< 2 Nyakati 20 >

1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
Après ces choses les enfants de Moab, et les enfants de Hammon vinrent, car les Hammonites s'étaient joints aux Moabites pour faire la guerre à Josaphat.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
Et on vint faire ce rapport à Josaphat, en disant: Il est venu contre toi une grande multitude de gens, des quartiers de delà la mer, [et] de Syrie; et voici ils sont à Hatsa-tson-tamar, qui est Henguedi.
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
Alors Josaphat craignit, et se disposa à rechercher l'Eternel, et publia le jeûne par tout Juda.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
Ainsi Juda fut assemblé pour demander du secours à l'Eternel; et on vint de toutes les villes de Juda pour invoquer l'Eternel.
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
Et Josaphat se tint debout en l'assemblée de Juda et de Jérusalem dans la maison de l'Eternel, au devant du nouveau parvis.
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
Et il dit: Ô Eternel! Dieu de nos pères, n'es-tu pas le Dieu qui es aux cieux, et qui domines sur tous les Royaumes des nations? et certes en ta main est la force et la puissance, de sorte que nul ne peut te résister.
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
N'est-ce pas toi, ô notre Dieu! qui as dépossédé les habitants de ce pays de devant ton peuple d'Israël; et qui l'as donné pour toujours à la postérité d'Abraham, lequel t'aimait?
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
De sorte qu'ils y ont habité, et t'y ont bâti un Sanctuaire pour ton Nom, en disant:
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
S'il nous arrive quelque mal, [savoir] l'épée de la vengeance, ou la peste, ou la famine, nous nous tiendrons devant cette maison et en ta présence; parce que ton Nom est en cette maison, nous crierons à toi à cause de notre angoisse, tu nous exauceras, et tu nous délivreras.
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
Or maintenant voici, les enfants de Hammon et de Moab, et ceux du mont de Séhir, parmi lesquels tu ne permis point aux enfants d'Israël de passer quand ils venaient du pays d'Egypte, car ils se détournèrent d'eux, et ils ne les détruisirent point;
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
Voici, pour nous récompenser, ils viennent nous chasser de ton héritage, que tu nous as fait posséder.
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
Ô notre Dieu! ne les jugeras-tu pas? vu qu'il n'y a point de force en nous [pour subsister] devant cette grande multitude qui vient contre nous, et nous ne savons ce que nous devons faire; mais nos yeux sont sur toi.
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
Et tous ceux de Juda se tenaient debout devant l'Eternel, avec leurs familles, leurs femmes, et leurs enfants.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
Alors l'Esprit de l'Eternel fut sur Jahaziël, fils de Zacharie, fils de Bénéia, fils de Jéhiël, fils de Mattania Lévite d'entre les enfants d'Asaph, au milieu de l'assemblée.
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
Et il dit: Vous tous de Juda, et vous qui habitez à Jérusalem, et toi, Roi Josaphat, soyez attentifs. L'Eternel vous parle ainsi: Ne craignez point, et ne soyez point effrayés à cause de cette grande multitude; car ce ne sera pas à vous de conduire cette guerre, mais à Dieu.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
Descendez demain vers eux; voici, ils vont monter par la montée de Tsits, et vous les trouverez au bout du torrent, vis-à-vis du désert de Jéruël.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Ce ne sera point à vous à combattre dans cette bataille, présentez-vous, tenez-vous debout, et voyez la délivrance que l'Eternel vous va donner. Juda et Jérusalem, ne craignez point, et ne soyez point effrayés; sortez demain au devant d'eux, car l'Eternel sera avec vous.
