant ce que vous avez accompli de vos mains, en disant: certainement nous accomplirons nos vœux que nous avons voués, en faisant des encensements à la Reine des cieux; et lui faisant des aspersions. Vous avez entièrement accompli vos vœux, et vous les avez effectués très exactement.
26 Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
C'est pourquoi écoutez la parole de l'Eternel, vous tous ceux de Juda qui demeurez au pays d'Egypte: voici, j'ai juré par mon grand Nom, a dit l'Eternel, que mon Nom ne sera plus réclamé par la bouche d'aucun de Juda, qui dise en tout le pays d'Egypte: le Seigneur l'Eternel est vivant.
27 Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
Voici, je veille contre eux pour [leur] mal, et non pour [leur] bien; et tous les hommes de Juda qui sont au pays d'Egypte seront consumés par l'épée, et par la famine, jusqu’à ce qu'il n'y en ait plus aucun.
28 Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
Et ceux qui seront échappés de l'épée retourneront du pays d'Egypte au pays de Juda en fort petit nombre, et tout le reste de ceux de Juda qui seront entrés au pays d'Egypte pour y séjourner, saura quelle est la parole qui s'accomplira, la mienne, ou la leur.
29 “‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
Et ceci vous sera pour signe, dit l'Eternel, que je vous punirai en ce lieu-ci, afin que vous sachiez que mes paroles seront infailliblement accomplies contre vous en mal.
30 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”
Ainsi a dit l'Eternel: voici, je m'en vais livrer Pharaon-Hophrah Roi d'Egypte en la main de ses ennemis, et en la main de ceux qui cherchent sa vie, comme j'ai livré Sédécias Roi de Juda en la main de Nébucadnetsar Roi de Babylone son ennemi, et qui cherchait sa vie.

< Yeremia 44 >