< 2 Wafalme 9 >

1 Nabii Elisha akamwita mtu mmoja kutoka kwa wana wa manabii na kumwambia, “Jikaze viuno, uichukue hii chupa ya mafuta, na uende Ramoth-Gileadi.
Alors Élisée, le prophète, appela un des fils des prophètes et lui dit: Ceins tes reins, prends en ta main cette fiole d'huile, et va-t'en à Ramoth de Galaad.
2 Ukifika huko, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi. Enda kwake, umtenge na wenzake, na umpeleke katika chumba cha ndani.
Quand tu y seras arrivé, regarde où sera Jéhu, fils de Josaphat, fils de Nimshi; puis entre et, l'ayant fait lever d'avec ses frères, tu le feras entrer dans quelque chambre secrète.
3 Kisha chukua hii chupa na umimine mafuta juu ya kichwa chake, nawe utangaze, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ Kisha ufungue mlango na ukimbie; usikawie!”
Tu prendras alors la fiole d'huile, tu la verseras sur sa tête et tu diras: Ainsi a dit l'Éternel: Je t'ai oint roi sur Israël! Puis, tu ouvriras la porte, et tu t'enfuiras sans attendre.
4 Basi yule kijana nabii akaenda Ramoth-Gileadi.
Ainsi le jeune homme, le serviteur du prophète, s'en alla à Ramoth de Galaad.
5 Wakati alipofika, akawakuta maafisa wa jeshi wameketi pamoja, akasema, “Nina ujumbe wako, ee jemadari.” Yehu akauliza, “Kwa yupi miongoni mwetu?” Akamjibu, “Kwako wewe, jemadari.”
Quand il arriva, voici, les capitaines de l'armée étaient assis; et il dit: J'ai à te parler, capitaine. Et Jéhu dit: A qui de nous tous? A toi, capitaine.
6 Yehu akainuka na kuingia ndani ya nyumba. Ndipo yule nabii akamimina mafuta juu ya kichwa cha Yehu na kutangaza, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Bwana, yaani Israeli.
Alors Jéhu se leva et entra dans la maison. Et le jeune homme lui versa l'huile sur la tête, et lui dit: Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Je t'ai oint roi sur le peuple de l'Éternel, sur Israël!
7 Inakupasa uiangamize nyumba ya bwana wako Ahabu, nami nitalipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Bwana iliyomwagwa na Yezebeli.
Tu frapperas la maison d'Achab, ton seigneur; et je vengerai sur Jésabel le sang de mes serviteurs les prophètes, et le sang de tous les serviteurs de l'Éternel.
8 Nyumba yote ya Ahabu itaangamia. Nitamkatilia mbali kila mzaliwa wa kiume wa Ahabu katika Israeli, aliye mtumwa ama aliye huru.
Et toute la maison d'Achab périra; et je retrancherai à Achab jusqu'à un seul homme, tant ce qui est serré que ce qui est abandonné en Israël;
9 Nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama ile nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama ile nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
Et je mettrai la maison d'Achab dans le même état que la maison de Jéroboam, fils de Nébat, et que la maison de Baesha, fils d'Achija.
10 Kuhusu Yezebeli, mbwa watamla kwenye kiwanja huko Yezreeli, wala hakuna mtu atakayemzika.’” Kisha akafungua mlango na kukimbia.
Les chiens mangeront aussi Jésabel dans le champ de Jizréel, et il n'y aura personne qui l'ensevelisse. Puis le jeune homme ouvrit la porte, et s'enfuit.
11 Yehu alipotoka nje na kurudi kwenda kwa maafisa wenzake, mmoja wao akamuuliza, “Je, kila kitu ni salama? Kwa nini huyu mwenye wazimu alikuja kwako?” Yehu akajibu, “Wewe unamfahamu huyo mtu, na aina ya mambo ambayo yeye husema.”
Alors Jéhu sortit vers les serviteurs de son seigneur. Et on lui dit: Tout va-t-il bien? Pourquoi cet insensé est-il venu vers toi? Il leur répondit: Vous connaissez l'homme et ses discours.
12 Wakasema, “Hiyo siyo kweli! Tuambie.” Yehu akasema, “Haya ndiyo aliyoniambia: ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’”
Mais ils dirent: C'est faux! Déclare-nous-le donc! Et il dit: Il m'a parlé de telle et telle sorte, disant: Ainsi a dit l'Éternel: Je t'ai oint roi sur Israël.
13 Wakaharakisha kuvua mavazi yao, na kuyatandaza chini ya Yehu ili akanyage juu kwenye ngazi ya nje. Kisha wakapiga tarumbeta na kupaza sauti wakisema, “Yehu ni mfalme!”
Alors ils prirent à la hâte chacun leurs vêtements, les mirent sous lui, au plus haut des degrés, sonnèrent de la trompette, et dirent: Jéhu est roi!
14 Basi Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, akafanya shauri baya dhidi ya Yoramu. (Wakati huu, Yoramu na Israeli wote walikuwa wakiilinda Ramoth-Gileadi dhidi ya Hazaeli mfalme wa Aramu,
Ainsi Jéhu, fils de Josaphat, fils de Nimshi, fit une conjuration contre Joram. Or, Joram gardait Ramoth de Galaad, lui et tout Israël, contre Hazaël, roi de Syrie.
