< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
La troisième année de Jéhojakim Roi de Juda, Nébucadnetsar Roi de Babylone vint [contre] Jérusalem, et l'assiégea.
2 Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
Et le Seigneur livra en sa main Jéhojakim Roi de Juda, et une partie des vaisseaux de la maison de Dieu, lesquels [Nébucadnetsar] fit emporter au pays de Sinhar en la maison de son Dieu; et il mit ces vaisseaux en la Trésorerie de son Dieu.
3 Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
Et le Roi dit à Aspenaz, Capitaine de ses Eunuques, qu'il amenât d'entre les enfants d'Israël, et de la race Royale et des principaux Seigneurs,
4 vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
Quelques jeunes enfants, en qui il n'y eût aucun défaut, beaux de visage, instruits en toute sagesse, connaissant les sciences, qui eussent beaucoup d'intelligence, et en qui il y eût de la force, pour se tenir au palais du Roi; et qu'on leur enseignât les lettres et la langue des Caldéens.
5 Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
Et le Roi leur assigna pour provision chaque jour une portion de la viande Royale, et du vin dont il buvait; afin qu'on les nourrît ainsi trois ans, et qu'ensuite [quelques-uns d'entre eux] servissent en la présence du Roi.
6 Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
Entre ceux-là il y eut des enfants de Juda, Daniel, Hanania, Misaël et Hazaria.
7 Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
Mais le Capitaine des Eunuques leur mit d'autres noms; car il donna à Daniel le nom de Beltesatsar; à Hanania, celui de Sadrac; à Misaël, celui de Mésac; et à Hazaria, celui d'Habed-nego.
8 Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
Or Daniel se proposa dans son cœur de ne se point souiller par la portion de la viande du Roi, ni par le vin dont le Roi buvait; c'est pourquoi il supplia le Chef des Eunuques afin qu'il ne l'engageât point à se souiller.
9 Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
Et Dieu fit que le Chef des Eunuques eut de la bonté pour Daniel, et qu'il eut pitié de lui.
10 lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
Toutefois le Capitaine des Eunuques dit à Daniel: Je crains le Roi mon maître, qui a ordonné votre manger et votre boire; pourquoi verrait-il vos visages plus défaits que ceux des autres jeunes enfants vos semblables, et rendriez-vous ma tête coupable envers le Roi?
11 Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
Mais Daniel dit à Meltsar, qui avait été ordonné par le Capitaine des Eunuques sur Daniel, Hanania, Misaël, et Hazaria;
12 “Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
Eprouve, je te prie, tes serviteurs pendant dix jours, et qu'on nous donne des légumes à manger, et de l'eau à boire.
13 Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
Et après cela regarde nos visages, et les visages des jeunes enfants qui mangent la portion de la viande Royale; puis tu feras à tes serviteurs selon ce que tu auras vu.
14 Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
Et il leur accorda cela, et les éprouva pendant dix jours.
15 Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
Mais au bout des dix jours leurs visages parurent en meilleur état, et ils avaient plus d'embonpoint que tous les jeunes enfants qui mangeaient la portion de la viande Royale.
16 Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
Ainsi Meltsar prenait la portion de leur viande, et le vin qu'ils devaient boire, et leur donnait des légumes.
17 Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
Et Dieu donna à ces quatre jeunes enfants de la science et de l'intelligence dans toutes les lettres, et de la sagesse; et Daniel s'entendait en toute vision, et dans les songes.
18 Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
Et au bout des jours que le Roi avait dit qu'on les amenât, le Capitaine des Eunuques les amena devant Nébucadnetsar.
19 Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
Et le Roi s'entretint avec eux; mais entre eux tous il ne s'en trouva point de tels que Daniel, Hanania, Misaël, et Hazaria; et ils se tinrent en la présence du Roi.
20 Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
Et dans toute question savante et qui demandait de la pénétration, sur quoi le Roi les interrogeait il trouva dix fois plus de science en eux que dans tous les tireurs d'horoscope et les astrologues qui étaient en tout son Royaume.
21 Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.
Et Daniel [y] fut jusqu'à la première année du Roi Cyrus.

< Danieli 1 >