< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
La vingt-cinquième année de notre captivité, au commencement de l'année, le dixième jour du mois, quatorze ans après la prise de la ville, en ce même jour, la main de l'Éternel fut sur moi, et il m'y transporta.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
Il m'amena, en visions divines, au pays d'Israël, et me plaça sur une montagne fort haute, sur laquelle, du côté du sud, se trouvaient comme les bâtiments d'une ville.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Et après qu'il m'y eut fait entrer, voici un homme dont l'aspect était semblable à celui de l'airain; il tenait en sa main un cordeau de lin et une canne à mesurer, et il était debout à la porte.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
Cet homme me dit: Fils de l'homme, regarde de tes yeux, et écoute de tes oreilles, et fais attention à tout ce que je vais te montrer. Tu as été amené ici afin que je te les montre. Fais connaître à la maison d'Israël tout ce que tu vas voir.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Et voici, il y avait un mur extérieur, entourant la maison de tous côtés. Et l'homme, qui avait à la main une canne à mesurer de six coudées, chaque coudée mesurant une palme de plus que la coudée usuelle, mesura la largeur de la construction, qui était d'une canne, et la hauteur qui était d'une canne.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Il alla vers la porte orientale, et en monta les degrés, pour mesurer le seuil de la porte, qui avait une canne de largeur; et l'autre seuil avait une canne de largeur.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
Chaque chambre était longue d'une canne, et large d'une canne; et entre les chambres il y avait un espace de cinq coudées; et le seuil de la porte, près du vestibule de la porte, à l'intérieur, avait une canne.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Il mesura le vestibule de la porte, à l'intérieur: il avait une canne;
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Il mesura le vestibule de la porte: il avait huit coudées, et ses poteaux deux coudées; c'était le vestibule de la porte, à l'intérieur.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Les chambres de la porte orientale étaient au nombre de trois de chaque côté, toutes trois de même grandeur, et les poteaux de chaque côté avaient une même mesure.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Il mesura la largeur de l'ouverture de la porte, c'étaient dix coudées, et sa hauteur, qui était de treize coudées.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Devant les chambres, il y avait un espace d'une coudée, de côté et d'autre; et chaque chambre avait six coudées d'un côté, et six de l'autre.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Il mesura la porte, depuis le toit d'une chambre jusqu'au toit de l'autre, ce qui donnait une largeur de vingt-cinq coudées entre les deux ouvertures opposées.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Puis il fit soixante coudées pour les poteaux; et près des poteaux, un parvis tout autour de la porte.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
L'espace entre la porte d'entrée et le vestibule de la porte intérieure, était de cinquante coudées.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
Il y avait des fenêtres grillées aux chambres et à leurs poteaux, à l'intérieur de la porte, tout autour, de même qu'aux vestibules; les fenêtres étaient tout autour, à l'intérieur; et sur les poteaux étaient sculptées des palmes.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Puis il me conduisit dans le parvis extérieur, où je vis des chambres, et un dallage posé tout autour du parvis; sur ce dallage se trouvaient trente chambres.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
Le dallage s'étendait sur les côtés des portes, et répondait à leur longueur; c'était le dallage inférieur.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Il mesura la largeur depuis le devant de la porte inférieure, jusque devant le parvis intérieur, au-dehors, cent coudées à l'Orient et au Nord.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Il mesura la longueur et la largeur de la porte septentrionale du parvis extérieur.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Ses chambres, au nombre de trois par côté, et ses poteaux, et son vestibule, avaient la même mesure que la première porte: cinquante coudées en longueur, et vingt-cinq en largeur.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Ses fenêtres, son vestibule et ses palmes, avaient les mêmes mesures que la porte orientale; on y montait par sept degrés, en face desquels était son vestibule.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
Et vis-à-vis de la porte septentrionale et de la porte orientale, se trouvait la porte du parvis intérieur; d'une porte à l'autre il mesura cent coudées.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Après cela il me conduisit du côté du Sud, où je vis la porte méridionale; il en mesura les poteaux et les vestibules, qui avaient la même mesure.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Cette porte et ses vestibules avaient des fenêtres tout autour, semblables aux fenêtres précédentes; et sa longueur était de cinquante coudées, et sa largeur de vingt-cinq.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
On y montait par sept degrés, en face desquels se trouvait un vestibule; de chaque côté, il y avait des palmes sur ses poteaux.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
Le parvis intérieur avait une porte au Midi, et il mesura d'une porte à l'autre, du côté du Midi, cent coudées.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Puis il me fit entrer au parvis intérieur par la porte du Midi; il mesura la porte du Midi; elle avait les mêmes mesures.
