< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Et tu feras la Demeure de dix tentures de fin lin retors, de pourpre, d'écarlate, et de cramoisi, avec des chérubins que tu feras en ouvrage d'art.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
La longueur d'une tenture sera de vingt-huit coudées, et la largeur de la même tenture de quatre coudées; toutes les tentures auront une même mesure.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Cinq tentures seront jointes l'une à l'autre, et les cinq autres tentures seront aussi jointes l'une à l'autre.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
Tu feras aussi des lacets de pourpre sur le bord de la première tenture, au bout de l'assemblage; et tu feras de même au bord de la dernière tenture, dans le second assemblage.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Tu feras cinquante lacets à la première tenture, et tu feras cinquante lacets au bout de la tenture qui sera dans le second assemblage. Les lacets seront en face l'un de l'autre.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
Tu feras cinquante crochets d'or, et tu joindras les tentures l'une à l'autre avec les crochets, pour que la Demeure forme un seul tout.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Tu feras aussi des tentures de poil de chèvre, pour servir de tabernacle sur la Demeure. Tu feras onze de ces tentures.
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
La longueur d'une tenture sera de trente coudées, et la largeur de la même tenture de quatre coudées; les onze tentures auront une même mesure.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
Et tu joindras cinq de ces tentures à part, et les six autres tentures à part; mais tu redoubleras la sixième tenture sur le devant du tabernacle.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Tu feras aussi cinquante lacets sur le bord de la première tenture, la dernière de l'assemblage, et cinquante lacets sur le bord de la tenture du second assemblage.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Tu feras aussi cinquante crochets d'airain, et tu feras entrer les crochets dans les lacets, et tu assembleras ainsi le tabernacle, pour qu'il forme un seul tout.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
Mais le surplus qui flottera des tentures du tabernacle, savoir la moitié de la tenture qui sera de reste, flottera sur le derrière de la Demeure.
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
Et la coudée d'un côté, et la coudée de l'autre, de ce qui sera de reste dans la longueur des tentures du tabernacle, sera flottant sur les flancs de la Demeure, d'un côté et de l'autre, pour la couvrir.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Tu feras aussi pour le tabernacle une couverture de peaux de bélier teintes en rouge, et une couverture de peaux de couleur d'hyacinthe par-dessus.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Et tu feras pour la Demeure des planches en bois de Sittim, qu'on fera tenir debout.
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
La longueur d'une planche sera de dix coudées, et la largeur de la même planche d'une coudée et demie.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Il y aura deux tenons à chaque planche, parallèles l'un à l'autre; tu feras de même pour toutes les planches de la Demeure.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
Tu feras donc les planches pour la Demeure: vingt planches du côté du Sud, vers le Midi.
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
Et sous les vingt planches tu feras quarante soubassements d'argent: deux soubassements sous une planche, pour ses deux tenons, et deux soubassements sous une autre planche, pour ses deux tenons.
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
Et tu feras vingt planches pour l'autre côté de la Demeure, du côté du Nord,
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Et leurs quarante soubassements d'argent; deux soubassements sous une planche, et deux soubassements sous une autre planche.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Tu feras six planches pour le fond de la Demeure vers l'Occident.
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
Tu feras aussi deux planches pour les angles de la Demeure, au fond.
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
Elles seront doubles par le bas, mais en même temps elles seront pleines par le haut jusqu'au premier anneau; il en sera ainsi pour toutes les deux; elles seront pour les deux angles.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Il y aura donc huit planches et leurs seize soubassements d'argent; deux soubassements sous une planche, et deux soubassements sous une autre planche.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
Tu feras aussi cinq traverses de bois de Sittim, pour les planches d'un côté de la Demeure;
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
Et cinq traverses pour les planches de l'autre côté de la Demeure; et cinq autres traverses pour les planches du côté de la Demeure formant le fond, vers l'Occident.
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
Et la traverse du milieu, qui sera au milieu des planches, ira d'un bout à l'autre.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
Tu couvriras d'or les planches et tu feras leurs anneaux d'or, pour y mettre les traverses; et tu couvriras d'or les traverses.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Tu dresseras donc la Demeure selon la forme qui t'en a été montrée sur la montagne.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Et tu feras un voile de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors; on le fera en ouvrage d'art, avec des chérubins.
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
Et tu le mettras sur quatre colonnes de bois de Sittim couvertes d'or; leurs clous seront en or; elles reposeront sur quatre soubassements d'argent.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
Et tu mettras le voile sous les crochets des tentures; et là, en dedans du voile, tu feras entrer l'arche du Témoignage; et le voile séparera pour vous le lieu saint d'avec le lieu très-saint.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
Et tu poseras le propitiatoire sur l'arche du Témoignage dans le lieu très-saint.
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
Et tu mettras la table en dehors du voile, et le chandelier vis-à-vis de la table, du côté de la Demeure qui sera vers le Midi; et tu placeras la table du côté du Nord.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Et pour l'entrée du tabernacle tu feras une tapisserie de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors, en ouvrage de broderie.
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
Et tu feras pour cette tapisserie cinq colonnes de bois de Sittim, que tu couvriras d'or; leurs clous seront en or; et tu leur fondras cinq soubassements d'airain.

< Kutoka 26 >