< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
Quand vous partagerez par le sort le pays en héritage, vous prélèverez comme offrande à l'Éternel une portion du pays, qui sera sacrée; elle sera de vingt-cinq mille cannes de long, et de dix mille de large; elle sera sacrée dans toute son étendue.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Dans cette portion, il y aura, pour le sanctuaire, cinq cents cannes sur cinq cents, formant un carré, autour duquel il y aura un rayon libre de cinquante coudées.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
Sur cet espace, de vingt-cinq mille en longueur et de dix mille en largeur, tu mesureras un emplacement pour le sanctuaire, le lieu très-saint.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
Ce sera la portion sainte du pays; elle appartiendra aux sacrificateurs qui font le service du sanctuaire, qui s'approchent de l'Éternel pour faire son service; ce sera un emplacement pour leurs maisons, et un lieu très saint pour le sanctuaire.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
Vingt-cinq mille cannes en longueur, dix mille en largeur, appartiendront aux Lévites qui font le service de la maison; ce sera leur possession, avec vingt chambres.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
Pour la possession de la ville, vous prendrez cinq mille cannes en largeur, et vingt-cinq mille en longueur, parallèlement à la portion sainte prélevée; ce sera pour toute la maison d'Israël.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
Pour le prince, vous réserverez un territoire, des deux côtés de la portion sainte prélevée et de la possession de la ville, le long de la portion sainte prélevée et de la possession de la ville, au côté de l'Occident vers l'Occident, au côté de l'Orient vers l'Orient, sur une longueur parallèle à l'une des parts, depuis la limite occidentale à la limite orientale.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
Ce sera sa terre, sa possession en Israël, et mes princes ne fouleront plus mon peuple; mais ils donneront le pays à la maison d'Israël, selon ses tribus.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Princes d'Israël, que cela vous suffise; ôtez la violence et l'oppression; faites droit et justice; enlevez vos extorsions de dessus mon peuple, dit le Seigneur, l'Éternel.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
Ayez des balances justes, un épha juste et un bath juste.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
L'épha et le bath auront la même mesure; le bath contiendra la dixième partie d'un homer, et l'épha la dixième partie d'un homer; leur mesure se réglera sur le homer.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
Le sicle aura vingt guéras; vingt sicles, plus vingt-cinq sicles, plus quinze sicles, feront la mine.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
Voici la portion que vous prélèverez: un sixième d'épha par homer de blé, et un sixième d'épha par homer d'orge;
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Pour l'huile, pour un bath d'huile, vous prélèverez un dixième de bath par cor, qui vaut un homer de dix baths; car dix baths font le homer.
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
Vous prélèverez une tête de menu bétail sur deux cents, dans les gros pâturages d'Israël, pour l'offrande, l'holocauste, les sacrifices de prospérités, afin de faire expiation pour eux, dit le Seigneur, l'Éternel.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
Tout le peuple du pays devra prélever cette offrande pour le prince d'Israël.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
Mais le prince sera tenu de fournir les holocaustes, les offrandes et les libations, aux fêtes, aux nouvelles lunes, aux sabbats, à toutes les solennités de la maison d'Israël. Il offrira le sacrifice pour le péché, l'offrande, et l'holocauste, et les sacrifices de prospérités, afin de faire propitiation pour la maison d'Israël.
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Au premier jour du premier mois, tu prendras un jeune taureau sans défaut, pour purifier le sanctuaire.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
Le sacrificateur prendra du sang de ce sacrifice pour le péché, pour en mettre sur les poteaux de la maison, sur les quatre angles de l'encadrement de l'autel, et sur les poteaux de la porte du parvis intérieur.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
Tu feras la même chose, le septième jour du mois, pour les hommes qui auront péché involontairement ou par imprudence, et vous ferez l'expiation pour la maison.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
Le quatorzième jour du premier mois, vous aurez la Pâque, fête de sept jours; on mangera des pains sans levain.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
Ce jour-là, le prince offrira pour lui et tout le peuple du pays un taureau pour le péché.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Et durant les sept jours de la fête, il offrira sept taureaux et sept béliers sans défaut, en holocauste à l'Éternel, chaque jour durant sept jours, et chaque jour un bouc en sacrifice pour le péché.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
Il offrira comme offrande un épha par taureau, et un épha par bélier, et un hin d'huile par épha.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
Le quinzième jour du septième mois, à la fête, il offrira durant sept jours les mêmes choses, le même sacrifice pour le péché, le même holocauste, les mêmes offrandes, et les mêmes mesures d'huile.

< Ezekieli 45 >