< 2 Nyakati 24 >

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
Joas était âgé de sept ans quand il devint roi, et il régna quarante ans à Jérusalem; sa mère s'appelait Tsibia, de Béer-Shéba.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
Joas fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, pendant toute la vie de Jéhojada, le sacrificateur.
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
Et Jéhojada lui donna deux femmes, dont il eut des fils et des filles.
4 Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
Après cela Joas eut la pensée de réparer la maison de l'Éternel.
5 Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
Il assembla donc les sacrificateurs et les Lévites, et leur dit: Allez par les villes de Juda, et amassez de l'argent par tout Israël, pour réparer la maison de votre Dieu d'année en année, et hâtez cette affaire. Mais les Lévites ne se hâtèrent point.
6 Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
Alors le roi appela Jéhojada, leur chef, et lui dit: Pourquoi n'as-tu pas veillé à ce que les Lévites apportassent, de Juda et de Jérusalem, l'impôt que Moïse, serviteur de l'Éternel, mit sur l'assemblée d'Israël, pour le tabernacle du témoignage?
7 Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
Car l'impie Athalie et ses enfants ont ravagé la maison de Dieu; et même ils ont employé pour les Baals toutes les choses consacrées à la maison de l'Éternel.
8 Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
Et le roi ordonna qu'on fît un coffre, et qu'on le mît à la porte de la maison de l'Éternel, en dehors.
9 Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
Puis on publia dans Juda et dans Jérusalem, qu'on apportât à l'Éternel l'impôt mis par Moïse, serviteur de Dieu, sur Israël dans le désert.
10 Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
Tous les chefs et tout le peuple s'en réjouirent, et ils apportèrent leur tribut, et jetèrent dans le coffre, jusqu'à ce qu'il fût plein.
11 Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
Or, quand c'était le moment d'apporter le coffre à l'inspection du roi, par l'entremise des Lévites, et que ceux-ci voyaient qu'il y avait beaucoup d'argent, un secrétaire du roi et un commissaire du principal sacrificateur venaient et vidaient le coffre; puis ils le rapportaient et le remettaient à sa place. Ils faisaient ainsi jour après jour, et ils recueillaient de l'argent en abondance.
12 Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
Le roi et Jéhojada le donnaient à ceux qui étaient chargés de l'ouvrage pour le service de la maison de l'Éternel, et ceux-ci louaient des tailleurs de pierres et des charpentiers pour réparer la maison de l'Éternel, et aussi des ouvriers en fer et en airain, pour réparer la maison de l'Éternel.
13 Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
Ceux qui étaient chargés de l'ouvrage travaillèrent donc, et par leurs soins, l'œuvre fut réparée; de sorte qu'ils rétablirent la maison de Dieu en son état, et la consolidèrent.
14 Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
Lorsqu'ils eurent achevé, ils apportèrent devant le roi et devant Jéhojada le reste de l'argent, dont il fit faire des ustensiles pour la maison de l'Éternel, des ustensiles pour le service et pour les holocaustes, des coupes et d'autres ustensiles d'or et d'argent. Et on offrit continuellement des holocaustes dans la maison de l'Éternel, tant que vécut Jéhojada.
15 Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
Or Jéhojada devint vieux et rassasié de jours, et il mourut; il était âgé de cent trente ans quand il mourut.
16 Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
On l'ensevelit dans la cité de David avec les rois; car il avait fait du bien à Israël, et à l'égard de Dieu et de sa maison.
17 Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
Mais, après que Jéhojada fut mort, les principaux de Juda vinrent et se prosternèrent devant le roi; alors le roi les écouta.
18 Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
Et ils abandonnèrent la maison de l'Éternel, le Dieu de leurs pères, et ils servirent les emblèmes d'Ashéra et les idoles; et la colère de l'Éternel fut sur Juda et sur Jérusalem, parce qu'ils s'étaient ainsi rendus coupables.
19 Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
Et l'Éternel envoya parmi eux, pour les faire retourner à lui, des prophètes qui témoignèrent contre eux; mais ils ne voulurent point les écouter.
20 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
Alors l'Esprit de Dieu revêtit Zacharie, fils de Jéhojada, le sacrificateur, et, se tenant debout au-dessus du peuple, il leur dit: Dieu a dit ainsi: Pourquoi transgressez-vous les commandements de l'Éternel? Vous ne prospérerez point; car vous avez abandonné l'Éternel, et il vous abandonnera.
21 Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Mais ils conspirèrent contre lui, et l'assommèrent de pierres, par le commandement du roi, dans le parvis de la maison de l'Éternel.
22 Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
Ainsi le roi Joas ne se souvint point de la bonté dont Jéhojada, père de Zacharie, avait usé envers lui; et il tua son fils, qui dit en mourant: L'Éternel le voit, et il en demandera compte!
23 Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
Et il arriva, quand l'année fut révolue, que l'armée de Syrie monta contre Joas, et vint en Juda et à Jérusalem. Or les Syriens détruisirent, d'entre le peuple, tous les principaux du peuple, et ils envoyèrent au roi, à Damas, tout leur butin.
24 Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
Bien que ce fût avec un petit nombre d'hommes qu'arrivât l'armée de Syrie, l'Éternel livra entre leurs mains une très nombreuse armée, parce qu'ils avaient abandonné l'Éternel, le Dieu de leurs pères. Ainsi les Syriens firent justice de Joas.
25 Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
Et quand ils se furent éloignés de lui, après l'avoir laissé dans de grandes souffrances, ses serviteurs conspirèrent contre lui, à cause du sang des fils de Jéhojada, le sacrificateur; ils le tuèrent sur son lit, et il mourut. On l'ensevelit dans la cité de David; mais on ne l'ensevelit pas dans les tombeaux des rois.
26 Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
Et ce sont ici ceux qui conspirèrent contre lui: Zabad, fils de Shimeath, femme ammonite, et Jozabad, fils de Shimrith, femme moabite.
27 Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Quant à ses fils et à la grande charge qui lui fut imposée, et à la restauration de la maison de Dieu, voici, ces choses sont écrites dans les mémoires sur le livre des rois. Amatsia, son fils, régna à sa place.

< 2 Nyakati 24 >