< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
Tu feras aussi l'autel en bois de Sittim, cinq coudées de long, et cinq coudées de large; l'autel sera carré, et sa hauteur sera de trois coudées.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
Et tu feras à ses quatre coins des cornes qui sortiront de l'autel; et tu le couvriras d'airain.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
Tu feras ses chaudrons pour ôter ses cendres, et ses pelles, et ses coupes, et ses fourchettes, et ses encensoirs; et tu feras tous ses ustensiles en airain.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
Tu lui feras une grille en treillis d'airain, et tu feras au treillis quatre anneaux d'airain, à ses quatre coins.
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
Et tu le mettras sous la corniche de l'autel, depuis le bas, et le treillis s'élèvera jusqu'au milieu de l'autel.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
Tu feras aussi des barres pour l'autel, des barres de bois de Sittim, et tu les couvriras d'airain.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
Et on fera entrer les barres dans les anneaux; et les barres seront aux deux côtés de l'autel, quand on le portera.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
Tu le feras creux, en planches; on le fera tel qu'il t'a été montré sur la montagne.
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
Tu feras aussi le parvis de la Demeure. Pour le côté du Sud, vers le Midi, il y aura pour le parvis des tentures en fin lin retors, de cent coudées de long pour un côté;
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Et vingt colonnes et leurs vingt soubassements d'airain; les clous des colonnes et leurs tringles, en argent.
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Et de même, pour le côté du Nord, il y aura dans la longueur, cent coudées de tentures, et vingt colonnes et leurs vingt soubassements d'airain; les clous des colonnes et leurs tringles, en argent.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
La largeur du parvis, du côté de l'Occident, sera de cinquante coudées de tentures, qui auront dix colonnes et leurs dix soubassements.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
Et la largeur du parvis, du côté de devant, vers l'Orient, sera de cinquante coudées:
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
A l'un des côtés, il y aura quinze coudées de tentures, avec leurs trois colonnes et leurs trois soubassements;
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Et à l'autre côté, quinze coudées de tentures, leurs trois colonnes et leurs trois soubassements.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
Il y aura aussi, pour la porte du parvis, une tapisserie de vingt coudées, en pourpre, écarlate, cramoisi et fin lin retors, en ouvrage de broderie, leurs quatre colonnes et leurs quatre soubassements.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
Toutes les colonnes autour du parvis seront jointes par des tringles d'argent; leurs clous seront d'argent, et leurs soubassements d'airain.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
La longueur du parvis sera de cent coudées; la largeur, de cinquante de chaque côté, et la hauteur, de cinq coudées; il sera de fin lin retors, et les soubassements seront d'airain.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
Quant à tous les ustensiles de la Demeure, pour tout son service, et tous ses pieux, et tous les pieux du parvis, ils seront d'airain.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
Et tu commanderas aux enfants d'Israël qu'ils t'apportent de l'huile pure d'olives broyées, pour le luminaire, afin de tenir la lampe continuellement allumée.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
Dans le tabernacle d'assignation, en dehors du voile qui est devant le Témoignage, Aaron avec ses fils l'arrangera, pour luire en la présence de l'Éternel, depuis le soir jusqu'au matin. Ce sera pour leurs générations une ordonnance perpétuelle, qui sera observée par les enfants d'Israël.

< Kutoka 27 >