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Ses chambres, ses poteaux et ses vestibules avaient les mêmes mesures. Cette porte et ses vestibules avaient des fenêtres tout autour; la longueur en était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
Tout autour était un vestibule de vingt-cinq coudées de long, et de cinq de large.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Les vestibules de la porte arrivaient au parvis extérieur; il y avait des palmes à ses poteaux, et huit degrés pour y monter.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Ensuite il me fit entrer au parvis intérieur du côté de l'Orient; et il en mesura la porte qui avait les mêmes mesures. Ses chambres, ses poteaux et son vestibule avaient les mêmes mesures, et cette porte et ses vestibules avaient des fenêtres tout autour.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
La longueur en était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Les vestibules de la porte arrivaient au parvis extérieur; il y avait des palmes à ses poteaux, de chaque côté, et huit degrés pour y monter.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Puis il me mena vers la porte du Nord, et la mesura; elle avait les mêmes mesures, ainsi que ses chambres, ses poteaux et ses vestibules;
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Il y avait des fenêtres tout autour; et la longueur en était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq;
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Ses vestibules arrivaient au parvis extérieur; il y avait des palmes sur ses poteaux, de chaque côté, et huit degrés pour y monter.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Il y avait une chambre qui avait ses ouvertures du côté des poteaux des portes; c'est là qu'on lavait les holocaustes.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Dans le vestibule de la porte se trouvaient deux tables, de chaque côté, pour y égorger les holocaustes pour le sacrifice pour le péché, et pour le sacrifice pour le délit.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
A l'un des côtés extérieurs, là où l'on montait, à l'entrée de la porte du Nord, étaient deux tables; à l'autre côté, vers le vestibule de la porte, deux tables.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Ainsi, quatre tables d'un côté, quatre tables de l'autre, aux côtés de la porte; ce qui fait huit tables, sur lesquelles on égorgeait les victimes.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Il y avait encore quatre tables pour l'holocauste, en pierre de taille, longues d'une coudée et demie, larges d'une coudée et demie, et hautes d'une coudée. On y déposait les instruments avec lesquels on égorgeait les victimes pour les holocaustes et les autres sacrifices.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
A la maison, tout autour, étaient fixés des crochets, larges d'une paume; et la chair des oblations devait être déposée sur les tables.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
En dehors de la porte intérieure étaient deux chambres pour les chantres, dans le parvis intérieur; l'une était à côté de la porte du Nord, et regardait le Midi; l'autre à côté de la porte Orientale, et regardait le Nord.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Il me dit: La chambre qui regarde le Midi, est pour les sacrificateurs qui font le service de la maison;
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
La chambre qui regarde le Nord, est pour les sacrificateurs qui font le service de l'autel. Ce sont les fils de Tsadok, qui, parmi les fils de Lévi, s'approchent de l'Éternel pour faire son service.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Et il mesura le parvis; il avait cent coudées de long, et cent coudées de large, en carré; l'autel se trouvait devant la maison.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Ensuite il me fit entrer dans le vestibule de la maison, et en mesura les poteaux, cinq coudées de chaque côté; la largeur de la porte était de trois coudées, de chaque côté.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
Le vestibule avait vingt coudées de long, et onze de large; on y montait par des degrés, et près des poteaux se trouvaient des colonnes, l'une d'un côté, l'autre de l'autre.

< Ezekieli 40 >