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
Alors Josaphat s'inclina le visage contre terre, et tout Juda et les habitants de Jérusalem se jetèrent devant l'Eternel, se prosternant devant l'Eternel.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
Et les Lévites d'entre les enfants des Kéhathites, et d'entre les enfants des Corites, se levèrent pour louer d'une voix haute et éclatante l'Eternel le Dieu d'Israël.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
Puis ils se levèrent de grand matin, et sortirent vers le désert de Tékoah, et comme ils sortaient, Josaphat se tenant debout, dit: Juda, et vous habitants de Jérusalem, écoutez-moi. Croyez en l'Eternel votre Dieu, et vous serez en sûreté; croyez ses Prophètes, et vous prospérerez.
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
Puis ayant consulté avec le peuple, il établit des gens pour chanter à l'Eternel et pour louer sa sainte magnificence, [lesquels] marchant devant l'armée, disaient: Célébrez l'Eternel, car sa gratuité demeure à toujours.
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Et à l'heure qu'ils commencèrent le chant du triomphe et la louange, l'Eternel mit des embûches contre les enfants de Hammon, les Moabites, et ceux du mont de Séhir, qui venaient contre Juda, de sorte qu'ils furent battus.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
Car les enfants de Hammon et les Moabites s'élevèrent contre les habitants du mont de Séhir, pour les détruire à la façon de l'interdit, et pour les exterminer; et quand ils eurent achevé d'exterminer les habitants de Séhir, ils s'aidèrent l'un l'autre à se détruire mutuellement.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
Et ceux de Juda vinrent jusqu'à l'endroit de Mitspa au désert, et regardant vers cette multitude, voilà, c'étaient tous des corps abattus par terre, sans qu'il en fût échappé un seul.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
Ainsi Josaphat et son peuple vinrent pour piller leur butin, et ils trouvèrent de grandes richesses parmi les morts, et des hardes précieuses, et ils en prirent tant, qu'ils n'en pouvaient plus porter; ils pillèrent le butin pendant trois jours, car il y en avait en abondance.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
Puis au quatrième jour ils s'assemblèrent dans la vallée [appelée] de bénédiction, parce qu'ils bénirent là l'Eternel; c'est pourquoi on a appelé ce lieu-là, la vallée de bénédiction, jusqu'à ce jour.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
Et tous les hommes de Juda et de Jérusalem, et Josaphat marchant le premier, tournèrent visage pour revenir à Jérusalem avec joie: car l'Eternel les avait remplis de joie à cause de leurs ennemis.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
Et ils entrèrent à Jérusalem dans la maison de l'Eternel, avec des musettes, des violons, et des trompettes.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
Et la frayeur de Dieu fut sur tous les Royaumes de ce pays-là, quand ils eurent appris que l'Eternel avait combattu contre les ennemis d'Israël.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
Ainsi le Royaume de Josaphat fut en repos, parce que son Dieu lui donna du repos tout à l'entour.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Josaphat donc régna sur Juda. Il était âgé de trente-cinq ans quand il commença à régner, et il régna vingt-cinq ans à Jérusalem; sa mère avait nom Hazuba, et elle était fille de Silhi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
Il suivit la voie d'Asa son père, et ne s'en détourna point, faisant ce qui est droit devant l'Eternel.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Toutefois les hauts lieux ne furent point ôtés, parce que le peuple n'avait pas encore disposé son cœur envers le Dieu de ses pères.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
Or le reste des faits de Josaphat, tant les premiers que les derniers, voilà ils sont écrits dans les Mémoires de Jéhu fils de Hanani, selon qu'il a été enregistré au Livre des Rois d'Israël.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
Après cela Josaphat Roi de Juda se joignit à Achazia Roi d'Israël, qui ne s'employait qu'à faire du mal.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
Et il s'associa avec lui pour faire des navires et pour les envoyer en Tarsis; et ils firent ces navires à Hetsjonguéber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
Alors Elihézer fils de Dodava, de Marésa, prophétisa contre Josaphat, en disant: Parce que tu t'es joint à Achazia, l'Eternel a détruit tes ouvrages. Les navires donc furent brisés, et ils ne purent point aller en Tarsis.

< 2 Nyakati 20 >