< Ezekieli 5 >

1 “Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
Davantage toi, fils d'homme, prends-toi un couteau tranchant; prends-toi un rasoir de barbier; et fais-le passer sur ta tête, et sur ta barbe; puis tu prendras une balance à peser, et tu partageras ce [que tu auras rasé].
2 Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
Tu [en] brûleras une troisième partie dans le feu, au milieu de la ville, lorsque les jours du siège s'accompliront, et tu en prendras une autre troisième partie, [et] tu frapperas de l'épée à l'entour; et tu disperseras au vent l'autre troisième partie; car je tirerai l'épée après eux.
3 Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
Et tu en prendras de là quelque petit nombre, et les serreras aux pans de ton manteau.
4 Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
Et de ceux-là, tu en prendras encore, et les jetteras au milieu du feu, et les brûleras au feu; [et] il en sortira du feu contre toute la maison d'Israël.
5 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: c'est ici cette Jérusalem que j'avais placée au milieu des nations et des pays qui sont autour d'elle.
6 Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
Elle a changé mes ordonnances en une méchanceté pire que celle des nations, et mes statuts en une méchanceté pire que celle des pays qui sont autour d'elle; car ils ont rejeté mes ordonnances, et n'ont point marché dans mes statuts.
7 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
C'est pourquoi le Seigneur l'Eternel a dit ainsi: parce que vous avez multiplié [vos méchancetés] plus que les nations qui [sont] autour de vous, [et] que vous n'avez point marché dans mes statuts, et n'avez point observé mes ordonnances, et que vous n'avez pas même fait selon les ordonnances des nations qui sont autour de vous;
8 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
A cause de cela le Seigneur l'Eternel dit ainsi: voici, j'[en veux] à toi, oui moi-même, et j'exécuterai au milieu de toi mes jugements, devant les yeux des nations.
9 Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
Et je ferai en toi, à cause de toutes tes abominations, des choses que je ne fis jamais, et telles que je n'en ferai jamais de semblables.
10 Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
Les pères mangeront leurs enfants au milieu de toi, et les enfants mangeront leurs pères; et j'exécuterai [mes] jugements sur toi, et je disperserai à tous vents tout ce qui restera de toi.
11 Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
Et je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, parce que tu as souillé mon Sanctuaire par toutes tes infamies, et par toutes tes abominations, moi-même je te raserai, et mon œil ne t'épargnera point, et je n'en aurai point de compassion.
12 Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
Une troisième partie d'entre vous mourra de mortalité, et sera consumée par la famine au milieu de toi; et une troisième partie tombera par l'épée autour de toi; et je disperserai à tous vents l'autre troisième partie, et je tirerai l'épée après eux.
13 “Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
Car ma colère sera portée à son comble, et je ferai reposer ma fureur sur eux, et je me satisferai; et ils sauront que moi l'Eternel j'ai parlé dans ma jalousie, quand j'aurai consommé ma fureur sur eux.
14 “Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
Je te mettrai en désert et en opprobre parmi les nations qui sont autour de toi, tellement que tous les passants le verront.
15 Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
Et tu seras en opprobre, en ignominie, en instruction, et en étonnement aux nations qui sont autour de toi, quand j'aurai exécuté mes jugements sur toi, avec colère, avec fureur, et par des châtiments pleins de fureur; moi l'Eternel j'ai parlé.
16 Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
Après que j'aurai décoché sur eux les mauvaises flèches de la famine, qui seront mortelles, lesquelles je décocherai pour vous détruire, encore j'augmenterai la famine sur vous, et je vous romprai le bâton du pain.
17 Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”
Je vous enverrai la famine, et des bêtes nuisibles, qui te priveront d'enfants; et la mortalité et le sang passeront parmi toi, et je ferai venir l'épée sur toi; moi l'Eternel j'ai parlé.

< Ezekieli 5 >