< Hosea 13 >

1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
Dès qu'Éphraïm parlait, on tremblait. Il s'était élevé en Israël. Mais il s'est rendu coupable par Baal, et il est mort.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
Et maintenant ils continuent à pécher; ils se font avec leur argent des images de fonte, des idoles de leur invention; et ce ne sont qu'ouvrages d'artisans. A leur sujet ils disent: “Que ceux qui sacrifient baisent les veaux! “
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
C'est pourquoi ils seront comme la nuée du matin, comme la rosée du matin qui bientôt se dissipe, comme la balle que le vent chasse de l'aire, comme la fumée qui s'échappe d'une fenêtre! Mais je suis l'Éternel ton Dieu dès le pays d'Égypte, et tu ne connais d'autre dieu que moi;
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
Il n'y a de sauveur que moi!
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
Je t'ai connu dans le désert, dans une terre aride.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
Ils ont été rassasiés dans leurs pâturages; ils ont été rassasiés, et leur cœur s'est élevé; c'est pourquoi ils m'ont oublié.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
Je serai donc pour eux comme un lion; comme un léopard, je les épierai sur le chemin;
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
Je les rencontrerai comme une ourse à qui l'on a enlevé ses petits. Et je déchirerai l'enveloppe de leur cœur, je les dévorerai là comme une lionne; la bête sauvage les mettra en pièces.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
Ce qui t'a perdu, ô Israël, c'est d'être contre moi, contre celui qui est ton secours.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Où est donc ton roi? Qu'il te délivre dans toutes tes villes. Où sont tes juges, au sujet desquels tu disais: Donne-moi un roi et des princes?
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
Je t'ai donné un roi dans ma colère, je te l'ôterai dans mon indignation.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
L'iniquité d'Éphraïm est liée, et son péché est réservé.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
Les douleurs de celle qui enfante lui surviendront. C'est un enfant qui n'est pas sage; car, au terme voulu, il ne se présente pas pour voir le jour.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol h7585)
Je les rachèterais de la puissance du Sépulcre; je les garantirais de la mort. O mort! je serais ta peste. O Sépulcre! je serais ta destruction. Le repentir se cache à mes yeux! (Sheol h7585)
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
Quoiqu'il ait fructifié parmi ses frères, le vent d'orient viendra, le vent de l'Éternel, montant du désert, viendra, desséchera ses sources et tarira ses fontaines. On pillera le trésor de tous ses objets précieux.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Samarie sera punie, car elle s'est rebellée contre son Dieu. Ils tomberont par l'épée; leurs petits enfants seront écrasés, et l'on fendra le ventre de leurs femmes enceintes.

< Hosea 13 >