< Hosea 8 >

1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
Embouche la trompette! L'ennemi fond comme un aigle sur la maison de l'Éternel, parce qu'ils ont violé mon alliance et péché contre ma loi.
2 Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
Ils crieront à moi: “Mon Dieu! Nous t'avons connu, nous, Israël! “
3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
Israël a rejeté ce qui est bon; l'ennemi le poursuivra.
4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
Ils ont fait des rois, mais non de ma part; des chefs, mais à mon insu. Ils se sont fait des dieux de leur argent et de leur or; c'est pourquoi ils seront retranchés!
5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! Hasira yangu inawaka dhidi yao. Watakuwa najisi mpaka lini?
Ton veau, ô Samarie, est rejeté! Ma colère s'est embrasée contre eux! Jusqu'à quand seront-ils incapables d'innocence?
6 Zimetoka katika Israeli! Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. Atavunjwa vipande vipande, yule ndama wa Samaria.
Car il vient d'Israël; c'est un ouvrier qui l'a fait, et il n'est point Dieu. C'est pourquoi le veau de Samarie sera mis en pièces!
7 “Wanapanda upepo na kuvuna upepo wa kisulisuli. Bua halina suke, halitatoa unga. Kama lingetoa nafaka, wageni wangeila yote.
Parce qu'ils sèment le vent, ils moissonneront la tempête. Ils n'auront point de blé debout; ce qui pousse ne donnera point de farine; et si peut-être il en donne, les étrangers la dévoreront.
8 Israeli amemezwa; sasa yupo miongoni mwa mataifa kama kitu kisicho na thamani.
Israël est dévoré. Ils sont maintenant parmi les nations comme un vase dédaigné.
9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. Efraimu amejiuza mwenyewe kwa wapenzi.
Car ils sont montés vers Assur, comme un âne sauvage qui se tient à l'écart. Éphraïm a fait des présents pour avoir des amis.
10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wataanza kudhoofika chini ya uonevu wa mfalme mwenye nguvu.
Et parce qu'ils font des présents chez les nations, je vais maintenant les rassembler, et ils commenceront à diminuer sous le fardeau du roi des princes.
11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi kwa ajili ya sadaka za dhambi, hizi zimekuwa madhabahu za kufanyia dhambi.
Parce qu'Éphraïm a multiplié les autels pour pécher, ces autels lui tourneront en piège.
12 Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi kuhusu sheria yangu, lakini wameziangalia kama kitu cha kigeni.
Que je lui multiplie mes enseignements par écrit, ils sont regardés comme une chose étrangère.
13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi nao wanakula hiyo nyama, lakini Bwana hapendezwi nao. Sasa ataukumbuka uovu wao na kuadhibu dhambi zao: Watarudi Misri.
Dans les sacrifices qui me sont offerts, ils sacrifient de la chair et la mangent; mais l'Éternel ne les agrée point. Maintenant il se souvient de leur iniquité, et il punira leur péché: ils retourneront en Égypte!
14 Israeli amemsahau Muumba wake na kujenga majumba ya kifalme, Yuda amejengea miji mingi ngome. Lakini nitatuma moto kwenye miji yao utakaoteketeza ngome zao.”
Israël a oublié celui qui l'a fait, et a bâti des palais, et Juda a multiplié les villes fortes; mais j'enverrai dans les villes de celui-ci un feu qui dévorera les palais de celui-là.

< Hosea 8 >