< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
Josaphat, son fils, régna à sa place, et se fortifia contre Israël.
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
Il mit des troupes dans toutes les villes fortes de Juda, et des garnisons dans le pays de Juda, et dans les villes d'Éphraïm qu'Asa, son père, avait prises.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
Et l'Éternel fut avec Josaphat, parce qu'il suivit les premières voies de David, son père, et qu'il ne rechercha point les Baalim;
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
Car il rechercha le Dieu de son père, et il marcha dans ses commandements, et non pas selon ce que faisait Israël.
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
L'Éternel affermit donc le royaume entre ses mains; et tout Juda apportait des présents à Josaphat, et il eut richesse et gloire en abondance.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
Son cœur s'enhardit dans les voies de l'Éternel, et il ôta encore de Juda les hauts lieux et les emblèmes d'Ashéra.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
Puis, la troisième année de son règne, il envoya ses chefs Benhaïl, Obadia, Zacharie, Nathanaël et Micaja, pour enseigner dans les villes de Juda;
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
Et avec eux les Lévites Shémaja, Néthania, Zébadia, Asaël, Shémiramoth, Jonathan, Adonija, Tobija et Tob-Adonija, Lévites, et avec eux Élishama et Joram, sacrificateurs.
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
Ils enseignèrent en Juda, ayant avec eux le livre de la loi de l'Éternel. Ils firent le tour de toutes les villes de Juda, et enseignèrent parmi le peuple.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
Et la terreur de l'Éternel fut sur tous les royaumes des pays qui entouraient Juda, et ils ne firent point la guerre à Josaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
Même de chez les Philistins on apportait des présents à Josaphat, et un tribut d'argent; et les Arabes lui amenèrent aussi du bétail, sept mille sept cents béliers, et sept mille sept cents boucs.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
Ainsi Josaphat alla grandissant jusqu'au plus haut degré. Et il bâtit en Juda des châteaux et des villes à magasins.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
Il fit de grands travaux dans les villes de Juda; et il avait des gens de guerre, hommes vaillants, à Jérusalem.
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
Et voici leur dénombrement, selon les maisons de leurs pères. Les chefs de milliers de Juda furent: Adna, le chef, avec trois cent mille vaillants guerriers.
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
A côté de lui, Jochanan, le chef, avec deux cent quatre-vingt mille hommes.
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
A côté de lui, Amasia, fils de Zicri, qui s'était volontairement offert à l'Éternel, avec deux cent mille vaillants guerriers.
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
De Benjamin, Éliada, vaillant guerrier, avec deux cent mille hommes, armés de l'arc et du bouclier;
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
A côté de lui Jéhozabad, avec cent quatre-vingt mille hommes équipés pour l'armée.
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
Tels sont ceux qui étaient au service du roi, outre ceux que le roi avait mis dans les villes fortes, dans tout Juda.

< 2 Nyakati 17 >