< Yeremia 36 >

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
La quatrième année de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole fut adressée à Jérémie par l'Éternel, en ces termes:
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
Prends un rouleau de livre, et y écris toutes les paroles que je t'ai dites contre Israël et contre Juda, et contre toutes les nations, depuis le jour où je t'ai parlé, depuis les jours de Josias jusqu'à ce jour.
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
Peut-être que, la maison de Juda entendant tout le mal que je me propose de leur faire, chacun se détournera de sa mauvaise voie, et je pardonnerai leur iniquité et leur péché.
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
Jérémie appela donc Baruc, fils de Nérija. Et Baruc écrivit, sous la dictée de Jérémie, dans le rouleau, toutes les paroles que l'Éternel lui avait dites.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
Puis Jérémie donna cet ordre à Baruc, et lui dit: Je suis retenu; je ne puis aller à la maison de l'Éternel.
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
Toi donc, vas-y, et tu liras, dans le rouleau que tu as écrit sous ma dictée, les paroles de l'Éternel aux oreilles du peuple, dans la maison de l'Éternel, le jour du jeûne. Tu les liras aussi aux oreilles de tous ceux de Juda qui seront venus de leurs villes.
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
Peut-être que leur supplication sera reçue devant l'Éternel, et qu'ils reviendront chacun de leur mauvaise voie; car la colère, la fureur que l'Éternel a prononcée contre ce peuple est grande.
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
Et Baruc, fils de Nérija, fit tout ce que lui avait ordonné Jérémie, le prophète, et lut dans le livre les paroles de l'Éternel, dans la maison de l'Éternel.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
La cinquième année de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda, le neuvième mois, on publia le jeûne devant l'Éternel, pour tout le peuple de Jérusalem, et pour tout le peuple qui venait des villes de Juda à Jérusalem.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
Alors Baruc lut dans le livre les paroles de Jérémie, dans la maison de l'Éternel, dans la chambre de Guémaria, fils de Shaphan, le secrétaire, dans le parvis supérieur, à l'entrée de la porte neuve de la maison de l'Éternel, aux oreilles de tout le peuple.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
Or, quand Michée, fils de Guémaria, fils de Shaphan, eut entendu de ce livre toutes les paroles de l'Éternel,
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
Il descendit à la maison du roi, à la chambre du secrétaire, et voici, tous les chefs étaient assis là, Élishama, le secrétaire, et Délaja, fils de Shémaja, Elnathan, fils d'Acbor, et Guémaria, fils de Shaphan, et Sédécias, fils de Hanania, et tous les chefs.
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
Et Michée leur rapporta toutes les paroles qu'il avait entendues, quand Baruc lisait dans le livre, aux oreilles du peuple.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
Alors tous les chefs envoyèrent Jéhudi, fils de Néthania, fils de Shélémia, fils de Cushi, vers Baruc, pour lui dire: Prends en ta main ce rouleau dans lequel tu as lu aux oreilles du peuple, et viens. Baruc, fils de Nérija, prit donc en sa main le rouleau et vint vers eux.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
Et ils lui dirent: Assieds-toi, et lis-le à nos oreilles. Et Baruc le lut à leurs oreilles.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
Mais il arriva qu'aussitôt qu'ils eurent entendu toutes ces paroles, ils furent effrayés entre eux, et dirent à Baruc: Nous ne manquerons pas de rapporter au roi toutes ces paroles.
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
Puis ils interrogèrent Baruc et dirent: Fais-nous savoir comment tu as écrit toutes ces paroles sous sa dictée.
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
Et Baruc répondit: Il me dictait de sa bouche toutes ces paroles, et je les écrivais dans le livre avec de l'encre.
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
Alors les chefs dirent à Baruc: Va, et cache-toi, ainsi que Jérémie, et que personne ne sache où vous êtes.
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
Puis ils allèrent vers le roi, dans la cour, après avoir déposé le rouleau dans la chambre d'Élishama, le secrétaire; et ils en rapportèrent aux oreilles du roi toutes les paroles.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
Et le roi envoya Jéhudi pour prendre le rouleau. Et quand Jéhudi l'eut pris de la chambre d'Élishama, le secrétaire, il le lut aux oreilles du roi et de tous les chefs qui se tenaient debout près de lui.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
Or le roi était assis dans la maison d'hiver, au neuvième mois, et un brasier était allumé devant lui.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
Et il arriva, quand Jéhudi eut lu trois ou quatre colonnes du livre, que le roi le coupa avec le canif du secrétaire, et le jeta au feu dans le brasier, jusqu'à ce que tout le rouleau fût entièrement consumé par le feu du brasier.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
Le roi et tous ses serviteurs, qui entendirent toutes ces paroles, n'en furent point effrayés et ne déchirèrent point leurs vêtements.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
Toutefois, Elnathan, et Délaja, et Guémaria avaient fait des instances auprès du roi, pour qu'il ne brûlât pas le rouleau; mais il ne les écouta point.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
Et le roi commanda à Jérachméel, fils de Hammélec, et à Séraja, fils d'Ozriel, et à Shélémia, fils d'Abdiel, de saisir Baruc, le secrétaire, et Jérémie, le prophète; mais l'Éternel les cacha.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
Alors la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie, en ces mots, après que le roi eut brûlé le rouleau et les paroles que Baruc avait écrites sous la dictée de Jérémie:
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
Prends un autre rouleau, et tu y écriras toutes les premières paroles qui étaient dans le premier rouleau que Jéhojakim, roi de Juda, a brûlé.
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
Et quant à Jéhojakim, roi de Juda, tu diras: Ainsi a dit l'Éternel: Tu as brûlé ce rouleau, en disant: “Pourquoi y as-tu écrit que le roi de Babylone viendra certainement, et qu'il détruira ce pays, et en exterminera les hommes et les bêtes? “
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Éternel, touchant Jéhojakim, roi de Juda: Aucun des siens ne sera assis sur le trône de David, et son cadavre sera jeté, et exposé le jour à la chaleur, et la nuit à la gelée.
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
Et je punirai sur lui, et sur sa postérité, et sur ses serviteurs, leur iniquité; et je ferai venir sur eux, et sur les habitants de Jérusalem, et sur les hommes de Juda, tout le mal que j'ai prononcé contre eux sans qu'ils m'aient écouté.
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
Jérémie prit donc un autre rouleau et le donna à Baruc, le secrétaire, fils de Nérija, qui y écrivit, sous la dictée de Jérémie, toutes les paroles du livre que Jéhojakim, roi de Juda, avait brûlé au feu; et plusieurs paroles semblables y furent encore ajoutées.

< Yeremia 36 >