< Ezekieli 19 >

1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
Et toi, prononce une complainte sur les princes d'Israël,
2 na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
Et dis: Qu'était-ce que ta mère? Une lionne couchée au milieu des lions, et élevant ses petits au milieu des lionceaux.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
Elle éleva un de ses petits, qui devint un jeune lion; il apprit à déchirer sa proie, et dévora des hommes.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
Mais les nations en entendirent parler, et il fut pris dans leur fosse; et, après lui avoir mis des boucles aux narines, elles l'emmenèrent au pays d'Égypte.
5 “‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
Quand la lionne vit qu'elle attendait en vain, que tout son espoir était perdu, elle prit un autre de ses petits, et en fit un jeune lion.
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
Il marcha parmi les lions, et devint un jeune lion; il apprit à déchirer sa proie, et dévora des hommes;
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
Il désolait leurs palais, et détruisait leurs villes; le pays avec tout ce qu'il contient fut frappé de stupeur à l'ouïe de son rugissement.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
Contre lui se rangèrent les nations de toutes les contrées voisines, et elles jetèrent sur lui leurs filets; il fut pris dans leur fosse.
9 Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
Elles le mirent en cage, avec des boucles aux narines; puis elles l'emmenèrent auprès du roi de Babylone, et le conduisirent dans une forteresse, afin qu'on n'entendît plus sa voix sur les montagnes d'Israël.
10 “‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
Ta mère était, comme toi, semblable à une vigne plantée près des eaux; elle était chargée de fruits et de sarments, grâce à l'abondance des eaux.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
Elle avait de vigoureux rameaux pour des sceptres de souverains; par son élévation elle atteignait jusqu'aux branches touffues; elle attirait les regards par sa hauteur et par l'abondance de ses rameaux.
12 Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
Mais elle fut arrachée avec fureur et jetée par terre; le vent d'orient a desséché son fruit; ses rameaux vigoureux ont été brisés et desséchés;
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
Le feu les a dévorés, et maintenant elle est plantée dans le désert, dans une terre sèche et aride.
14 Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
Le feu est sorti d'un rameau de ses branches et a consumé son fruit, et elle n'a plus de rameau vigoureux pour un sceptre de roi. Telle est la complainte, et elle servira de complainte.

< Ezekieli 19 >