< 2 Nyakati 24 >

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
Joas était âgé de sept ans quand il commença à régner, et il régna quarante ans à Jérusalem. Sa mère avait nom Tsibia, [et] elle était de Béer-sebah.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
Or Joas fit ce qui est droit devant l'Eternel, durant tout le temps de Jéhojadah le Sacrificateur.
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
Et Jéhojadah lui donna deux femmes, desquelles il eut des fils et des filles.
4 Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
Après cela Joas prit à cœur de renouveler la maison de l'Eternel.
5 Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
Et il assembla les Sacrificateurs et les Lévites, et leur dit: Allez par les villes de Juda, et amassez de l'argent de tout Israël, pour réparer la maison de votre Dieu, d'année en année, et hâtez cette affaire; mais les Lévites ne la hâtèrent point.
6 Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
Et le Roi appela Jéhojadah le principal [Sacrificateur], et lui dit: Pourquoi n'as-tu pas fait en sorte que les Lévites apportassent de Juda, et de Jérusalem, et de tout Israël, le tribut ordonné par Moïse serviteur de l'Eternel, pour le Tabernacle du Témoignage?
7 Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
Car la méchante Hathalie [et] ses enfants avaient dépouillé la maison de Dieu, et ils avaient même approprié aux Bahalins toutes les choses consacrées à la maison de l'Eternel.
8 Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
C'est pourquoi le Roi commanda qu'on fit un coffre, et qu'on le mît à la porte de la maison de l'Eternel en dehors.
9 Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
Puis on publia dans Juda et dans Jérusalem, qu'on apportât à l'Eternel l'impôt que Moïse serviteur de Dieu avait mis dans le désert sur Israël.
10 Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
Et tous les principaux et tout le peuple s'en réjouirent; et ils apportèrent [l'argent], et le jetèrent dans le coffre, jusqu'à ce qu'on eût achevé [de réparer le Temple].
11 Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
Or quand les Lévites emportaient le coffre suivant l'ordre du Roi, ce qu'on faisait dès qu'on voyait qu'il y avait beaucoup d'argent; le Secrétaire du Roi, et le Commis du principal Sacrificateur venaient, et vidaient le coffre, puis ils le reportaient, et le remettaient en sa place Ils faisaient ainsi tous les jours; et on amassa quantité d'argent.
12 Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
Et le Roi et Jéhojadah le distribuaient à ceux qui avaient la charge de l'ouvrage du service de la maison de l'Eternel, lesquels louaient des tailleurs de pierres et des charpentiers pour refaire la maison de l'Eternel, et des ouvriers travaillant en fer et en airain pour réparer la maison de l'Eternel.
13 Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
Ceux donc qui avaient la charge de l'ouvrage travaillèrent, et il fut entièrement achevé par leur moyen, de sorte qu'ils rétablirent la maison de Dieu en son état, et l'affermirent.
14 Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
Et dès qu'ils eurent achevé, ils apportèrent devant le Roi et devant Jéhojadah le reste de l'argent, dont il fit faire des ustensiles pour la maison de l'Eternel; [savoir] des ustensiles pour le service et pour les oblations, et des tasses et d'autres ustensiles d'or et d'argent; et ils offrirent continuellement des holocaustes dans la maison de l'Eternel, durant tout le temps de Jéhojadah.
15 Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
Or Jéhojadah étant devenu vieux et rassasié de jours, mourut. Il était âgé de cent trente ans quand il mourut.
16 Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
Et on l'ensevelit en la Cité de David avec les Rois, parce qu'il avait fait du bien en Israël, envers Dieu, et envers sa maison.
17 Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
Mais après que Jéhojadah fut mort, les principaux de Juda vinrent, et se prosternèrent devant le Roi; [et] alors le Roi les écouta.
18 Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
Et ils abandonnèrent la maison de l'Eternel le Dieu de leurs pères, et [s'attachèrent] au service des bocages, et des faux dieux; c'est pourquoi la colère de [l'Eternel s'alluma] contre Juda et contre Jérusalem, parce qu'ils s'étaient rendus coupables en cela.
19 Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
Et quoiqu'il leur envoyât des Prophètes pour les faire retourner à l'Eternel, et que [ces Prophètes] les [en] sommassent, toutefois ils ne voulurent point écouter.
20 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
Et même l'Esprit de Dieu revêtit Zacharie fils de Jéhojadah le Sacrificateur, de sorte qu'il se tint debout au dessus du peuple, et leur dit: Dieu a dit ainsi: Pourquoi transgressez-vous les commandements de l'Eternel? Car vous ne prospérerez point; [et] parce que vous avez abandonné l'Eternel, il vous abandonnera aussi.
21 Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Et ils se liguèrent contre lui, et l'assommèrent de pierres, par le commandement du Roi, au parvis de la maison de l'Eternel;
22 Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
De sorte que le Roi Joas ne se souvint point de la gratuité dont Jéhojadah, père de Zacharie, avait usé envers lui; mais il tua son fils, qui en mourant dit: Que l'Eternel le voie, et le redemande!
23 Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
Et il arriva qu'au bout d'un an l'armée de Syrie monta contre lui, et vint en Juda et à Jérusalem, et [les Syriens] détruisirent d'entre le peuple tous les principaux du peuple, et envoyèrent au Roi à Damas tout leur butin.
24 Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
Et quoique l'armée venue de Syrie fût peu nombreuse, l'Eternel livra pourtant entre leurs mains une très-grosse armée, parce qu'ils avaient abandonné l'Eternel Dieu de leurs pères. Ainsi [les Syriens] mirent Joas pour un exemple de jugement.
25 Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
Et quand ils se furent retirés d'avec lui, parce qu'ils l'avaient laissé dans de grandes langueurs, ses serviteurs conjurèrent contre lui, à cause du meurtre des fils de Jéhojadah le Sacrificateur, et le tuèrent sur son lit; et ainsi il mourut, et on l'ensevelit en la Cité de David, mais on ne l'ensevelit point aux sépulcres des Rois.
26 Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
Et ce sont ici ceux qui conjurèrent contre lui, Zabad, fils de Simhat femme Hammonite, et Jéhozabad fils de Simrith femme Moabite.
27 Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Or quant à ses enfants, et à la grande levée de deniers qui avait été faite pour lui, et au rétablissement de la maison de Dieu, voilà, ces choses sont écrites dans les Mémoires du Livre des Rois; et Amatsia son fils régna en sa place.

< 2 Nyakati 24 >