15 lakini Mfalme Yoramu alikuwa amerudishwa Yezreeli ili kujiuguza kutokana na majeraha ambayo Waaramu walimtia katika vita na Hazaeli mfalme wa Aramu.) Yehu akasema, “Kama hii ndiyo nia yenu, msimruhusu hata mmoja kutoroka nje ya mji kwenda kupeleka habari huko Yezreeli.”
Et le roi Joram était revenu se faire guérir à Jizréel des blessures que les Syriens lui avaient faites, quand il combattait contre Hazaël, roi de Syrie. Et Jéhu dit: Si vous le trouvez bon, que personne ne sorte ni n'échappe de la ville pour aller en porter avis à Jizréel.
16 Ndipo Yehu akaingia katika gari lake la vita na kuendesha kwenda Yezreeli, kwa sababu Yoramu alikuwa amepumzika huko, na Ahazia mfalme wa Yuda alikuwa ameenda kumwona.
Alors Jéhu monta sur son char, et s'en alla à Jizréel, car Joram y était alité; et Achazia, roi de Juda, y était descendu pour visiter Joram.
17 Mlinzi aliyesimama juu ya kinara cha Yezreeli alipoona askari wa Yehu wanakuja, akaita akisema, “Naona askari wanakuja.” Yoramu akaamuru, “Mtwae mpanda farasi umtume akakutane nao na kuuliza, ‘Je, mmekuja kwa amani?’”
Or la sentinelle qui se tenait sur la tour, à Jizréel, vit venir la troupe de Jéhu, et dit: Je vois une troupe de gens. Et Joram dit: Prends un cavalier, et envoie-le au-devant d'eux, et qu'il dise: Y a-t-il paix?
18 Mpanda farasi akaondoka kwenda kukutana na Yehu na kusema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme: ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Yehu akamjibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.” Mlinzi akatoa habari, “Mjumbe amewafikia lakini harudi.”
Et le cavalier s'en alla au-devant de lui, et dit: Ainsi dit le roi: Y a-t-il paix? Jéhu répliqua: Qu'as-tu à faire de paix? Passe derrière moi. Et la sentinelle le rapporta, et dit: Le messager est allé jusqu'à eux, et il ne revient point.
19 Basi mfalme akamtuma mpanda farasi wa pili. Wakati alipowafikia akasema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme, ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Yehu akajibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”
Et on envoya un second cavalier, qui vint à eux et dit: Ainsi dit le roi: Y a-t-il paix? Jéhu répliqua: Qu'as-tu à faire de paix? Passe derrière moi.
20 Yule mlinzi akatoa taarifa akasema, “Mjumbe amewafikia, lakini hata yeye harudi. Uendeshaji ule ni kama wa Yehu mwana wa Nimshi, anaendesha kama mwenye wazimu!”
La sentinelle le rapporta encore, et dit: Il est allé jusqu'à eux, et il ne revient point; mais la manière de conduire a l'air de celle de Jéhu, fils de Nimshi; car il mène avec furie.
21 Yoramu akaagiza, akasema, “Weka tayari gari langu la vita.” Na baada ya gari kuwa tayari, Yoramu mfalme wa Israeli, na Ahazia mfalme wa Yuda, wakaondoka kila mmoja kwenye gari lake ili kukutana na Yehu. Walikutana naye katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli.
Alors Joram dit: Attelle! Et on attela son char. Ainsi Joram, roi d'Israël, sortit avec Achazia, roi de Juda, chacun dans son char, et ils s'avancèrent à la rencontre de Jéhu, et le rencontrèrent dans le champ de Naboth, le Jizréélite.
22 Yoramu alipomwona Yehu akauliza, “Je, Yehu, umekuja kwa amani?” Yehu akajibu, “Kunawezaje kuwa na amani wakati ibada za sanamu na uchawi wa mama yako Yezebeli ungaliko?”
Et dès que Joram eut vu Jéhu, il dit: Y a-t-il paix, Jéhu? Mais Jéhu répondit: Quelle paix, tandis que les prostitutions de Jésabel, ta mère, et ses enchantements sont en si grand nombre?
23 Yoramu akageuka nyuma na kukimbia, akimwambia Ahazia, “Huu ni uhaini, Ahazia!”
Alors Joram tourna bride et s'enfuit, en disant à Achazia: Trahison, Achazia!
24 Kisha Yehu akatwaa upinde wake na kumchoma Yoramu katikati ya mabega. Mshale ukapenya kwenye moyo wake, naye akaanguka ghafula ndani ya gari lake.
Mais Jéhu saisit l'arc à pleine main, et frappa Joram entre les épaules, de sorte que la flèche lui traversa le cœur, et qu'il s'affaissa sur ses genoux dans son char.
