< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
La troisième année du règne de Jéhojakim, roi de Juda, Nébucadnetsar, roi de Babylone, vint contre Jérusalem et l'assiégea.
2 Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
Et le Seigneur livra entre ses mains Jéhojakim, roi de Juda, et une partie des vases de la maison de Dieu; et Nébucadnetsar les transporta au pays de Shinear, dans la maison de son dieu, et il mit les vases dans la maison du trésor de son dieu.
3 Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
Et le roi ordonna à Ashpénaz, chef de ses eunuques, d'amener d'entre les enfants d'Israël, de la race royale et des principaux seigneurs,
4 vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
Quelques jeunes gens en qui il n'y eût aucun défaut corporel, de belle apparence, instruits en toute sagesse, ayant de la science et pleins d'intelligence, et qui fussent capables de se tenir au palais du roi, et de leur enseigner les lettres et la langue des Caldéens.
5 Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
Et le roi leur assigna, pour chaque jour, une portion des mets de sa table et du vin dont il buvait, afin de les élever ainsi pendant trois ans, au bout desquels ils se tiendraient devant le roi.
6 Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
Il y avait parmi eux, d'entre les enfants de Juda, Daniel, Hanania, Mishaël et Azaria.
7 Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
Et le chef des eunuques leur donna d'autres noms: il donna à Daniel le nom de Beltshatsar; à Hanania celui de Shadrac; à Mishaël celui de Méshac; et à Azaria celui d'Abed-Négo.
8 Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
Or Daniel résolut dans son cœur de ne pas se souiller par les mets du roi, ni par le vin qu'il buvait; et il pria le chef des eunuques de ne pas l'obliger à se souiller.
9 Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
Et Dieu fit trouver à Daniel grâce et faveur auprès du chef des eunuques.
10 lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
Et le chef des eunuques dit à Daniel: Je crains le roi mon maître, qui a ordonné votre manger et votre boire. Pourquoi verrait-il vos visages plus défaits que ceux des jeunes gens de votre âge, et mettriez-vous ma tête en danger auprès du roi?
11 Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
Mais Daniel dit au maître d'hôtel, qui avait été établi par le chef des eunuques sur Daniel, Hanania, Mishaël et Azaria:
12 “Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
Éprouve, je te prie, tes serviteurs pendant dix jours, et qu'on nous donne des légumes à manger et de l'eau à boire;
13 Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
Après cela, tu regarderas notre visage et le visage des jeunes gens qui mangent les mets du roi; puis tu feras avec tes serviteurs selon ce que tu auras vu.
14 Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
Alors il leur accorda cela, et les éprouva pendant dix jours.
15 Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
Et au bout de dix jours, on leur vit meilleur visage et plus d'embonpoint qu'à tous les jeunes gens qui mangeaient les mets du roi.
16 Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
C'est pourquoi le maître d'hôtel enlevait les mets qui leur étaient destinés et le vin qu'ils devaient boire, et il leur donnait des légumes.
17 Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
Or Dieu donna à ces quatre jeunes gens de la science, et de l'intelligence dans toutes les lettres, et de la sagesse; et Daniel comprenait toutes sortes de visions et de songes.
18 Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
Et au bout des jours fixés par le roi pour qu'on les lui amenât, le chef des eunuques les amena devant Nébucadnetsar.
19 Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
Le roi s'entretint avec eux; et parmi eux tous, il ne s'en trouva point de tels que Daniel, Hanania, Mishaël et Azaria; et ils entrèrent au service du roi.
20 Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
Et dans toute question qui demandait de la sagesse et de l'intelligence, et sur laquelle le roi les interrogeait, il les trouvait dix fois supérieurs à tous les magiciens et astrologues qui étaient dans tout son royaume.
21 Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.
Ainsi fut Daniel jusqu'à la première année du roi Cyrus.

< Danieli 1 >