25 Yehu akamwambia Bidkari, mwendeshaji wa gari lake, “Mwinue na umtupe katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. Kumbuka jinsi mimi na wewe tulivyokuwa tukiendesha pamoja magari yetu nyuma ya Ahabu baba yake, wakati Bwana alipotoa unabii huu kumhusu:
Et Jéhu dit à Bidkar, son officier: Prends-le, et le jette dans le champ de Naboth, le Jizréélite. Car souviens-toi que, lorsque nous étions à cheval, moi et toi, l'un auprès de l'autre, à la suite d'Achab, son père, l'Éternel prononça contre lui cet oracle:
26 ‘Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya wanawe, nami kwa hakika nitakufanya uilipe juu ya shamba hili, asema Bwana.’ Sasa basi, mwinue na umtupe juu ya kiwanja, kulingana na neno la Bwana.”
Aussi vrai que je vis hier le sang de Naboth et le sang de ses fils, dit l'Éternel, aussi vrai je te le rendrai dans ce champ, dit l'Éternel. C'est pourquoi, maintenant prends-le et le jette dans ce champ, selon la parole de l'Éternel.
27 Wakati Ahazia mfalme wa Yuda alipoona kilichotokea, akakimbia kupitia barabara ya Beth-Hagani. Yehu akamkimbiza akipaza sauti na kusema, “Muue naye pia!” Wakamjeruhi katika gari lake kwenye njia ielekeayo Guri karibu na Ibleamu, lakini akatorokea Megido na akafia huko.
Et Achazia, roi de Juda, ayant vu cela, s'enfuit vers le pavillon du jardin; mais Jéhu le poursuivit, et dit: Frappez-le aussi sur son char! Ce fut à la montée de Gur, près de Jibléam. Puis Achazia s'enfuit à Méguiddo, et y mourut.
28 Watumishi wake wakambeba kwa gari la vita na kumpeleka Yerusalemu, wakamzika pamoja na baba zake kwenye kaburi lake katika Mji wa Daudi.
Et ses serviteurs le transportèrent sur un char à Jérusalem et l'ensevelirent dans son tombeau avec ses pères, dans la cité de David.
29 (Katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu, Ahazia alianza kutawala katika Yuda.)
Or Achazia avait commencé à régner sur Juda la onzième année de Joram, fils d'Achab.
30 Kisha Yehu akaenda Yezreeli. Yezebeli aliposikia habari hii, akayapaka macho yake rangi, akatengeneza nywele zake na kutazama nje dirishani.
Puis Jéhu vint à Jizréel. Et Jésabel, l'ayant appris, farda ses yeux, orna sa tête, et se mit à la fenêtre.
31 Yehu alipokuwa akiingia langoni, Yezebeli akasema, “Je, umekuja kwa amani, Zimri, wewe muuaji wa bwana wako?”
Et comme Jéhu passait la porte, elle dit: En a-t-il bien pris à Zimri qui assassina son maître?
32 Yehu akaangalia juu dirishani na kuita, “Je, ni nani aliye upande wangu? Ni nani?” Matowashi wawili au watatu wakamtazama.
Aussitôt il leva la tête vers la fenêtre et dit: Qui est pour moi? qui? Et deux ou trois eunuques se penchèrent vers lui.
33 Yehu akasema, “Mtupeni huyo mwanamke chini!” Kwa hiyo wakamtupa chini, nayo baadhi ya damu yake ikatapanyika ukutani na nyingine juu ya farasi walipokuwa wakimkanyaga kwa miguu yao.
Et il leur dit: Jetez-la en bas! Et ils la jetèrent, de sorte qu'il rejaillit de son sang contre la muraille et contre les chevaux; et il la foula aux pieds.
34 Yehu akaingia ndani, akala na akanywa. Akasema, “Mshughulikieni huyo mwanamke aliyelaaniwa. Mzikeni, kwa sababu alikuwa binti wa mfalme.”
Et, étant entré, il mangea et but. Puis il dit: Allez voir maintenant cette maudite, et ensevelissez-la; car elle est fille de roi.
35 Lakini walipotoka kwenda kumzika, hawakukuta kitu chochote isipokuwa fuvu la kichwa, miguu yake na mikono.
Ils y allèrent donc pour l'ensevelir; mais ils ne trouvèrent d'elle que le crâne, les pieds et les paumes des mains.
36 Wakarudi na kumwambia Yehu, ambaye alisema, “Hili ndilo neno la Bwana alilosema kupitia kinywa cha mtumishi wake Eliya Mtishbi, kwamba: Katika kiwanja cha Yezreeli, mbwa wataikula nyama ya Yezebeli.
Et, étant retournés, ils le lui rapportèrent. Alors il dit: C'est la parole que l'Éternel a prononcée par son serviteur Élie, le Thishbite, en disant: Dans le champ de Jizréel les chiens mangeront la chair de Jésabel;
37 Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mavi shambani katika uwanja wa Yezreeli, kwamba hakutakuwepo mtu atakayeweza kusema, ‘Huyu ndiye Yezebeli.’”
Et le cadavre de Jésabel sera, dans le champ de Jizréel, comme du fumier sur la campagne, de sorte qu'on ne pourra point dire: C'est ici Jésabel.

< 2 Wafalme 9 >